Nilijifunza siwezi kuongea negative ya mtu yeyote kwa lugha yoyote, ni kheri nimwambie usoni

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,272
Huyu mama ni mtanzania anaishi London wengi tulimzoea kama aunt, alikwenda miaka ya 70 na mume wake kimasomo lakini baada ya hapo wazungu walimpa baba kazi. Wamelea vijana wengi wanaokwenda kusoma Uingereza kwa muda mrefu.

Ilitokea katika vijana waliokuwa wanawaangalia alimaliza shule kama dentists, alioa dada wa kizungu, alifungua dental practice yake maeneo ya Exeter kwa wale wanaojua Uingereza. Sasa nikiwa mwanafunzi aunt alipata mualiko kutoka kwa dentist, anabatiza mtoto wake wa kwanza.

Alimualika baba yake mzazi kutoka TZ, baba alishukia Heathrow, dentist alimuelekeza baba jinsi ya kufika Exeter kwa train kutokea Paddington. Aunt aliniomba nimsindikize kwenye shughuli, basi tulichukua train Paddington, kiti tulichokaa kilitazamana na kiti alichokaa huyu mzee kutoka TZ. Aunt kuanza kulalamika Kiswahili, mzee ananuka sana, sijui watu wengine hawajui deodorant? Mzee wa watu hakujibu wala hakuongea.

Ilikuwa safari ya takriban masaa matatu. Tulipofika kituo chetu na yule mzee alishuka. Dentist alipofika akamkumbatia yule mzee, akatufahamisha kwa baba yake, aunt yangu pa kuweka sura hakupaona. Kibaya zaidi kwa siku tatu tulizokaa pale kila asubuhi aunt hakuweza kumwangalia yule mzee usoni.

Nilijifunza siwezi kuongea negative ya mtu yeyote kwa lugha yoyote ni kheri nimwambie usoni.
 
Dunia nzima, kila mtu ansababu zake kwa hivyo alivyo usiwazage kusikiliza maneno ya mtu juu ya mtu wala kumshuku, muhimu ni kumfuata na kumuuliza usoni kwa nini yupo vile alivyo, why one does what he does? Believe me or not people have their reasons.
 
Dunia nzima, kila mtu ansababu zake kwa hivyo alivyo usiwazage kusikiliza maneno ya mtu juu ya mtu wala kumshuku, muhimu ni kumfuata na kumuuliza usoni kwa nini yupo vile alivyo, why one does what he does? Believe me or not people have their reasons.

No ile dhana ya kufikiri huyu haelewi Kiswahili, jamani aunt yangu aliumbuka sana.
 
Iliwahi tutokea mi na mwenza kwenye gari, tukiwa na kababy ketu kachanga tunakashobokea, mmama mmoja akatuelekeza namma ya kumhandle vizuri. Kiukweli tulijifanya kumshukuru ila hapo hapo tukamteta kwa kilugha kuwa ana kimbelembele na kujipendekeza. Baada ya nusu saa alipigiwa simu akawa anajibu kwa lugha ile tulomteta nayo, eh wacha tuhangaike. we sirudiii ng'o
 
Funzo zuri
Hata kuongeongea kilugha ovyo bila kujua uko na nani.
Mfano nimewahi kupanda daladala kiti cha nyuma Niko katikati ya wamamawawili. Mmoja anamwambia kwa lugha ambayo naifahamu japo sio yangu kuwa, kanisani huwa anaiba sadaka kila akipewa jukumu LA kukusanya kwa sababu yeye hana kazi. Sasa mazingira anayoyasema nayajua na hata reference ya siku aliyotoa nilikuwepo.

Ulimi ni kama usukani Wa meli, ukikosea kidogo Unaweza kukuzamisha meli yote.
 
Funzo zuri
Hata kuongeongea kilugha ovyo bila kujua uko na nani.
Mfano nimewahi kupanda daladala kiti cha nyuma Niko katikati ya wamamawawili. Mmoja anamwambia kwa lugha ambayo naifahamu japo sio yangu kuwa, kanisani huwa anaiba sadaka kila akipewa jukumu LA kukusanya kwa sababu yeye hana kazi. Sasa mazingira anayoyasema nayajua na hata reference ya siku aliyotoa nilikuwepo.

Ulimi ni kama usukani Wa meli, ukikosea kidogo Unaweza kukuzamisha meli yote.

Mungu alitaka kumuumbua, kama unaissue kama hiyo kweli unafungua mdomo?
 
Kuna siku jamaa wawili walikua wanamsema MTU mwingine aliyekua na tumbo kubwa, yule jamaa kwa bahati akapita pale karibu yao, wakasema tena ona tumbo lilivyokua kubwa sijui anakula vitu gani? Jamaa akawatazama akatabasamu kisha akawasalimia kwa ile lugha waliyokua wanamsema kuhusu tumbo lake.
 
Kuna kanuni moja japo ni ngumu kuitekeleza lakini inaweza kukuepusha na matatizo mengi sana, hii haijalishi unatumia lugha gani...
"If you can't say something good about someone, shut up ".

Sijui kama nimepatia kunukuu lakini maudhui ni hayo.

Somo zuri sana mleta Uzi, ubarikiwe.
 
Tatizo sisi waafrika "Moyo" Upo ndani "ngozi" ipo nje. Kwa tafsiri lahisi "sisi ni wanafiki"

Wenzetu "weupe" ngozi ipo ndani na moyo upo "Nje" tafsiri wao ni wakweli kwa kiasi kikubwa. Kama mdomo unanuka anakwambia.
 
Iliwahi tutokea mi na mwenza kwenye gari, tukiwa na kababy ketu kachanga tunakashobokea, mmama mmoja akatuelekeza namma ya kumhandle vizuri. Kiukweli tulijifanya kumshukuru ila hapo hapo tukamteta kwa kilugha kuwa ana kimbelembele na kujipendekeza. Baada ya nusu saa alipigiwa simu akawa anajibu kwa lugha ile tulomteta nayo, eh wacha tuhangaike. we sirudiii ng'o
Ha ha ha.... Umenchekesha sana, mimi niliingia duka flani kuchagua viatu vya watoto, kwa kuwa walikuwa skuli basi nilikuwa nakadiria size itakayowatosha, so nilichagua sana, Basi wakaanza kunisema kwa kilugha chao ambacho nakijua A-Z, eti huyu mwanamke anachagua hivi anataka kuondoka na duka au? Mwenzake kadakia hawa ndo chuma ulete, viatu vyote alivyoshika vinahamia kwake.. Teh. Wakiwa wanaendelea kuniteta nikampigia mtu simu nikaongea naye kilugha, wakaanza kuangaliana na kujikosha, eti dada kumbe na wewe ni mwenzetu, tusamehe mwaya tumekusema vibaya
 
Kweli.Mi nilisikia watu wakimsema ndugu yangu kwenye daladala nikaenda kumchana basi wale watu mpaka kesho hawajui alijuaje istoshe hawanifahamu mi nilisikia jina lake.Never speak ill of anyone!
 
Kuna kanuni moja japo ni ngumu kuitekeleza lakini inaweza kukuepusha na matatizo mengi sana, hii haijalishi unatumia lugha gani...
"If you can't say something good about someone, shut up ".

Sijui kama nimepatia kunukuu lakini maudhui ni hayo.

Somo zuri sana mleta Uzi, ubarikiwe.
2016 - 1.jpg
 
Back
Top Bottom