Nilichogundua kutoka kwa mwamuzi Nassir Salim (Azam FC vs Simba SC) fainali ya Mapinduzi Cup

Lupweko

JF-Expert Member
Mar 26, 2009
20,690
20,451
Mwamuzi Nassir Salim wa Zanzibar aliyechezesha fainali ya Kombe la Mapinduzi kati ya Azam FC na Simba SC hakuwa na ufahamu kuhusu sheria ya mchezaji kurudisha mpira kwa golikipa wake. Mwamuzi huyu alikuwa anajua kwamba mpira wowote uakaorudishwa na mchezaji kwa golikipa wake ni faulo. Alifanya hivyo katika matukio mawili:

1. Wakati golikipa Mathias Kigonya alipomchezea rafu mbaya Pape Sackho, mwamuzi alikuwa hajaliona tukio hili la rafu, ila alikuwa ameliona na kulitolea adhabu tukio lililofanyika kabla Kigonya hajacheza faulo. Alichokiona ni beki wa Azam akirudisha kwa golikipa wake akitumia kichwa. Mwamuzi akatafsiri ni kosa na ndio maana akatoa adhabu ya indirect kick ndani ya box la Azam. Tukio hili waliligundua wachache maana lilikuja kufunikwa na maamuzi mapya baada ya mwamuzi msaidizi na fourth official kumuita kwenye kibendera na kumueleza kuwa kuna faulo mbaya amefanyiwa Sackho, na ndipo ikawa penati, otherwise isingekuwa Sackho amfanyiwa faulo wengi mngeshangazwa na uamuzi wa indirect kick kwa sababu kipa amerudishiwa mpira, wakati sheria inaruhusu kurudishiwa kwa kichwa au kifua

2. Tukio la pili ni pale Onyango alipourudisha mpira nyuma, Henock Inonga akaubetua na kuuinua kisha akaupiga kichwa kumpa Manula. Cha kushangaza mwamuzi akakimbilia aliposimama Inonga na kuamuru ipigwe indirect kick, na hii ndio iliyakuwa dhahiri maana ilipigwa ingawa kila anayejua sheria za soka alishangaa


1642136856046.png
 
No wonder waamuzi wa Tanzania wanaishia kuchezesha mechi za kitaifa tu.

Nichukue fursa hii pia kuwapongeza mashabiki, uongozi na wachezaji wa SIMBA SPORTS CLUB.....bila kusahau benchi la ufundi.

Pia nawapa pole mashabiki wa Yanga kwa maumivu waliyopata.

Sijawapa pole mashabiki wa AZAM.

Nina maana yangu.
 
Ile ya inonga yuko sahihi Hairuhusiwi mchezaji kurudisha kwa kichwa mpira uliotulia yani uubetue umpe ni kosa mpira unaopaswa wa kichwa ni ule wa kwenye motion
View attachment 2080195
hicho kifungu unakielewaje mkuu
Kwa nini refa alipiga filimbi kabla Manula hajaushika mpira? Sheria hii inazuia back pass pale ambapo golikipa ataukamata kwa mikono, lakini back pass huku kipa akiucheza kwa miguu inaruhusiwa. Ina maana Inonga angeurudisha kwa mguu halafu Manula angeendelea kuwa nao mguuni na kucheza tena pasi, nalo pia ni kosa?

1642141676741.png
 
Mwamuzi Nassir Salim wa Zanzibar aliyechezesha fainali ya Kombe la Mapinduzi kati ya Azam FC na Simba SC hakuwa na ufahamu kuhusu sheria ya mchezaji kurudisha mpira kwa golikipa wake. Mwamuzi huyu alikuwa anajua kwamba mpira wowote uakaorudishwa na mchezaji kwa golikipa wake ni faulo. Alifanya hivyo katika matukio mawili:

1. Wakati golikipa Mathias Kigonya alipomchezea rafu mbaya Pape Sackho, mwamuzi alikuwa hajaliona tukio hili la rafu, ila alikuwa ameliona na kulitolea adhabu tukio lililofanyika kabla Kigonya hajacheza faulo. Alichokiona ni beki wa Azam akirudisha kwa golikipa wake akitumia kichwa. Mwamuzi akatafsiri ni kosa na ndio maana akatoa adhabu ya indirect kick ndani ya box la Azam. Tukio hili waliligundua wachache maana lilikuja kufunikwa na maamuzi mapya baada ya mwamuzi msaidizi na fourth official kumuita kwenye kibendera na kumueleza kuwa kuna faulo mbaya amefanyiwa Sackho, na ndipo ikawa penati, otherwise isingekuwa Sackho amfanyiwa faulo wengi mngeshangazwa na uamuzi wa indirect kick kwa sababu kipa amerudishiwa mpira, wakati sheria inaruhusu kurudishiwa kwa kichwa au kifua

2. Tukio la pili ni pale Onyango alipourudisha mpira nyuma, Henock Inonga akaubetua na kuuinua kisha akaupiga kichwa kumpa Manula. Cha kushangaza mwamuzi akakimbilia aliposimama Inonga na kuamuru ipigwe indirect kick, na hii ndio iliyakuwa dhahiri maana ilipigwa ingawa kila anayejua sheria za soka alishangaa


View attachment 2080189
Kwa Inonga ilikuwa sahihi Mana pale inaangaliwa dhamira yake kwamba ni kupoteza muda Kwa wazi kabisa pasipo sababu za msingi. Henock alikuwa peke yake angeweza kuendeleza tu mchezo hivyo hakukuwa na sababu za kufanya vile. Kwa tukio la sacko refa alichemka kutoa penati. Ilipaswa kuwa faulo ndani ya 18 na red card kwa kipa!
 
Kwa Inonga ilikuwa sahihi Mana pale inaangaliwa dhamira yake kwamba ni kupoteza muda Kwa wazi kabisa pasipo sababu za msingi. Henock alikuwa peke yake angeweza kuendeleza tu mchezo hivyo hakukuwa na sababu za kufanya vile. Kwa tukio la sacko refa alichemka kutoa penati. Ilipaswa kuwa faulo ndani ya 18 na red card kwa kipa!
Umekula?

Sent from my PBBM00 using JamiiForums mobile app
 
Kwa Inonga ilikuwa sahihi Mana pale inaangaliwa dhamira yake kwamba ni kupoteza muda Kwa wazi kabisa pasipo sababu za msingi. Henock alikuwa peke yake angeweza kuendeleza tu mchezo hivyo hakukuwa na sababu za kufanya vile.
Nimeuliza swali lakini sijajibiwa bado. Mbona alipourudisha mpira nyuma, Manula hakuukamata kwa mikono ila refa akapiga filimbi ya kosa? Mimi nijuavyo kipa anachokatazwa ni kudaka/kushika mpira uliorudishwa nyuma kwa makusudi, lakini anaweza kuucheza kwa miguu
 
Kwa Inonga ilikuwa sahihi Mana pale inaangaliwa dhamira yake kwamba ni kupoteza muda Kwa wazi kabisa pasipo sababu za msingi. Henock alikuwa peke yake angeweza kuendeleza tu mchezo hivyo hakukuwa na sababu za kufanya vile. Kwa tukio la sacko refa alichemka kutoa penati. Ilipaswa kuwa faulo ndani ya 18 na red card kwa kipa!
Kwa Inonga referee alikua sahihi, Ila kwa Sacko mwamuzi hakuona tukio ndio maana hakumpa nyekundu, Ila ilipaswa apewe nyekundu na penati. Kwa sababu ile ilikua violence faul sio reckless.
 
Huyo ni Ivan Perisic mchezaji Mkubwa tu alipewa kadi kwa kitendo kama cha Inonga, Lakini wana Simba hawataki
 
Back
Top Bottom