Mfalme Daudi
Senior Member
- Dec 23, 2011
- 110
- 245
NAANDIKA KWA NIABA YA DADA YANGU MMOJA MUHANGA ANAYEPITIA HILI,NIMEONA NISHEE ILI KUPATA USHAURI WA PAMOJA JINSI YA KUMSAIDIA.
Tulikutana Facebook na ni Mwaka wa nne sasa tangu tufahamiane,alikua akisoma chuo Songea ila kwao ni Dar. Tukaanza urafiki na kuwa wapenzi, akamaliza chuo wakati huo nikiwa nimeajiriwa kwenye hotel Mirerani Manyara. Baada ya kumaliza akawa hana kazi, nikampambania akapata kazi duka moja la nguo akaja Arusha akawa akifanya kazi huku anaishi kwa Uncle wangu.
Akasema ile kazi haiwezi anahitaji kufanya kazi aliyosomea(Alisomea Ualimu). Nikampambania akapata kazi shule fulani iko hapa Arusha nje kidogo ya mji. Akafanya ile kazi kwa mwaka mzima tukawa tuko vizuri kidogo kimaisha,akaondoka kwa uncle akapanga nyumba akaanza kujitegemea, nikawa nikipata nafasi naenda nakaa siku 2, narudi kazini.Kuna Mkopo nilikopa kama laki 8, akaniongezea nikanunua kiwanja huko ngaramtoni nikaandika kwa jina langu mwanzo na la kwake mwisho.
Nikaweka tumaini langu kwake nikiamini ndio mwanaume wa maisha,nikampeleka nyumbani kumtambulisha kwa mama akawa anajulikana,ila mimi skuwahi wajua familia wala ndugu zake aliniahidi siku moja tungesafiri kwenda kwao kunitambulisha.
Tukaanza fanya mambo ya kimaendeleo,sehemu niko hamna umeme Nikamwambia nataka kufunga sola za mkopo akanipa hela nikaenda chukua ya 2M na Laki 6 unalipa kwa mwaka mmoja na nusu nikawa naonesha mpira kwa kutoza kiingilio,nikafungua na mgahawa mdogo nikaacha kazi niliyokua nafanya nikawa nimejiajiri mwenyewe,kiukweli tulikua vizuri.
Mwaka Jana mwezi wa 10 nikapata msiba Mwanza nikasafiri nikakaa kule kama mwezi. Kurudi mwenzangu nikawa kama simuelewi,kabadilika akaniambia ''Mi Nataka Mtoto'',Kwakuwa nilikua nampenda na tulishaanza kufanya maisha nikamwambia hilo halina tatizo sababu nilimwona ni Mwanaume anayejali na sikua na shaka juu ya hilo.
Nikabeba mimba,nilipomwambia akaanza kubadilika kitabia akawa simu anapiga kwa siku mara moja au asipige kabisa. Nikachunguza nikagundua tayari alikua ashapata mwanamke mwingine.
Kuna siku akaja kwangu akaniambia anataka kusafiri aende kwao nikamwambia sawa,kumbe aliiba ile hati ya kiwanja akaenda kukiuza. Akanitumia tu massage ''kanipa zawadi ya mtoto'' nikaanza kumtafuta sikumpata hewani, ile shule aliyokua anafundisha nikaenda wakaniambia alishaacha kazi,mpaka sasa sijui aliko.
Kinachonichanganya zaidi ameniacha na Mimba ya miezi 6 mpaka sasa, nina madeni ya kulipa kuanzia lile la sola nalipa kwa siku 3600/-Tsh na rejesho la ule mkopo wa laki 8, nalipia kila jumatatu 38,000/-Tsh natakiwa kulipa kodi ya chumba nakaa 40,000/Tsh na frem ya ule mgahawa nilifungua Mimba inaenda mwezi wa 7 sasa, sina akiba yoyote ndani,Mama yangu anaumwa na ananitegemea mtaji umekata, Mpaka sasa nimechanganyikiwa nashindwa la kufanya! Naomba ushauri wa kimawazo nifanye nini?
Tulikutana Facebook na ni Mwaka wa nne sasa tangu tufahamiane,alikua akisoma chuo Songea ila kwao ni Dar. Tukaanza urafiki na kuwa wapenzi, akamaliza chuo wakati huo nikiwa nimeajiriwa kwenye hotel Mirerani Manyara. Baada ya kumaliza akawa hana kazi, nikampambania akapata kazi duka moja la nguo akaja Arusha akawa akifanya kazi huku anaishi kwa Uncle wangu.
Akasema ile kazi haiwezi anahitaji kufanya kazi aliyosomea(Alisomea Ualimu). Nikampambania akapata kazi shule fulani iko hapa Arusha nje kidogo ya mji. Akafanya ile kazi kwa mwaka mzima tukawa tuko vizuri kidogo kimaisha,akaondoka kwa uncle akapanga nyumba akaanza kujitegemea, nikawa nikipata nafasi naenda nakaa siku 2, narudi kazini.Kuna Mkopo nilikopa kama laki 8, akaniongezea nikanunua kiwanja huko ngaramtoni nikaandika kwa jina langu mwanzo na la kwake mwisho.
Nikaweka tumaini langu kwake nikiamini ndio mwanaume wa maisha,nikampeleka nyumbani kumtambulisha kwa mama akawa anajulikana,ila mimi skuwahi wajua familia wala ndugu zake aliniahidi siku moja tungesafiri kwenda kwao kunitambulisha.
Tukaanza fanya mambo ya kimaendeleo,sehemu niko hamna umeme Nikamwambia nataka kufunga sola za mkopo akanipa hela nikaenda chukua ya 2M na Laki 6 unalipa kwa mwaka mmoja na nusu nikawa naonesha mpira kwa kutoza kiingilio,nikafungua na mgahawa mdogo nikaacha kazi niliyokua nafanya nikawa nimejiajiri mwenyewe,kiukweli tulikua vizuri.
Mwaka Jana mwezi wa 10 nikapata msiba Mwanza nikasafiri nikakaa kule kama mwezi. Kurudi mwenzangu nikawa kama simuelewi,kabadilika akaniambia ''Mi Nataka Mtoto'',Kwakuwa nilikua nampenda na tulishaanza kufanya maisha nikamwambia hilo halina tatizo sababu nilimwona ni Mwanaume anayejali na sikua na shaka juu ya hilo.
Nikabeba mimba,nilipomwambia akaanza kubadilika kitabia akawa simu anapiga kwa siku mara moja au asipige kabisa. Nikachunguza nikagundua tayari alikua ashapata mwanamke mwingine.
Kuna siku akaja kwangu akaniambia anataka kusafiri aende kwao nikamwambia sawa,kumbe aliiba ile hati ya kiwanja akaenda kukiuza. Akanitumia tu massage ''kanipa zawadi ya mtoto'' nikaanza kumtafuta sikumpata hewani, ile shule aliyokua anafundisha nikaenda wakaniambia alishaacha kazi,mpaka sasa sijui aliko.
Kinachonichanganya zaidi ameniacha na Mimba ya miezi 6 mpaka sasa, nina madeni ya kulipa kuanzia lile la sola nalipa kwa siku 3600/-Tsh na rejesho la ule mkopo wa laki 8, nalipia kila jumatatu 38,000/-Tsh natakiwa kulipa kodi ya chumba nakaa 40,000/Tsh na frem ya ule mgahawa nilifungua Mimba inaenda mwezi wa 7 sasa, sina akiba yoyote ndani,Mama yangu anaumwa na ananitegemea mtaji umekata, Mpaka sasa nimechanganyikiwa nashindwa la kufanya! Naomba ushauri wa kimawazo nifanye nini?