cocastic
JF-Expert Member
- Nov 30, 2019
- 85,462
- 137,062
Watu wa hivyo wapo sana wala sishangai.
kuna dogo mmoja tulimtoa bush huko akaletwa Dar kuuza Duka!
Kabla ya Dogo kuja mauzo yalikua laki 2 max.
Baada ya Dogo kuja biashara ikaanza kupaa mdogo mdogo, anauza peke yake mpaka laki 9 wakati mwingine anagonga hadi milioni.
Ule mtaa ulikuwa na maduka kama 10 hivi lakini cha ajabu wengine wakawa wanauza kidogo sana kulinganisha na duka alilokuwa dogo.
ikafikia hatua akaitwa msukule.
basi Bwana walimwengu hawana wema kabisa, Dogo kafanya kazi kwa Moyo, kuamka saa kumi alfajiri, kulala saa sita usiku lakini cha ajabu boss akamzulumu mshahara wa miezi mitatu
Dogo kaona isiwe shida, katoroka dukani na kama laki 1 hivi, elfu 60 ya tiketi mpaka kwao, 40 ikawa ya emergence..
Dogo kaamsha mpaka kwao kijijini huko kaacha Duka.
Wiki nyingi aisee wateja wakaanza kupungua, mmoja baada ya mwingine, duka likaporomoka kwa speed ya airforce
Boss kaamua kubembeleza tena ili Dogo arudi...
Dah ntarejea..