Avanti
JF-Expert Member
- Aug 24, 2010
- 1,209
- 239
Ni pekee ninayemwona ana udhati wa moyoni wa upendo wa nchi yake. Ameshaongea mengi ambayo ni makubwa na yanaweza hata kumgharimu kwa vyovyote vile lakini ameyasema. Ni mtendaji wa uhakika, hana hata chembe ya kashfa yeyote, ana uwezo mkubwa kiakili na hawezi kukosa kazi nzuri zaidi ya hii ya siasa anayoifanya akaishi maisha yake mazuri mno.
Kwao anakubalika ni mtu wa watu na hajibagui nao anapokuwa kule, nina uhakika na hili kwa kuwa ni mtani wangu ambaye ni rafiki yangu ndugu yake amenieleza hili. Tundu Lisu, nimewahi kuongea naye tukiwa kwenye mkutano wa wanasheria Arusha, ukweli he is a son of peasant and of the people.
Hata ndugu yake Alute naye sio mtu wa kudharaulika, ana hekima sana na ndiyo maana yeye na mdogo wake pamoja na kuwa vyama tofauti bado wapo pamoja na wanacheza siasa nzuri. Nakumbuka katika mkutano wa hivi karibuni kule Arusha Alute akichangia kujadili presentation ya Lisu alimwuliza inakuwaje sisi Tanzania tunataka Katiba yetu ipunguze nguvu ya Raisi katika maamuzi wakati Katiba za wenzetu kama Marekani wameimarisha nguvu za Raisi katika Katiba (Have you contemplated the effects of having a weak president in decision making?). Tulipotoka nje ya mkutano nilimchombeza Lisu kuhusu hoja ya kaka yake ambayo hakupata nafasi ya kuijibu mkutanoni na akaniambia ama kaka yake hakumwelewa vizuri kuhusu hilo ama yeye hakuelewesha vizuri.
Wana JF kikubwa ninachotaka kusema, ukweli unabaki pale pale kwamba kwangu mimi Tundu Lisu ndiye mwanasiasa ninayeamini ana utashi wa dhati na ni msafi hadi moyoni mwake. Kama huwa anapitia JF basi atambue kuwa kuna mtu angalau anamtazama katika taswira ya namna hii na ajiimarishe katika hili bila kujalisha anaweza kuja kuwa Raisi wetu ama la! Thawabu zake kwa Mungu zipo.
Kwao anakubalika ni mtu wa watu na hajibagui nao anapokuwa kule, nina uhakika na hili kwa kuwa ni mtani wangu ambaye ni rafiki yangu ndugu yake amenieleza hili. Tundu Lisu, nimewahi kuongea naye tukiwa kwenye mkutano wa wanasheria Arusha, ukweli he is a son of peasant and of the people.
Hata ndugu yake Alute naye sio mtu wa kudharaulika, ana hekima sana na ndiyo maana yeye na mdogo wake pamoja na kuwa vyama tofauti bado wapo pamoja na wanacheza siasa nzuri. Nakumbuka katika mkutano wa hivi karibuni kule Arusha Alute akichangia kujadili presentation ya Lisu alimwuliza inakuwaje sisi Tanzania tunataka Katiba yetu ipunguze nguvu ya Raisi katika maamuzi wakati Katiba za wenzetu kama Marekani wameimarisha nguvu za Raisi katika Katiba (Have you contemplated the effects of having a weak president in decision making?). Tulipotoka nje ya mkutano nilimchombeza Lisu kuhusu hoja ya kaka yake ambayo hakupata nafasi ya kuijibu mkutanoni na akaniambia ama kaka yake hakumwelewa vizuri kuhusu hilo ama yeye hakuelewesha vizuri.
Wana JF kikubwa ninachotaka kusema, ukweli unabaki pale pale kwamba kwangu mimi Tundu Lisu ndiye mwanasiasa ninayeamini ana utashi wa dhati na ni msafi hadi moyoni mwake. Kama huwa anapitia JF basi atambue kuwa kuna mtu angalau anamtazama katika taswira ya namna hii na ajiimarishe katika hili bila kujalisha anaweza kuja kuwa Raisi wetu ama la! Thawabu zake kwa Mungu zipo.