Nikki Mbishi: Maneno ya mashabiki

screpa

JF-Expert Member
Sep 10, 2015
10,788
15,682
Wapenzi wa Hiphop tulitegemea baada ya diss track ya P Mawenge na Unju angekuja na diss track ya kumjibu ila imekuwa tofauti, naona Unju kaachia track yenye maudhui mengine. Sina hakika kama hii ngoma ni mpya, ila kwakuwa nimeiona dakika chache zilizopita kupitia U-Tube naamini ni ngoma mpya, kifupi anazungumzia the way mashabiki huwa wanamzungumzia/ mtazamo wa mashabiki kumuhusu yeye, kiukweli kapita mulemule ambapo mimi huwa namfikiria. Huyu mwana anajua sana kuchana, kwenye top 20 yangu ya G.O.A.Ts wa Hiphop bongo hawezi kukosa, ila anatabia za kikuda sana



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maneno ya mashabiki ni track ya muda mrefu sana
Sikunyingi nimeacha kufatilia Hiphop ya chimbo (underground), zamani ngoma za Tamaduni wazee wa Kilingeni zilikuwa hazinipiti, yaani gheto ni Hiphop kwa kwenda front tena zile zenyewe sio hizi Mainstream, naona uzee unagonga hodi, sikuhizi eti namshabikia Diamond na wabana pua wenzake kweli maisha yanabadilika, vipi Nash MC uchebe anaendeleaje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi nilishasema humu, ule mkwaju wa P umemuathiri kisaikojia, hawezi kutuliza kichwa kujibu anaogopa kutoa kichekesho. Yaani mpaka tunaingia hii weekend, P the MC 4 - Nikki 0.
P huwa namkubali sikunyingi, anachora vizuri sana mashairi, sema alikuwa underrated. Ngoja tusubiri jibu la Unju, navyomjua mimi hawezi kukaa kimya huyu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nini mnataka mazee, mafans hawakuelewi/
zamani walijibu rhymes, Leo imebaki aibu/........................
Hizi ni nyakati za mashaka jiandae kuvuta shati...
Baba Malcom ukiondoa mambo yake ya kumdiss kila mtu ila ni mbaya sana
 
Kama unataka Kiki ongea na Insta mange ......

Huku Baba Malcom kule baba yao
Unju wa siku hizi siyo yule wa zamani anazingua
 
Sikunyingi nimeacha kufatilia Hiphop ya chimbo (underground), zamani ngoma za Tamaduni wazee wa Kilingeni zilikuwa hazinipiti, yaani gheto ni Hiphop kwa kwenda front tena zile zenyewe sio hizi Mainstream, naona uzee unagonga hodi, sikuhizi eti namshabikia Diamond na wabana pua wenzake kweli maisha yanabadilika, vipi Nash MC uchebe anaendeleaje?

Sent using Jamii Forums mobile app
Rudi kundini mkuu, huku hip hop imenoga ma underground wanatoa ngoma kali kinyama kuliko hawa mainstream

Maalim nash katoa ngoma na singasinga ila bado sijaipata ila wametisha mno niliona kwenye intro alipost IG
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom