Niko Njia Panda: Namchumbia msichana mwenye mtoto lakini kwetu sitaki wajue ana mtoto

Asemavyo

JF-Expert Member
Oct 22, 2017
312
821
Jamaa anaomba ushauri Habari zenu, kuna binti niko naye kwenye mahusiano yapata miezi 8 sasa, nimefika hatua ya kutambulika kwao na yeye kutambulika kwetu,

Ila kipindi naanza naye mahusiano aliniambia Ana mtoto anaishi na Bibi, yaan mama yake msichana. Tukaendelea na mahusiano. Kadri nilivyokaa naye naona anafaa kabisa, niwe mkweli. Nikasema nyumbani kuwa nina mchumba wakafurahi, lakin nikihofia wakijua Ana mtoto nitakataliwa.

Baada ya kushibana kabisa nikaamua tuandae mshenga kwa ajili ya kwenda kusema. Akaniuliza kuwa lakin kwenu uliwaeleza kuwa nina mtoto. Nikasema hapana na mtoto wako ni kama wangu istoshe yuko kwa bibi huko tutamtunza tu kwa kuyatuma matumizi na ada ya shule akakubali

Tatizo likaja alipomweleza mama yake kakataa kata kata kwamba lazima mshenga aambiwe kuwa ana mtoto na akasema kwamba kwanza ameahirisha hataki kusikia habari za mshenga wala mgeni yeyote maana kashamchefua tiyari.

Binti akanirudia akiwa na machungu kwamba mama kakataa kasema tutashindwaje kusema kuwa ana mtoto? Pili Binti alimuelezea kuwa nimeshamshawishi kaacha kazi jambo ambalo ni kweli na nimempa mtaji wa 10M aanze biashara yake, lakin pamoja na hiyo mama kakataa

Binti kanipa mtihan kuwa niwaeleze sasa wazazi wangu ukweli na nirekodi wakati wa mazungumzo ajiridhishe kama ni ukweli. Pia kama sitafanya hivyo yeye anafuata familia yake inasemaje, na anasema kwamba anirudishie kila nilichompa aanze upya maisha huku akilia

Naombeni ushauri tunafanyaje, sitaki kwetu wajue , na ukizingatia tumeshaweka malengo makubwa
 
Mkuu,ndoa inaunganisha familia,kwa maana familia yako na yake,usijaribu kufanya suala la mtoto likawa siri kwsb litakuja kugundulika baadae na litawavuruga,Pia sijui kama wewe na mwenza wako mmezungumzia kwa kina suala la mtoto kujua labda baba yake yuko wapi,je analeta matunzo ya mtoto au wana mawasiliano? hili pia lina nafasi kwenye mustakabali wa mahusiano yenu,zingatia haya na uyafanyie,vinginevyo utaukumbuka usemi wa "majuto ni mjukuu"
 
Mkuu,ndoa inaunganisha familia,kwa maana familia yako na yake,usijaribu kufanya suala la mtoto likawa siri kwsb litakuja kugundulika baadae na litawavuruga,Pia sijui kama wewe na mwenza wako mmezungumzia kwa kina suala la mtoto kujua labda baba yake yuko wapi,je analeta matunzo ya mtoto au wana mawasiliano? hili pia lina nafasi kwenye mustakabali wa mahusiano yenu,zingatia haya na uyafanyie,vinginevyo utaukumbuka usemi wa "majuto ni mjukuu"
Binti anaishi dar es salaam na mtoto yuko Mbeya
 
Ndoa ni yako mkuu, SI ya know baba au mama au mtu yeyote tofauti na wewe na mke wako mtarajiwa.

Kuhusu suala la kuwaambia wazazi wako naona halina shida, shida inakuja ambapo tayari ushakaa nae mpendwa tena kwa muda mrefu bila kuwa mkweli kwa wazazi wako implication yake ni ngumu kutoa majibu ambayo yatakuwa expected na wewe kwani unaweza kuleta uzi mwingine wa kulalamika kuacha mpenzi uliye pewa na mola.

Tafuta namna ya kuwaamhia wazazi, tell them on how you're wife to be qualifies . Hakikisha unajiridhisha kweli mtarajiwa wako ana nia ya dhati isije ikawa ni hizo 10mils mkuu.Ndoa ni wewe, chunguza kama atafaa kuwa mke wako, usitangulize hisia zaid kwenye hili,itapendeza ukifahamu kama huyo mwanaume hana mawasiliano ya karibu na mtarajiwa wako, utanikumbuka kiongozi kwani huenda mwanamke au mpenzi wako huyo ni mpenzi wa jamaa aliyezaa nae.

Note, ndoa haiwi influenced na mambo kama pesa, ndugu nk nk, jiangalie wewe kama wewe mengine yatafuat kwa wazazi ambayo automatically ni ngumu kukukatalia

Thanks

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ramli chonganishi

Kwanza huyo mpenzi wako hakupendi na amemkumbuka baba wa mtoto wake na huenda wameanza mawasiliano ya kujenga penzi lao
Hivyo kaona mbinu ya kuachana na wewe kwa amani ni kushinikiza uwambie wazazi wako juu ya mtoto aliyenaye.

Imani yake ni kuwa wazazi wako hawatokubari hivyo utakuwa umebariki safari njema juu yake.

Mama yake hawezi shinikiza juu ya hulo bali hayo ni mawazo yake tu ama ya marafik zake ili afanikishe wazo lake.

Kama kweli hilo ni wazo la mama yake bas huyo mama yake ndo hayataki mahusiano yenu basi ye kaona kete ya kushinda ni hiyo ya mtoto
 
Habari zenu, kuna binti niko naye kwenye mahusiano yapata miezi 8 sasa, nimefika hatua ya kutambulika kwao na yeye kutambulika kwetu,

Ila kipindi naanza naye mahusiano aliniambia Ana mtoto anaishi na Bibi, yaan mama yake msichana. Tukaendelea na mahusiano. Kadri nilivyokaa naye naona anafaa kabisa, niwe mkweli. Nikasema nyumbani kuwa nina mchumba wakafurahi, lakin nikihofia wakijua Ana mtoto nitakataliwa.

Baada ya kushibana kabisa nikaamua tuandae mshenga kwa ajili ya kwenda kusema. Akaniuliza kuwa lakin kwenu uliwaeleza kuwa nina mtoto. Nikasema hapana na mtoto wako ni kama wangu istoshe yuko kwa bibi huko tutamtunza tu kwa kuyatuma matumizi na ada ya shule akakubali

Tatizo likaja alipomweleza mama yake kakataa kata kata kwamba lazima mshenga aambiwe kuwa ana mtoto na akasema kwamba kwanza ameahirisha hataki kusikia habari za mshenga wala mgeni yeyote maana kashamchefua tiyari.

Binti akanirudia akiwa na machungu kwamba mama kakataa kasema tutashindwaje kusema kuwa ana mtoto? Pili Binti alimuelezea kuwa nimeshamshawishi kaacha kazi jambo ambalo ni kweli na nimempa mtaji wa 10M aanze biashara yake, lakin pamoja na hiyo mama kakataa

Binti kanipa mtihan kuwa niwaeleze sasa wazazi wangu ukweli na nirekodi wakati wa mazungumzo ajiridhishe kama ni ukweli. Pia kama sitafanya hivyo yeye anafuata familia yake inasemaje, na anasema kwamba anirudishie kila nilichompa aanze upya maisha huku akilia

Naombeni ushauri tunafanyaje, sitaki kwetu wajue , na ukizingatia tumeshaweka malengo makubwa
tatizo kubwa ambalo unakaribia kulifanya ni kuwaficha wazazi wakO ukweli wa mkeo,
Jua maisha ni kuishi na kwenye kuishi kuna mengi hapo badae yatakitokeza ukianza kwakumfichia ilo jua ipo siku utakuja kumfichia jambo baya zaidi ya ilo na utadhalilika wewe, usiogope wazazi watasema nini waambie upendacho,
Mzazi anapenda kumsadia mtoto apate anachokitaka naamini watakuelewa.
 
Si tumeisha kataa viwanja vyenye mgogoro visinunuliwe? Viwanja visivyo na migogoro vipo.
Hii kitu sielewi inakaaje ati wanawake Fulani wanavaa condom wanajinyima utamu, afu wanawake wengine hawajui hata matumizi ya ndomu utamu wote wale wao, ati kirahisi leo aolewe rasmi kwa Mara ya pili? Inaingia akilini jamani?

Sheria inasema achojoe ndani aliyetoa mahari tu kama mahari bado chojoa kwenye mfuko au asubiri ndoa. Si ndo jamani?
 
Mkuu wewe muda wa kuoa bado....

1. Umefanya maamuzi ya wanandoa ukiwa upo kwenye mahusiano ya girl nd boy friend, kumuachisha kazi na kumpa mtaji wa 10M, hizo decison wanafanyaga wanandoa.

2. Huyu mwanamke ashakucholea mstari, kama utaki kufata vile anaona sawa, iwe basi...nafasi ya kiume inapotea hapo.

3. Upo kwenye nafasi ya kuchoose, lakini unajaribu kujibanza kwenye shida, jaribu kuchagua chenye unafuu kwasababu nafasi bado unayo.....angalizo usioe mtu kwa kumuonea huruma.

4. Bro mechi ya kuanza moja bila, ina ugumu wake.

5. Usipende Democracy sana, kwenye mambo yako ya msingi....invest sanaa kwenye instructions life.

Don't forget, mapenzi yanazaliwa, yanakufa, tunazoea, tunasahu....etc,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom