Nilichogundua teuzi za Rais Magufuli

Habari wana-JF
Mhe. JPM mara nyingi hufanya teuzi mbalimbali akiwa anachagua wasomi,wahadhiri na wanataaluma.

Mfano jana kamteua "nguli wa sheria kuwa mbunge"(kwa mujibu wa gazeti la mwananchi). Nilichogundua ni kuwa anachagua watu wa aina hii kama njia ya kujihami kwa sababu zifuatazo;

1. Hawa wasomi anaowachagua hawawezi kupingana na bosi wao hata ikitokea kakosea mambo.

2. Kuwanyamazìsha watu wasiweze kuhoji pale inapoonekana jambo limekosewa na Mhe. maana utaambiwa mbona akina fulani ni wasomi wamesema mambo yako sawa.

3. Kuonyesha kuwa anajenga serikali ya wasomi ambao wanaamua masuala ya nchi kitaalamu jambo ambalo si kweli tunaona mambo mengine yanaamulia kinyume mfano uvunjaji wa katiba
Na Abdallah Bulembo ni msomi aliyebobea au?
 
Mkuu hayo uliyoyaandika mheshimiwa JPM anayajua fika, ndio maana baraza la mawaziri la sasa limejaa PHD na Prof.

Kama ulinielewa nilichokisema, usingeandika haya. Nimesema, Tanzania haijawahi kuwa na uhaba wa wasomi serikalini. Tatizo ni wasomi hao hawatumiwi (mawazo yao hayafanyiwi kazi). Pili, serikali za CCM zimekuwa na tabia ya ku-silent critical na radical wasomi kwa kuwahonga madaraka. Hiyo imekuwa haswa kwa wasomi wanaotanguliza matumbo yao mbele.

Nimekupa mfano wa Mwakyembe kukana kile alichokiandika kwenye PhD thesis yake! Walikuwepo wakina Prof. Mbilinyi, Dr. Kigoda, Dr. Limbu, Prof. Sarungi, Prof. Tibaijuka, Prof. Mwakyusa, Dr. Kawambwa, Dr. William Shija, Prof. Maghembe n.k. Na makumi ya PhD holders kwenye wizara na taasisi nyingine za serikali. Lakini nchi yetu ipo kama haijawahi kuwa na wasomi; hususani post-Nyerere era.

Lawama tu siku nzima bila ya kutazama mambo katika jicho positive, sio suluhisho la matatizo tuliyonayo.

Utakuwa positive kwa serikali ambayo kwa miaka 50 imeshindwa kukamilisha jambo lolote lenye manufaa kwa wananchi kwa asilimia 100? Unakuwaje positive hapo; wakati bado wana-struggle kupata basic human needs, huku viongozi wakiishi kitajiri?

Suluhisho ni CCM kuondoka madarakani. PERIOD
Halafu maCCM hayo hayo yakakupeni makombo, na hayo makombo ndio aliyekuwa mgombea kwa tiketi ya UKAWA.
Ona sasa! Wewe nawe ndiyo wale wanaofikiri kila asiyewapenda CCM ni UKAWA. Mimi naichukia CCM tu. Sijali hata kama CHAUMMA waongoze taifa hili, lakini si CCM.
 
Msomi anaacha kuwa msomi pale anapochagua kufanya au kusimamia jambo nje ya kile alichosomea. Mfano msomi wa kemia akiwa rais kupitia kura huyo sio msomi tena wa kemia bali ni mwanasiasa. Ili ubaki kuwa msomi unatakiwa uwe independent, impartial, unbiased na uonyeshe transparency kwenye kazi zako. Haya yote yanapotea unapojiingiza Kwenye siasa au chama.

Nchi za wenzetu wamewatenga wasomi na siasa kwa kuwaundia taasisi ambazo kazi yake ni kuishauri serikali na vyombo vyote vya maamuzi pasipo kujali chama wala itikadi zao. Sisi hapa NMRI imekuwa ya siasa, Repoa/Twaweza imejaa wasomi-siasa, TANESCO hivyo hivyo, vyuoni maptofesa waliotakiwa waisaidie nchi pasipo upendeleo ndio kwanza wanaandika vimemo wateuliwe nafasi za kisiasa. Usomi sasa ni siasa sio taaluma nyingine. Mhadhiri akiteuliwa nafasi ya kisiasa anashindwa kujuwa kwamba taaluma yake ndio basi tena.

Tutapataje wasomi halisi na makini watakao ongoza maamuzi ya serikali endapo kila kitengo cha maamuzi mkuu wake anateuliwa na rais kutoka chungu cha wasomi? Kwa maneno mengine msomi aliyeteuliwa ukurugenzi wa taasi anapata wapi nguvu ya kuwa unbiased, transparent, impartial, na independent kwenye maamuzi yake na kazi zake? Vyuo vyetu vimegeuka viwanda vya makada sio wasomi.
Mkuu, I couldn't agree more. Umemaliza kila kitu. Shukrani kwa haya uliyoyasema. Ubarikiwe.
 
Suluhisho ni CCM kuondoka madarakani. PERIOD
Mkuu kwenye hilo aupo pekee kuna wapiga mbiu wa CCM wenye shughuli zingine za kupata mlo lakini wanajishughulisha na mambo ya CCM katika muda wao. Kuna baadhi yao pia nimewasikia kwa mara ya kwanza wanadhani kuna sababu ya CCM kukaa benchi kwanza.

Kikubwa ni kwamba kuna wanasiasa huko juu wanadhani CCM ni tabaka halali la kuongoza nchi na awajali tena nani anapewa nyadhifa gani na ana uwezo gani pamoja na majibu ya mkato kwenye hoja muhimu.

Tatizo ukiwasikiliza hawa upinzani jinsi ya kutatua kero ndipo hapo mtu unapoona afadhali hata hao CCM its catch 22.
 
Tatizo kubwa ni njaa,kutaka sifa,kutaka vyeo na kutaka utajiri wa haraka ndiko kunafanya wasomi kutaka vyeo LAITI KAMA wasomi tulionao wangeweka msimamo na kutumia taaluma zao vizuri tusingefika hapa tulipo na malalamiko mengi yangepungua tusimlaumu Bw. Magu kuwa hasikilizi ushauri tuwalaumu wasomi wanaoshindwa kutumia taaluma zao kumshauri bwana mkubwa
 
Nikusaidie kuweka maneno sawa kwa vitendo..

1: Makocha wanajua mpira sana kwenye papers only | Theorists, Wasomi, Educators |

2: Messi, Ronaldo, Suarez hawa ndio wanajua sana mpira kwa vitendo, uhalisia | watendaji bora wenye kuchapa kazi, haijalishi kiwango cha elimu yaweza kuwa diploma, degree, masters Phd etc, wenye kujituma, waaminifu, wabunifu, wazalendo daima |

Ukitaka ushinde mechi vizuri, unahitaji sana sana namba 2, alafu namba 1 inafuata.. sio kinyume chake..!!

So, to conclude, MTENDAJI BORA WA KAZI, SIO LAZIMA AWE MSOMI SANAAA, LA HARSHA..!!
 
Sasa mtu mkweli muwazi na mtetea wananchi kama Kabudi anaenda kuingia kwenye serikali ya dikteta uchwara lengo lake likuwa kutesa kupoteza watu kutukana kufirisi uchumi wa nchi kuvunja sharia si ndio maajabu ya wasomi wa Tanzania hawawezi kusema hapana ndio maana mtu kama jaji Agustine akashikishwa koba la CCM na yeye akakubali hii inchi ni vituko
 
Sasa mtu mkweli muwazi na mtetea wananchi kama Kabudi anaenda kuingia kwenye serikali ya dikteta uchwara lengo lake likuwa kutesa kupoteza watu kutukana kufirisi uchumi wa nchi kuvunja sharia si ndio maajabu ya wasomi wa Tanzania hawawezi kusema hapana ndio maana mtu kama jaji Agustine akashikishwa koba la CCM na yeye akakubali hii inchi ni vituko

Huyu Kabudi Palamagamba si ndio huyu huyu JPM alimteua siku za kwanza kwanza za utawala wake kuwa Mwenyekiti wa bodi ya TIB; sasa kama alivyomteua kuwa mbunge je ataendelea kuwa Mwenyekiti wa hiyo benki ilihali wabunge ndio wasimamizi wa hizi taasisi za umma? Hopefully makosa ya mkweree hayatarudiwa kwa kurundika vyeo vingi kwa mtu mmoja kwa sababu ya mapenzi tu!!
 
Ni walimu hao tu na sio wasomi jamani. Kuna tofauti kubwa kati ya mwalimu na msomi. Msomi anaweka katika vitendo yale aliyoyasomea. Mwalimu anabakia na nadharia zake kichwani tu. Nakumbuka Mwalimiu wangu wa hesabu alinisumbua sana darasani. Baadae akageuka ombaomba wangu. Nilibaki kumheshimu japo ukweli ndio huo. Kujua kote hesabu zile hakukumsaidia maishani!
 
Mkuu zamani hata mimi nilikuwa nawaamini wasomi ile mbaya. Lakini nilivyoonza kuona mikataba ya kipuuzi kwenye raslimali zetu, makumpuni kibao kufa mikononi mwa wasomi , basi tokea hapo nawadharau wasomi ile mbaya. Kitu kingine kinachonifanya kuwadharau wasomi wengi, unakuta mtu ni msomi lakini maisha yake yote yanategemea ajira, akikosa ajira hata wazo la kufungua mradi wowote hana. Ukitaka kucheka mkabidhi mradi ausimamie, mpe miezi sita tu huo mradi utakuwa duni au hoi kabisa.
Siwezi kukubaliana na wewe 100% kuna baadhi ya mambo kama mtu hajasomaa huwezi kumkabidhi mradi. Wasomi kuna mabo wanafanya vizuri na mengine wanafanya vibaya sana. Hasa siasa sidhani kama inatekelezeka kwa professionals, hawa wanatakiwa kufundisha wanafunzi vyuo vikuu.
 
Kikwete aliwahi kusema kuwa "uwaziri au ubunge hausomewi" huu ni mpango mkakati, Tanzania ya viwanda is loading....please wait....
 
Back
Top Bottom