Nilifurahi kwa kuwa niliweza kumsaidia japo aliniacha na maswali yasiyo na majibu.

Stephen Ngalya Chelu

JF-Expert Member
Oct 31, 2017
7,621
16,372
Nikiwa ndani ya moja ya daladala zinazofanya safari zake huko jijini 'Daslam', alikuja mzee mmoja akakaa pembeni yangu. Mazungumzo yetu yakawa hivi:

Mzee: Asalam aleykum (sijui ndo huwa inaandikwa hivi!?)

Mimi: Salama, shikamoo...(Nilimjibu hivi kwa sababu hiyo salamu aliyonisalimia huwa nashindwa kuijibu kiufasaha)

Mzee: Marahaba. (Kimya kidogo) Samahani kijana, wewe ni muislamu?

Mimi: Hapana

Yeye: (kimya kidogo) Wewe ni Mzanzibari?

Mimi: hapana.

Yeye: Sawa. (kimya kirefu kidogo) Samahani kijana, ninaelekea Bagamoyo lakini sina nauli ya kunifikisha. Kwa hiyo nilikuwa naomba kama unaweza unisaidie nauli tu ili niweze kufika.

Mimi: Ni kiasi gani hadi kufika unakoelekea?

Alitaja, nikatoa pesa nikampa. Alishukuru na kuniombea baraka kwa Mungu kisha baada ya kama nusu dakika hivi akahama siti na kwenda kukaa siti nyingine.

Nilifurahi kwa kuwa niliweza kumsaidia japo aliniacha na maswali yasiyo na majibu. Siku zote maisha hutuacha na maswali yasiyo na majibu.
 
Nikiwa ndani ya moja ya daladala zinazofanya safari zake huko jijini 'Daslam', alikuja mzee mmoja akakaa pembeni yangu. Mazungumzo yetu yakawa hivi:

Mzee: Asalam aleykum (sijui ndo huwa inaandikwa hivi!?)

Mimi: Salama, shikamoo...(Nilimjibu hivi kwa sababu hiyo salamu aliyonisalimia huwa nashindwa kuijibu kiufasaha)

Mzee: Marahaba. (Kimya kidogo) Samahani kijana, wewe ni muislamu?

Mimi: Hapana

Yeye: (kimya kidogo) Wewe ni Mzanzibari?

Mimi: hapana.

Yeye: Sawa. (kimya kirefu kidogo) Samahani kijana, ninaelekea Bagamoyo lakini sina nauli ya kunifikisha. Kwa hiyo nilikuwa naomba kama unaweza unisaidie nauli tu ili niweze kufika.

Mimi: Ni kiasi gani hadi kufika unakoelekea?

Alitaja, nikatoa pesa nikampa. Alishukuru na kuniombea baraka kwa Mungu kisha baada ya kama nusu dakika hivi akahama siti na kwenda kukaa siti nyingine.

Nilifurahi kwa kuwa niliweza kumsaidia japo aliniacha na maswali yasiyo na majibu. Siku zote maisha hutuacha na maswali yasiyo na majibu.
Hao ni wahuni tu. Huyo haendi hata mbali anashukia kituo cha mbele tu anapanda gari jingine na kuendelea kuomba.

Tena usipowapa sometimes wanakuwa wakali.
 
Hao ni wahuni tu. Huyo haendi hata mbali anashukia kituo cha mbele tu anapanda gari jingine na kuendelea kuomba.

Tena usipowapa sometimes wanakuwa wakali.
Inawezekana pia maana hata wahuni nao huwa wanazeeka, ila niliwiwa kumsaidia tu japo sio mara zote naweza kumpa pesa mtu yeyote akiniomba hata kama ninayo. Sometime nakuwa bandidu.
 
Wapo wengi sana hao siku hizi, wanaji "update" kila siku na njia mpya za kuomba.
 
Hongera kwa kutoa pesa yako kwa chuma ulete...usisahau kuweka uzi part 2
 
Wapo wengi sana.
Ila mi hawa ambao wanapata vibali vya wakuu wa serikali kama vile ma Afisa Tawala ili wapate kuomba misaada kwa shida zao ndo nashindwa pia kuwaelewa vizuri.
Wanakuwa na either watoto ama majeraha makubwa hadi unashangaa anawezaje kutembea.
Lakini anyway, tunatoa Mungu ndio mwamuzi!!!
 
Mkuu apo ulipigwa.. Usishangae tena ukaja kukutana nea kwenye daladala
Hata kama alitaka kunipiga, kulikuwa na ulazima gani wa kuniuliza maswali hayo yahusuyo dini na ukanda? Au ndo version mpya kama gia ya kuinhilia!!😀😀😀
 
Hongera kwa kutoa pesa yako kwa chuma ulete...usisahau kuweka uzi part 2
😀 😀 😀 😀
Halafu pesa niliyobeba ilikuwa imebalance na mizunguko yangu, hivyo ikabidi baadhi ya vitu nisivifanye. Sometimes huruma inaweza kukuponza mara mbili.
 
Mzee: Marahaba. (Kimya kidogo) Samahani kijana, wewe ni muislamu?



Mimi: Hapana



Yeye: (kimya kidogo) Wewe ni Mzanzibari?



Mimi: hapana.



japo aliniacha na maswali yasiyo na majibu.

Mkuu mbona maswali uliyajibu au alikuachia mengine kwenye karatasi Kama homework?
Kitu nachojiuliza ni kuwa kulikuwa na ulazima gani kuniuliza kuhusu dini na ukanda kabla hajaomba msaada?
 
Hata kama alitaka kunipiga, kulikuwa na ulazima gani wa kuniuliza maswali hayo yahusuyo dini na ukanda? Au ndo version mpya kama gia ya kuinhilia!!
Alikupiga kisaikolojia, Hapo aliamua akuanzie mbali ile hakulete karibu ili iwe rahisi kukupiga mzinga
 
Kitu nachojiuliza ni kuwa kulikuwa na ulazima gani kuniuliza kuhusu dini na ukanda kabla hajaomba msaada?

Just relax Ni mbinu tuu ya utapeli uislam(atakuwa muislam)na Zanzibari (atakua aliishi/alikaa). Ungekuwa na kimoja wapo angepata topic ili akusokote vizuri.
 
Mzee: Marahaba. (Kimya kidogo) Samahani kijana, wewe ni muislamu?



Mimi: Hapana



Yeye: (kimya kidogo) Wewe ni Mzanzibari?



Mimi: hapana.



japo aliniacha na maswali yasiyo na majibu.

Mkuu mbona maswali uliyajibu au alikuachia mengine kwenye karatasi Kama homework?
😂😂😂
 
Back
Top Bottom