Nikivipi kusafiri kama kasi ya mwanga kunadhoofisha(kusimamisha)umri kwenda mbele..?

KENZY

JF-Expert Member
Dec 27, 2015
26,213
56,850
Hyperspace.jpg

Hii imekuwa ni moja kati ya dhana ambayo sijaielewa vizuri,iko hivi imekuwa ikisemekana kwamba mtu akiweza kusafiri kama speed ya mwanga unavyosafiri basi ataweza kudhoofisha/kusimamisha umri wake! means kama atasafiri kwa spidi ya mwanga akiwa na miaka 20 hata akirudi hapa duniani ikiwa imepita miaka 100 toka aondoke atarudi vilevile na miaka 20 bila kuzeeka!

sasa nachotaka mimi kujua ni nini kinaathiri mwili mpk umri usisonge..?
au ukisafiri kwa spidi ya mwanga nini kinatokea kwenye mwili mpk kusababisha umri usisonge..?

ni hicho ndicho nachokitakia ufumbuzi kwa anaejua anijuze ili nielewe,mengine tutaendelea kujuzana kadri mjadala utakavyokuwa

karibuni
 
Kwa elimu yangu sina majibu ngoja waje Great Thinkers watatujuza
mkuu nikikosa majibu/wakishindwa kulitetea hili basi jambo hili litakuwa na asilimia 0.0001 kwenye kichwa changu!
 
Nazani hivi.
Ili mtu azeeke lazima cell zife. Lakin ili cell za mwili zife nilazima mfumo wa mwili ufanye kazi yake vizuri, bila ya kuathiriwa na mazingira ya nje. Sas fikiria ukiwa upo kwenye speed ya mwanga (3^8 m/sec), nazan hata mwili huwezi ukawa katika hali yake ya kawaida. Physiological process za za mwili lazima zita simama kwa kipindi chote utachokuw kweny hiyo speed. Note : wanadai kuwa hata ngamia akisafiri kwa speed hiyo, basi ataweza hata kupika kwenye tundu la sindano. Hivyo kwa binadam atakuw mdgo mara 3 kama si 4 ya tundu la sindano na kwa udogo huo anaweza pita hata kwenye blood capillaries.
 
Duuuh mkuu hii ni theory ngumu kidogo kuielezea. Haswa kwa kutumia maandishi. Kwa elimu yangu ndogo ya Fisikia ni kwamba Einsten alikuja na kitu kinaitwa "space of time fabric" ambapo katika theory hio space(nafasi inayochukuliwa na maada yeyote) na muda ni kama kitu kimoja. Na inaweza kuelezewa vizuri kwa kutumia mfano wa kitambaa kilivyo(fabric of cloth) unapokitizama katika 2D na 3D dimension.

Kimsingi ni kwamba maada yoyote(in this case mwili wa binadamu) ikiweza kuonganisha spacetime(timetravel) na kurudi. Maada ile itakua haijabadilika katika kitu chochote kile(hence age) na hapa tofautisha age(kukua na kuzeeka) na time(muda). Kwamba unaweza kuwa na umri wa miaka 20(kwa kuzeeka/kukua/kukaa katika certain point in that fabric). Ila ukawa na time spent in universe ya miaka 100.

Ni theory ngumu kidogo. Ngoja nijaribu kutafuta mifano rahisi nitakuelezea zaidi.

NB:Ili theory hio ifanye kazi inapaswa nguvu(energy) isiwepo. Kwakua energy ikiingia hapo tu inaharibu(distort)???

Wengine mtajazia
 
Nazani hivi.
Ili mtu azeeke lazima cell zife. Lakin ili cell za mwili zife nilazima mfumo wa mwili ufanye kazi yake vizuri, bila ya kuathiriwa na mazingira ya nje. Sas fikiria ukiwa upo kwenye speed ya mwanga (3^8 m/sec), nazan hata mwili huwezi ukawa katika hali yake ya kawaida. Physiological process za za mwili lazima zita simama kwa kipindi chote utachokuw kweny hiyo speed. Note : wanadai kuwa hata ngamia akisafiri kwa speed hiyo, basi ataweza hata kupika kwenye tundu la sindano. Hivyo kwa binadam atakuw mdgo mara 3 kama si 4 ya tundu la sindano na kwa udogo huo anaweza pita hata kwenye blood capillaries.
nadhani ungeeleza nikivipi hizo process za mwili zitasimama kutokana na hiyo speed hapo nitakuelewa.. kusema tu zitasimama sasa si hata moyo utasimama na huyo kiumbe si atakufa!
 
GeoMex nasubiri kwa haja maana hiki kitu hapo tu ndio kinapotia dosari kwangu kutokukielewa
 
Kweny makala flan ya albert estein inayoelezea uvumbizi wake wa ile kanuni ya e=mc2, hilijambo liligusiwa kidogo na kuniacha nikiwa na maswali mengi zaid ya majibu.
Nadhani hyo ndio 1 ya vitu vya msingi ktk masuala ya specific relativity aliyoiandika kwa sehem kubwa.
Mfano uliotumika ni huu *" ukichukua pacha m1 na kumsafirisha kweny space universe kwa kasi ya mwanga basi atarudi akiwa na umri tofauti na yule pacha mwenzie"*
.
.
Nataraji wanajamvi mliopitia vizuri elimu hii mtujuze.
 
nadhani ungeeleza nikivipi hizo process za mwili zitasimama kutokana na hiyo speed hapo nitakuelewa.. kusema tu zitasimama sasa si hata moyo utasimama na huyo kiumbe si atakufa!
Kama ushawahi sikia, kuna baazi ya wanyam wakiwa katika hali ngumu ( namaanisha wakiwa wanapitia hali ngumu ya kimajanga ya asili, mfano njaa, joto au baridi au predators) huwa hawa wanyama wanatumia mechanism fulani kujilinda kwa mfano HIBERNATION. hapa mnyama anakuwa hajafa ila hali chakula, hajamian wala kufany shughuli zingine. Kipindi hiki hata moyo wake huwa unafanya kazi kidogo tofaut na hali ya kawaida. Mwili unatumia chakula kwa kiasi kidogo sana hivyo anaweza kukaa mda mrefu bila kupata chakula. Hivyo kwa habari hiyo hata miili yetu ikiwswa inactivated. Moyo hauta simama lkn utafanya kazi kwa kiasi kidogo sana, hivyo ataweza kuishi kabisa. Pia kumbuka kuna teknolojia ziligunduliwa zikisema mtu anaweza akahifadhiwa akiwa na miaka 20, kwa mda wa miaka mia. Akija kuamshwa atakuw ktk umri uleule aliohifadhiwa.
Note; haya niliyo toa ni maoni tyu sio habari ya kuaminika iliyo chunguzwa kisayansi. Pia si zan kama mtu anaweza safiri kwa speed hiyo, Maana hata NASA hawana hiyo tekinoloji ktk kuendesha spaceship zake.
 
When the gravitational force is so strong time also tends to slow down, miller's planet jamaa walienda wakaspend masaa machache tu waliporudi wakakuta wenzao waliowaacha ni wazee tayari miaka ilipita almost 20 waliokoenda 2 seconds zilikuwa ni sawa na 20 hours walikotoka. Refer "interstellar" movie
 
boniuso nashukuru kwa maelezo yako hapo juu lkn bado hayajajibu swali langu! kuhusu huko kustopisha mtu kwa tecknolojia hilo si geni ila kuhusu kusafiri kama kasi ya mwanga hapa ndipo napopataka
 
Nachojua mm gravity inplay part kubwa mtu kuzeeka that's why wazee wanajikunja fluid zikiisha kwenye spinal cord nguvu dhidi ya gravity inapungua, wanawake matiti kushuka as time goes by
 
Hyperspace.jpg

Hii imekuwa ni moja kati ya dhana ambayo sijaielewa vizuri,iko hivi imekuwa ikisemekana kwamba mtu akiweza kusafiri kama speed ya mwanga unavyosafiri basi ataweza kudhoofisha/kusimamisha umri wake! means kama atasafiri kwa spidi ya mwanga akiwa na miaka 20 hata akirudi hapa duniani ikiwa imepita miaka 100 toka aondoke atarudi vilevile na miaka 20 bila kuzeeka!

sasa nachotaka mimi kujua ni nini kinaathiri mwili mpk umri usisonge..?
au ukisafiri kwa spidi ya mwanga nini kinatokea kwenye mwili mpk kusababisha umri usisonge..?

ni hicho ndicho nachokitakia ufumbuzi kwa anaejua anijuze ili nielewe,mengine tutaendelea kujuzana kadri mjadala utakavyokuwa

karibuni
Einstein theory of relativity:
There is so called Time dilation which is the time difference between the two events. Example, imagine uko mwenge Saa 2:00 inabidi ufike posta kwA muda wa Saa 2 kwenda na kurud hence Uend posta alf urud mwenge Saa 4:00 .clock moja umeiacha mwenge nyingine unayo mfukoni let's say una speed ya jet kwenda posta na kurud mwenge . Ukirudi mwenge utapata majibu haya kwenye Saa zako :
Saa uliyo iacha mwenge itakuambia Umetumia 2hrs hence now ni 4:00 which is exerctly.
Saa uliyo tembea nayo itakuambia kuwa Umetumia 1hr and hence yenyewe itakuambia now ni Saa 3:00. The difference in time ie time dilation btn the clocks is 4-3=1hr . In short clock in motion is slower than the stationary clock due to relative velocity and gravity difference btn the two clocks from the inertial frame of reference. If the relative speed is high let's say inakaribia speed ya light bas utegemee moving clock kutumia lesser time than the stationary one and this is the reason why astronauts in space will not get old easily due to that they are traveling with high relative speed when they return on earth they seem to use much less time than the one's who left on the earth....
.....


Mzee Bado au Unataka ipigwe Einstein theory of relativity yote?
 
Niliona hii theory kwenye movie ya interstellar nikatoka kapa.
 
Physics ya A level ilitosha kabisa kuumiza kichwa mpaka nikaapa sisomi tena hayo makitu.

Sasa kwa mada ngumu kama hii, naona tunarudishana kulekule
 
Ipo hivi:

Kwanza ukae ukijua, kamwe huwezi kusafiri na kufikia mwendo kasi wa mwanga, kwa sababu nguvu inayotakiwa ni kubwa sana.

Pale kasi yako inapoongezeka, uzito wako pia huongezeka (ukilinganisha na uzito wako ukiwa umetulia tu), kwa hiyo nguvu itakayohitaji kukusukuma ni kubwa sana.


Endapo utafanikiwa kufikia mwendo kasi wa mwanga, Muda nao husimama kusonga kabisa.
Tuseme unasafiri kwa asilimia 99 ya mwendo kasi wa mwanga, hii itapelekea muda kupungua kasi yake ya kawaida mara 7 kwako, tofauti na yule aliyekaa akikutazama.

Endapo utasafiri kwa mwendo huu kwa mwaka , utamuona yule anayekuangalia akiwa katulia miaka yake 7 imepita wakati unasafiri. Wakati huo ukiwa unamuangalia ukiwa angani. Utamuona yeye akifikia miaka saba sivyo kawaida, haraka sana yani. Ni kama vile uwe umeshikilia remote ya TV alafu ushikilie fast-forwading, utawaona wanafanya vitu kwa speed ya mara 7 zaidi yako wewe, wakati wewe watakuona unafanya vitu taratibu mara 7yake.

Endapo utaamua kusimama, utajikuta wenzako wamesogea mbele kwa miaka 7, wakati wewe umesogea mwaka 1 tu.

Kwa hiyo wewe utajikuta umesogea mwaka 1 tu, ilo upo mdogo kwa miaka7, wakati wenzako washasonga mbele kwa miaka 7.

Kama ulikuwa una miaka 20. Na ukaamua kusafiri kwa mwendo kasi wa mwanga kwa mwaka1 alafu ukasimama. Utajikuta unamiaka 21, ila wenzako wana miaka 27.

Cc: mahondaw
 
boniuso nashukuru kwa maelezo yako hapo juu lkn bado hayajajibu swali langu! kuhusu huko kustopisha mtu kwa tecknolojia hilo si geni ila kuhusu kusafiri kama kasi ya mwanga hapa ndipo napopataka

Kuhusu hapo alipoelezea mkuu boniuso ngoja nikupe mfano rahisi labda utapata mwanga.

Hicho kipimo chako cha moyo kufanya kazi unahesabu mapigo 72-100 kwa dakika(sekunde 60) at a certain space(point) in universe. Sasa fikiria huyo binadamu akaweza kumove kutoka space moja kwenda nyingine in universe(spacetime)in the same fabric. Sio kwa sekunde moja(ambayo ni mapigo 1.6.....) ila chukulia kwa millisecond au nanosecond huo moyo utadunda kwa mapigo kias gani(~aprox 0) hivo basi mtu anaweza akaenda katika space nyingine na kuexist na kurudi akiwa kapitisha muda(time) mrefu ila umri ule ule(age) kutokana na muda wa kuhama kutoka space moja kwenda nyingine kuwa ndogo mno kuweza kubadilisha umri.

Mfano wa pili. Katika dunia tu(same space) kuna uwezekano wa watu kutoka sehemu tofauti kuwa na birthday moja ila umri tofauti(kutokana na mzunguko wa dunia east na west) sasa pata picha mtu ambaye ana birthday moja na watu hao hao wawili walioko mabara tofauti na wakawa na umri tofauti at a certain point of time(their birthday eve for example). Sasa huyu mtu wa tatu tuseme hayuko mbali yupo hapo juu tu ISS(iko km 400 tu kutoka duniani) sasa mtu huyu aliondoka akiwa na umri sawa na wale jamaa wawili tayari wana umri tofauti katika siku hiyo. Hapo utajikuta una 3cariables tayari umri wa jamaa wa kwanza wa east atategemewa kutangulia kuwa mkubwa kwa namba ya miaka atafuatiwa na jamaa wa west. Na je yule aliyekua space station at that moment ana umri gani? Na je akitua east atakua na umri gani? Akitua west je?(kumbuka na kuzeeka kunachangiwa na functions za ubongo pia) na hili unaweza kulithibitisha hata kwa jet lagging tu pale unaposafiri na ndege kwenda west ya dunia huwa ubongo unahangaika kuadjust kuishi the same day in your life twice.

Sasa huo ni utangulizi(kwa huyu jamaa aliyekua 400km from earth surface. Fikiria sasa mtu huyu(teknolojia ikiwepo) aweze kusafiri zaidi ya km 400 kwenda huko mbali kwenye intergalactic planetary universe(kwa spidi ya mwanga) umbali atakaokuwepo ni hundreads million light years.

Hivyo basi akiweza kwenda na kurudi atawakuta wenzake wana umri mkubwa kuliko yeye. Hata kama kwake itakua ni blink of a second.

Duuuuh... sijui unanisoma?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom