NIKO LIVE toka Diamondo Jubilee

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Kwa mshangao mkubwa na mtisiko TVT sasa wameacha kutupa habari za Dodoma ambazo zina mambo ya kugusa Taifa .Mjadala wa Richmond sina hakika kama Watanzania wanaweza kuusikia labda iwe recorded.Sasa JK anaongea na wazee wa Mkoa wa Dar Es Salaam .CCM again kwa mara nyingine inakuwa ya kwanza na issue za Taifa zinakuwa za mwisho .

I am confused lakini niko LIVE hapa Dar
 
Huyu anataka kufanya maigizo gani kwenye taifa hili?mbona masuala ya kitaifa yanafanywa ya chama.

Nashangaa sana kuona jinsi ambavyo suala nchi linafanywa kuwa la kichama.
 
Huyu anataka kufanya maigizo gani kwenye taifa hili?mbona masuala ya kitaifa yanafanywa ya chama.

Nashangaa sana kuona jinsi ambavyo suala nchi linafanywa kuwa la kichama.


Hii risala mimi inanishangaza sana .Wanasema JK ameifanya Nchi iwe na utulivu na amani .Kuna vizee hapa hata sijui vimefikaje hapa ni makofi tu na kumwaga sifa .TVT ni chombo cha Taifa na kwa maana hii Bunge could come first than CCM.Lakini mimi kama kawaida nasema kwa JK Chama ni mbele then Taifa .
 
Dodoma muda huu anachangia Zitto juu ya ripoti husika ,wakati huo huo huko Dar JK ananguruma na vyombo vyote vya habari na kuliacha hili la kujadili Richmond kama sio jambo la msingi.
 
Dodoma muda huu anachangia Zitto juu ya ripoti husika ,wakati huo huo huko Dar JK ananguruma na vyombo vyote vya habari na kuliacha hili la kujadili Richmond kama sio jambo la msingi.

Ni ajabu sana .Huyu Mwinyimvua hata kusema anashindwa kusema yaani wanampa TV na tuna acha mambo ya maana ?Kweli Tanzania Nchi yangu ni kichwa cha mwendawazimu .


Dodoma tueleze Zitto anasemaje .
 
Hii risala mimi inanishangaza sana .Wanasema JK ameifanya Nchi iwe na utulivu na amani .Kuna vizee hapa hata sijui vimefikaje hapa ni makofi tu na kumwaga sifa .TVT ni chombo cha Taifa na kwa maana hii Bunge could come first than CCM.Lakini mimi kama kawaida nasema kwa JK Chama ni mbele then Taifa .

Lunyungu,
Ni usanii mtupu.CCM hawana jipya kwa hiyo lazima wafanye hii public relations stunt.
 
Zitto anasisitizaz kuwa mikataba sio siri kwani wao kama wajumbe wa kamati ya madini wamepewa mikataba bila hata ya kiapo kwa nini wabunge wasipewe mikataba hiyo?

Anasisitiza kuwa kuna haja ya mikataba kudaiwa na wabunge na kama serikali ikikataa wabunge wa kila kamati waanzishe kamati kama ya mwakyembe ili kudai mikataba husika .
 
Lunyungu,
Ni usanii mtupu.CCM hawana jipya kwa hiyo lazima wafanye hii public relations stunt.


Ndiyo maana we need separation of 2 kila kimoja kiwe na lake .Kisa ni Rais na the same time Mwenyekiti masuala nyeti sasa hakuna .Hizi ni kampeni ambazo hazitafika popote .
 
Zitto anasisitiza kuwa ni lazima jambo hili lichukuliwe kama la kitaifa na sio suala la vyama kwani kufanya hivyo vyama na haswa CCM walipaswa kuwachukulia hatua viongozi wao na hata kuwavua madaraka kwenye kamati za vyama na sio kuandamana kwa ajili ya mtu kujiuzulu bila kumchukulia hatua .

atafuatiwa na CHACHA WANGWE HAPO BAADAE.
 
Now JK akiri kwamba alitaka kufanya mabadiliko ya baraza . Long LIVE JF tulisema mapema akawa ana buy muda kwamba hadi Bush aondoke .Lakini siku zote alisema ni uvumi leo amekiri LIVE.Hongera JF kwa nyeti .
 
Mbunge wa CCM anasisitiza kuwa Daniel Yona na Rostam Azizi waletwe na waseme kwa nini wamekaidi amri ya bunge ya kwenda kuhojiwa na kamati ya bunge na kwanini wanalidharau bunge .

Anasisitiza pia kuwa lazima viongozi wote waliohusika kwenye richmond basi wawekwe rumande ili kuruhusu uchunguzi wa haki na wafunguliwe mashtaka mara moja.
 
JK aingia ushabiki atangaza kwamba CCM ndiyo wenye issue ya Richmond na kwamba ni CCM ndiyo wanafanya kazi .Amponda Dr.Slaa na kusema anataka sifa binafsi na si mkweli kabisa .Kawataja wana CCM kwenye kamati na kuonyesha kwamba ni Shelukindo kaanza issue .
 
Katika mabadiliko haya bila shaka JK alipanga pia kumwaga EL, maana hajasema
 
mbona nanusa harufu ya viti vya ubunge kuwa wazi. Ningekuwa mimi Lowassa, Msabaha na Karamagi, naamua kujiuzulu Ubunge ili CCM walipie gharama ya uchaguzi..
 
mbona nanusa harufu ya viti vya ubunge kuwa wazi. Ningekuwa mimi Lowassa, Msabaha na Karamagi, naamua kujiuzulu Ubunge ili CCM walipie gharama ya uchaguzi..



JK anamwaga simu kwa Kamati ya Siasa ya CCM na kusema kwa maana nyingine kwamba walitoa uamuzi wa kuwaondoa wachafu kama Lowasa nk .
 
JK sasa anajitetea juu ya kuwamwaga washikaji zake na hasa Lowasa .It is so sad Rais kuja kuelezea hili kama vile walizaliwa Mawaziri
 
JK asema Lowasa ni safi sana .Ni mzalendo na mtu ambaye anaipenda Tanzania na kaisukuma mbele sana Ilani ya CCM. JK anasema kwamba Lowasa kaondoka lakini kaacha alama kubwa .
 
Mwanakijiji
hata mie nimeanza kuhisi jambo hilo. Ninashangaa sana mpaka sasa watuhumiwa bado wanaendelea na ubunge, ingawa na msikia hapa Muungwana anamfagilia Lowasa ila najua anamkonga. Ila sijui umafia wa EL na wanamtandao wenzake kama wataweza kuzima balaa linalowajia...
 
Ki-Protocol Rais anastahili kupewa vyombo kuliko Bunge. Hii kwa katiba ya sasa. may be tukibadilisha . Isije kuwa ile issue ya Adam Malima Vs Mengi ktk vyombo vyake vya Habari...nafikiri hii kesi yafahamika.

JK anaharibu kuanza kushambulia watu ambao walisimama kidete kuamsha umma wa watanzania na wabunge juu ya Richmond...angekaa kimya ingetosha pia kuwa kampeni ya CCM, kuanza kutangaza huku wengi tunaingiwa na mashaka juu ya maamuzi yake.

Kwanza Baraza lenyewe BOMU...may be kikao cha bungeni kiwe kidedea kuutokomeza ufisadi...
 
Kwa mara nyingine tena JK anazima mjadala wa bunge kumhusu Lowassa. Mapema leo mbunge wa Sikonge alikuja juu na kudai chama kiwashughulikie. Sasa wabunge hawa wakijua baadaye kuwa JK amemtetea Lowassa kesho mjadala utaanza kubadilika na watetezi wake wataanza kujitokeza. Wabunge wa CCM ambao wataendelea kulilia 'kichwa cha Lowassa' kwenye sahani wataonekana wanaenda kinyume na Rais.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom