Uchaguzi 2020 Nilichokiona hapa Korogwe kwenye mapokezi ya Magufuli, aaah huyu mtu anapendwa sana

Anapendwa na nani?

Yaani atese wananchi kwa miaka mitano halafu wampende?

Kuna lipi jipya na lenye maana aliwaahidi kuwafanyia wakazi wa Korogwe mwaka 2015 halafu mwisho wa siku akawafanyia?
Unao uhuru wa kuandika unachoandika. CCM hoyeeeee
 
Ukiwalinganisha wanaotaka urais, baadhi wanaopata kushabikiwa hadi unaona huruma. Hivi kweli akili ya Lissu inaweza kuongoza nchi na ukaamini nchi itaendelea! Tutajikuta kila siku rais akitunga sheria.
Hahahah nimecheka sana.
Eti utajikuta kila siku nchi inatunga sheria? Hii serikal ya sasa toka iingie imetunga sheria ngapi?
No offence.. lakin kama hujamfanyia vetting na physc eval huwez jua nn anawaza.
 
Anakwenda kaskazini kuomba nn Hali aliwanyima maendeleo, yaani kwenye shida ndo anajifanya kukumbuka wa kaskazini.
 
Nyie mnaosema magufuli baba lao ndio nyie nyie mtakaokuja kusema magufuli bibi lao
 
Asilimia kubwa sio wakazi wa hapo,wengi wameletwa kutoka magoma,kwashemshi,mombo na vijiji vya karibu kwa ufupi mikutano ya CCM ni ya kutengeneza sio halisi hili lipo wazi na nimelishudia
Sasa, watu wasipotengenezwa na wakaja, hizo sera ataiambia miti? Cha msingi hawana pingu mikononi, na hakuna polisi wa kuwazuia kuondoka.
 
Hahaha hakuna kijana mwenye akili timamu atakekuwa ccm leo hii.

Kwa lipi hasa?!
Hiyo Slogan ya kwamba CCM ni ya wazee ilifanikisha sana wakati wa 2015 lakini kwa mwaka huu haina mashiko. Vijana wengi wako CCM sema cdm ina waadholika wa kutumbuliwa ambao siyo wengi.

Na tumbua pia athali zake ni ndogo sana kwa CCM kwa sababu asili ya Watanzania ni watu wa kufulahia wakiona mwenzao anaharibikiwa (anapata matatizo). Hivyo tumbu tumbua kwa ujumla imewafurahisha wengi na kuwaudhi wachache waliyotumbuliwa
 
Wakuu,

Niko hapa Korogwe ambapo Kesho tutakuwa na kampeni ya mkoa kwa mgombea wa CCM ndugu Magufuli.

Wananchi wamejitokeza kwa wingi sana kumsalimia barabarani. Watu ni wengi mno. Nimeamini kuwa kiongozi anayeshughulika na matatizo ya watu, atapendwa na kuheshimiwa.

UPDATES

20/10/2020 0805

Uwanja umefurika watu na babu Seya anatumbuiza hapa.

Kuingia uwanjani ni lazima unawishwe na vitakasa mikono (sanitizer) na upimwe joto la mwili. CCM inajali na inachukua hatua zote za kiafya kama inavyoshauriwa na wataalamu wa afya

0830

Helikopta ya CCM inaamsha popo uwanjani hapa

0835

Humphrey Polepole anaongea

0850

Wagommbea Ubunge wanaeleza Utekelezaji wa ilani ya CCM, kumuombea kura Magufuli, wait wenyewe na madiwani wa CCM

0950

Magufuli anawasili uwanjani

Hongera sana Magufuli na karibu Tanga

Amani

View attachment 1605139

Video (Dkt. Magufuli akiwa Mkata)

View attachment 1605611
Hapendwi
 
Back
Top Bottom