Nikiwa kama kijana ninasikitika na kuumia kwa kutokuwa na kipato cha kutosha kuendesha maisha. Nahisi kudharaulika na kila mtu

Moniel

JF-Expert Member
Nov 17, 2020
228
553
Mimi ni graduate katika moja ya chuo maarufu hapa Tanzania mwaka huu, Nina miaka 24, nimesomea bachelor of Accounting and Finance

Kutokana na changamoto kadhaa ya ugumu wa ajira na maisha kiujumla nimeamua niwe dereva bodaboda, nilinunua used kutoka kwa hela niliyoipata kwa kusave nikiwa chuo (boom) niliamua kuisafirisha Hadi nyumbani Kanda ya Kati ili niweze kusukuma maisha, ninakaa kwa wazazi baba yangu mzazi na mama yangu wa kambo, kwani mama mzazi alishafariki.

Leo nimeonana na rafiki zangu tuliosoma pamoja, nmekua nikiogopa Hata kufanya kazi hii kwani wengi wanafahamu Mimi nilikua Nina uwezo mkubwa Sana darasani wengine wamekua wakinikejeli kwa mafumbo na misemo ya hovyo mfano "kweli kusoma sio kupata kazi" kila nikikutana na wazee barabarani wananiuliza "umepangiwa wapi," "siku hizi unakazi gani" yaani wanaamimini kwa vyovyote vile nitakua nimepata kazi tu, dah😞

Kazi hii ya bodaboda inaanza kuwa ngumu Sana kwangu, mfano Leo Kuna wadada wamenikuta kijiweni nimepaki , wanabaki kushangaa tu, "yule si Fulani" Yani unaamua kuzuga na kuondoka unaekt Kuna sehem unawahi.

Juzi Kuna abiria kaja ana dharau kweli, we "boda nimesema huku" Hata anavyonielekeza kwake anaelekeza kwa dharau, ukimuuliza wapi anakaa kimya mdada ana nyodo hatari

Kingine kinachoniumiza kichwa ni Hali ya hapa nyumbani, maisha yamekua ni magumu Sana, sometimes najitegemea kwa chakula kwa kula mgahawani, naogopa Hata kumwambia yule mama Kama Kuna msosi alipika, naweza kaa na njaa tu kisa kuogopa kuuliza, Mana sipendi Sana.

Nilinunua kitanda na godoro nilipokua chuo na kuvisafirisha Hadi home ili nije nipange lakini Bei ya pango ni kubwa mno sh 40 kwa mwezi nimeshindwa kulipa kwa miezi 3 120k Kwan hela nayopata inaishia kwenye chakula tu.

Rafiki zangu tuliosoma nao wakafeli Wana maisha mazuri wengi wameoa na wamejenga,m wapo mbali kimaendeleo sana
Nafikiria kivipi nitaweza pata hela nipambane na haya maisha ya mtaani

Kwa yeyote mwenye connection ya kazi yoyote halali mkoa wowote naomba anisaidie, nitaifanya kwa uaminifu na upendo kwani huku napokaa jamii inashindwa kunielewa.
 
Kwa namna fulani umesoma hapa Dar, ungekuwa unapark pale Ubungo Plaza nakuambia usingekuwa unakosa elfu 30 kwa siku na kwa sababu boda boda ni yako, hiyo yote ni hela yako.

Hapa mjini ungeishi kwa amani, usingekutana na hao watu wanaokufahamu mara kwa mara.

Amini nakuambia. Maneno haya.
 
Nakukumbusha baadhi tu ya advantages ulizo nazo:

1. Degree yako
2. Elimu (maana unaonekana unajitambua & kutafuta mafanikio bora)
3. Umri wa 24 yrs
4. Tayari una bodaboda
5. Unaonekana unajua kutunza pesa (uwekevu/iktisari)
6. Unapenda kushauriwa na kujifunza

Don't give up. Usijilinganishe sana na wengine katika namna ya kukukatisha tamaa. Kumbuka hushindani na yeyote hapa duniani. Jitahidi kuweka bidii utafanikiwa tu.

"Uzuri wa jambo lolote lile, uko katikati!"~ Steven Kanumba.
 
Unapoamua kufanya lako usiangalie wa pembeni yako wanasema nini..ili hali wafanya kwa halali umuibii mtu wewe chapa kazi. Tafuta kijiwe chenye wateja fanya kazi yako kwa uaminifu na usisahau kumshirikisha Mungu naamini ipo siku utaona mafanikio.

Usikumwema
 
Mkuu pole sana. Usivunjike moyo. Kikubwa una elimu we go to school so that we can live a meaningful life. Pokea ushauri wa wadau humu jamvin na uutendee kazi muombe Mungu naye akusafishie njia.

Those who lose today will win tomorrow (1500 French saying)
 
Hapo kwenye boda boda ulianza kuitumia degree yako vizuri ila ulivyo kichaa umeona kazi ya uboda boda ni kama kazi teule kwa kundi la watu ambalo Mungu halipendi sio.

KWELI NIMEAMINI ELIMU YA BONGO NI KIWANDA CHA KUTENGENEZA WALALAMISHI,WAVIVU,WACHAGUA KAZI NA WABAGUZI,WAPENDA KUPATA HELA KWA KUBONYEZA KOMPYUTA.Mimi nilimaliza degree nikaingia mtaani na kuanza kufanya kazi ya home teaching then nikaja kuwa mfyatua matofali na kusukuma toroli cha ajabu huko kwenye kufyatua matofali ndipo nikaonwa na nikapata kazi ya ndoto yangu leo hii nikikuambia navyomiliki utashangaa.Ngedere na mademu majinga yaliyokuwa yananicheka na kunibagua leo yanatamani niwe hata mchepuko wao coz nimeshaoa.
 
Hapo kwenye boda boda ulianza kuitumia degree yako vizuri ila ulivyo kichaa umeona kazi ya uboda boda ni kama kazi teule kwa kundi la watu ambalo Mungu halipendi sio.
KWELI NIMEAMINI ELIMU YA BONGO NI KIWANDA CHA KUTENGENEZA WALALAMISHI,WAVIVU,WACHAGUA KAZI NA WABAGUZI,WAPENDA KUPATA HELA KWA KUBONYEZA KOMPYUTA.Mimi nilimaliza degree nikaingia mtaani na kuanza kufanya kazi ya home teaching then nikaja kuwa mfyatua matofali na kusukuma toroli cha ajabu huko kwenye kufyatua matofali ndipo nikaonwa na nikapata kazi ya ndoto yangu leo hii nikikuambia navyomiliki utashangaa.Ngedere na mademu majinga yaliyokuwa yananicheka na kunibagua leo yanatamani niwe hata mchepuko wao coz nimeshaoa.
Zingatia niliyoandika hapo juu kwa sababu kazi utayoanza nayo haimanishi utakufa nayo wakati mwingine hizi kazi za kijungu jiko zinatumika kama ngazi kukupeleka kwenye kazi ya ndoto yako
 
Back
Top Bottom