Chilli
JF-Expert Member
- Jul 17, 2011
- 1,655
- 743
Nilikua na hamu kweli ya kuangalia mahojiano ya Mrisho Mpoto 'Mjomba' na Salama kwenye kipindi cha Mkasi nikitegemea kukutana na Kiswahili kilichonyooka na misemo mitamumitamu ya Kiswahili.
Lakini nilichokutana nacho ni uharibifu mkubwa wa lugha yetu adhimu ya Kiswahili kwa kushindwa hata kutumia maneno sahihi ya Kiswahili katika maongezi.
Jaribu kufikiri, nguli wa mashairi ya Kiswahili kama Mpoto ndani ya muda usiozidi dakika 30 alichanganya maneno ya kiingereza yapatayo 24 kwenye maongezi yake?huu ni wastani wa neno moja kwa kila dakika. Halafu watu hawahawa ndio wanasema wanahamasisha Kiswahili.
Maneno yenyewe aliyoyachanganya Mpoto ambayo kwa kweli ni 'marahisi' mno kuniambia Mpoto alishindwa kupata maana yake kwa Kiswahili. Maneno hayo ni pamoja na energy, design, category, resight, hobbie, character, concentrate, theory, research, promote, character, page, cote, audience, interview, explain, programmed, management, peak, what next, failure, time less na mengine machache.
Kiukweli Mpoto alinikera na kupunguza heshima yangu kwake kama mwanazuoni mwenzangu.
Lakini nilichokutana nacho ni uharibifu mkubwa wa lugha yetu adhimu ya Kiswahili kwa kushindwa hata kutumia maneno sahihi ya Kiswahili katika maongezi.
Jaribu kufikiri, nguli wa mashairi ya Kiswahili kama Mpoto ndani ya muda usiozidi dakika 30 alichanganya maneno ya kiingereza yapatayo 24 kwenye maongezi yake?huu ni wastani wa neno moja kwa kila dakika. Halafu watu hawahawa ndio wanasema wanahamasisha Kiswahili.
Maneno yenyewe aliyoyachanganya Mpoto ambayo kwa kweli ni 'marahisi' mno kuniambia Mpoto alishindwa kupata maana yake kwa Kiswahili. Maneno hayo ni pamoja na energy, design, category, resight, hobbie, character, concentrate, theory, research, promote, character, page, cote, audience, interview, explain, programmed, management, peak, what next, failure, time less na mengine machache.
Kiukweli Mpoto alinikera na kupunguza heshima yangu kwake kama mwanazuoni mwenzangu.