Pre GE2025 Nilichogundua katika zoezi la usajili wa wana CCM kidigitali: Wanaoandikishwa wanajua ni uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Freed Freed

JF-Expert Member
Jun 27, 2017
6,497
6,957
Walisema tembea uone mengi pia uliza ujifunze.

Katika zoezi la CCM kusajili wanachama wake, kuna mengi wananchi wanaojitokeza kuandikishwa hawajui au wamefichwa. Wengi wanaenda na kadi za tume ya uchaguzi wakitaka kuandikisha taarifa zao na kukuta watu wamevaa sare za chama.

Hapo huambiwa usiwe na shaka leta hiki na kile na baada ya hapo usajili huanza na watu wengi wasivyo waelewa hudhani wameandikishwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Nachojiuliza kwa haya maeneo ambapo daftari la kudumu la wapiga kura bado halijapita, si itakuja kuwa ngumu kuwaita watu hawa wasajiliwe?

NB: Watu wanajitokeza kwa wingi na wameitikia wito kwelikweli.
 
Nlicho gundua yale majina wanayo chukua wanakuja kuprint kisha wanakuwekea alama ya V (vema) kwenye sura ya mhombea wa kijani then automatically utakuwa umesha piga kura kwahiyo uwende usiende umesha hesabika kama umepiga kura
 
Nlicho gundua yale majina wanayo chukua wanakuja kuprint kisha wanakuwekea alama ya V (vema) kwenye sura ya mhombea wa kijani then automatically utakuwa umesha piga kura kwahiyo uwende usiende umesha hesabika kama umepiga kura
Wizi wa mapema na vuruga mapema ya uchaguzi.
 
Nlicho gundua yale majina wanayo chukua wanakuja kuprint kisha wanakuwekea alama ya V (vema) kwenye sura ya mhombea wa kijani then automatically utakuwa umesha piga kura kwahiyo uwende usiende umesha hesabika kama umepiga kura
Wanachama hao huenda wasigundue umuhimu wa dafatari la NEC
 
Hilo daftari pia hutumika kuibiana kura wenyewe kwa wenyewe.
Wajumbe feki hupatikana humohumo.
 
Walisema tembea uone mengi pia uliza ujifunze.

Katika zoezi la CCM kusajili wanachama wake, kuna mengi wananchi wanaojitokeza kuandikishwa hawajui au wamefichwa. Wengi wanaenda na kadi za tume ya uchaguzi wakitaka kuandikisha taarifa zao na kukuta watu wamevaa sare za chama.

Hapo huambiwa usiwe na shaka leta hiki na kile na baada ya hapo usajili huanza na watu wengi wasivyo waelewa hudhani wameandikishwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Nachojiuliza kwa haya maeneo ambapo daftari la kudumu la wapiga kura bado halijapita, si itakuja kuwa ngumu kuwaita watu hawa wasajiliwe?

NB: Watu wanajitokeza kwa wingi na wameitikia wito kwelikweli.
Mkuu ina maana hilo eneo limejangaa wajinga wa hatari, yaani wamejitokeza kwa wingi lakini hawajui tofauti ya daftari la wapiga kura, na kadi za ccm? Kama kuna wajinga wa hivyo hakuna namna ya kuwasaidia. Hizo kura zenu wapeni ccm maana ndio wanaotegemea kura za wajinga.
 
Walisema tembea uone mengi pia uliza ujifunze.

Katika zoezi la CCM kusajili wanachama wake, kuna mengi wananchi wanaojitokeza kuandikishwa hawajui au wamefichwa. Wengi wanaenda na kadi za tume ya uchaguzi wakitaka kuandikisha taarifa zao na kukuta watu wamevaa sare za chama.

Hapo huambiwa usiwe na shaka leta hiki na kile na baada ya hapo usajili huanza na watu wengi wasivyo waelewa hudhani wameandikishwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Nachojiuliza kwa haya maeneo ambapo daftari la kudumu la wapiga kura bado halijapita, si itakuja kuwa ngumu kuwaita watu hawa wasajiliwe?

NB: Watu wanajitokeza kwa wingi na wameitikia wito kwelikweli.
Punguza unafiki, inatangazwa kabisa na CCM wenyewe kwamba wanawasajili wanachama wao kielektroniki na anayekwenda kujisajili anaulizwa kadi yake ya uanachama wa CCM ya zamani zoezi linaendelea na hata kama hana kadi ya zamani basi taratibu za usajili kwa mwanachama mpya zinafanyika tena kwa uhuru mkubwa pasi na shinikizo.
 
Vijana wanajiunga CCM kwa wingi, mwenyewe ningekua KIJANA ningejiunga,aminini tu kitokeacho
 
Punguza unafiki, inatangazwa kabisa na CCM wenyewe kwamba wanawasajili wanachama wao kielektroniki na anayekwenda kujisajili anaulizwa kadi yake ya uanachama wa CCM ya zamani zoezi linaendelea na hata kama hana kadi ya zamani basi taratibu za usajili kwa mwanachama mpya zinafanyika tena kwa uhuru mkubwa pasi na shinikizo.
Sivyo kwa maeneo yote. Wengine wanaingizwa mkenge.
 
Back
Top Bottom