Nilichomfanya X wangu sijui huko alipo atakuwa anajisikaje

Applicant

JF-Expert Member
Feb 12, 2020
1,962
1,746
Miaka miwili nyuma niliachana na binti mmoja single mother, alikua na mashauzi sana na kujiona mzuri ikatokea tukaachana, ni binti aliekua ananichukulia poa sana aliniona sina pesa.

Sasa leo, niko zangu kwenye pantoni natoka zangu Kigamboni, mara uso kwa uso naonana nae kwenye panton! Alivyoniona akasema " eeeh!!! Ndio wewe, umebadlika sana!" Na mimi nikamwambia hata wewe umebadlika, wakati huo alikua kamshka mkono mtoto wake wa kike, kiukweli alikua amekua sana yule mtoto! Mama yake akamwambia " weee msalimie ankooo unamkumbuka???!!" Basi mtoto akanisalimia akiwa anatabasam.

Basi nikaona kwakua tumekutana nae, tulivyoshuka kwenye panton nikawapeleka KFC pale posta, nikamnunulia misosi na vinywaji mtoto wake alifurahi sana, wakala na kusaza, sasa ili kumuonyesha kua mimi sio yule, tulivyomaliza kula nikamuaga, wakati naongea nae aliniambia anakaa CHANIKA kwasasa, basi nikatoa pochi, nakumbuka hiyo siku nilikua na 400,000 tuu kwenye pochi, basi baada ya malipo ya chakula na vinywaji, nikabakiwa kama na 350,000 hivi.

Nikampa 150,000 nikamwambia hiyo itakua ya nauli ya kwenda kwake chanika!

Na mtoto nikamuita " ankooo! Chukua hii zawadi yako utanunulia hata madaftari na kalamu kwa ajili ya shule, nikamuhesabia mtoto 80,000 " pesa iliobak nikairudisha kwenye pochi chap! Nikaangalia saa ya mkononi nikamwambia basi nimepokeaa sms nahitajika kazini ngoja niwahi tutaonana siku nyingine!

Tukaamka pale kwenye viti, tukaondoka, ikafika mbele kidogo tukaachana kila mtu na njia yake yeye akawa anaelekea kupanda dalala mimi akaniacha nimekaa seehemu nasubiri uber, mara baada ya dakika kama 3 hivi nkashangaa anarud anahemaaa jasho linamtitirika! Etii anasema "hee wewe nmesahau kuchukua namba zako niandikie hapo! Akanipa simu yake nikaandika namba zangu akaondoka, baada ya dakika 10 sms inaingia " tushapanda daladala mpenzi"

Yani kwa kifupi nilichojifunza kwenye haya maisha TUTAFUTENI PESA WASHKAJI

YANI UKIWA HUNA PESA KWENYE HII DUNIA NI KAMA MZURURAJI TUU !

YAANI TAFUTA PESA KWA HALI NA MALI
 
Miaka miwili nyuma niliachana na binti mmoja single mother, alikua na mashauzi sana na kujiona mzuri ikatokea tukaachana, ni binti aliekua ananichukulia poa sana aliniona sina pesa.

Sasa leo, niko zangu kwenye pantoni natoka zangu kigamboni, mara uso kwa uso naonana nae kwenye panton! Alivyoniona akasema " eeeh!!! Ndio wewe, umebadlika sana!" Na mimi nikamwambia hata wewe umebadlika, wakati huo alikua kamshka mkono mtoto wake wa kike, kiukweli alikua amekua sana yule mtoto! Mama yake akamwambia " weee msalimie ankooo unamkumbuka???!!" Basi mtoto akanisalimia akiwa anatabasam..

B
Heading ibadilishe iwe hivi, Alichokufanya ex wako mpaka sasa hujasahau hadi umefungua thread kwa uchungu wa expenditure ulizofanya bila kutaraji. Huwezi kulikomoa jiwe kwa kulipiga ngumi mkuu
 
Back
Top Bottom