Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,988
Habari zenu watani, mabibi nanyi mabwana,
Miye nawasalimuni, kindugu siyo kitwana,
Na beti zangu someni, ni hizi za kiungwana,
Nina vyakula viwili, nichague kipi kwanza?
Ninayo njaa mwenzenu, na tumbo linanguruma,
Sasa nimepewa menu, si ya wali wala sima,
Si vya kula vya kikwenu, vya kigeni natazama,
Nina vyakula viwili, nichague kipi kwanza?
Cha moto hicho cha kwanza, meza imeandaliwa,
Harufu inapendeza, Hanifa kakipakuwa,
sasa nataka kuanza, msosi kuuchukuwa,
Nina vyakula viwili nichague kipi kwanza?
Lakini hicho cha moto, kinahitaji subira,
Hakimfai mtoto, wala kula kwa papara,
Nangojea kama loto, nisikile kwa hasira,
Nina vyakula viwili nichague kipi kwanza?
Kingine ni cha baridi, kimeandikwa mezani,
Mdomoni chakaidi, hakiingii kinywani,
Amenipa Mwanaidi, ati nikile jamani,
Nina vyakula viwili, nichague kipi kwanza?
Kasema ati kitamu, nikikila cha baridi,
Nitajilamba kwa hamu, kama ni siku ya Idi,
Kakipika kitaalamu, hivyo nisije kaidi,
Nina vyakula viwili, nichague kipi kwanza?
Mwenzenu sasa natingwa, midomo naumauma,
Naona sasa nategwa, ninayo hamu ya nyama,
Ninajiona mfungwa, wa njaa inayouma,
NIna vyakula viwili, nichague kipi kwanza?
Kalamu naweka chini, kichwa changu najikuna,
Kosa langu mimi nini, nachombezwa kiana,
Viwili vyote vya nini, ubaya twatafutana,
Nina vyakula viwili, nichague kipi kwanza?
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)
Miye nawasalimuni, kindugu siyo kitwana,
Na beti zangu someni, ni hizi za kiungwana,
Nina vyakula viwili, nichague kipi kwanza?
Ninayo njaa mwenzenu, na tumbo linanguruma,
Sasa nimepewa menu, si ya wali wala sima,
Si vya kula vya kikwenu, vya kigeni natazama,
Nina vyakula viwili, nichague kipi kwanza?
Cha moto hicho cha kwanza, meza imeandaliwa,
Harufu inapendeza, Hanifa kakipakuwa,
sasa nataka kuanza, msosi kuuchukuwa,
Nina vyakula viwili nichague kipi kwanza?
Lakini hicho cha moto, kinahitaji subira,
Hakimfai mtoto, wala kula kwa papara,
Nangojea kama loto, nisikile kwa hasira,
Nina vyakula viwili nichague kipi kwanza?
Kingine ni cha baridi, kimeandikwa mezani,
Mdomoni chakaidi, hakiingii kinywani,
Amenipa Mwanaidi, ati nikile jamani,
Nina vyakula viwili, nichague kipi kwanza?
Kasema ati kitamu, nikikila cha baridi,
Nitajilamba kwa hamu, kama ni siku ya Idi,
Kakipika kitaalamu, hivyo nisije kaidi,
Nina vyakula viwili, nichague kipi kwanza?
Mwenzenu sasa natingwa, midomo naumauma,
Naona sasa nategwa, ninayo hamu ya nyama,
Ninajiona mfungwa, wa njaa inayouma,
NIna vyakula viwili, nichague kipi kwanza?
Kalamu naweka chini, kichwa changu najikuna,
Kosa langu mimi nini, nachombezwa kiana,
Viwili vyote vya nini, ubaya twatafutana,
Nina vyakula viwili, nichague kipi kwanza?
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)