Nijulisheni taratibu na vigezo vya kujiunga na uber

ichenjezya

JF-Expert Member
Sep 26, 2013
1,010
1,119
Habari, naomba kujua taratibu na vigezo vya kujiunga na Uber kwa sasa vikoje, nina kagari kangu nataka nijiunge huko, msaada kwa anaejua alie na current information.....asanteni!

======

1.Gari lako liwe limetengenezwa kiwandani kuanzia mwaka 2001,aidha iwe sedan au hatchback itapendeza zaidi,na liwe na uwezo wa kubeba abiria wanne.

2. Utahitajika kubadilisha usajili wa gari lako kutoka kuwa private car hadi commercial car hivyo kadi ya gari lako itabidi ukabadili ikiwa ni pamoja na number plate kuweka nyeupe.

3. Kama utaendesha gari wewe mwenyewe inabidi uwe na driving licence with class A B C1 C2 C3 D na E pamoja na hati ya kipolisi ya tabia njema,"police clearance certificate" inayotolewa makao makuu ya polisi.

4. Uwe na smartphone.

5. Uwe ni mkazi wa jiji la dar.

6. Ukishakuwa na vigezo vyote hivyo karibu sana ofisini Viva tower kila siku za wiki Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 9 alasiri
 
Habari,naomba kujua taratibu na vigezo vya kujiunga na Uber kwa sasa vikoje,nina kagari kangu nataka nijiunge huko,msaada kwa anaejua alie na current information.....asanteni!
Nenda pale viva tower, posta karibu na serena hotel. Mwinyi Road
Ndio kuna ofisi zao utapata utaratibu mzima
 
Nenda pale viva tower, posta karibu na serena hotel. Mwinyi Road
Ndio kuna ofisi zao utapata utaratibu mzima
Thanks mkuu,napafahamu ila nilikua nataka kama kuna alie na taarifa za hivi karibuni,kabla sijaenda ili nijue kabisa!
 
Thanks mkuu,napafahamu ila nilikua nataka kama kuna alie na taarifa za hivi karibuni,kabla sijaenda ili nijue kabisa!

1.Gari lako liwe limetengenezwa kiwandani kuanzia mwaka 2001,aidha iwe sedan au hatchback itapendeza zaidi,na liwe na uwezo wa kubeba abiria wanne.

2. Utahitajika kubadilisha usajili wa gari lako kutoka kuwa private car hadi commercial car hivyo kadi ya gari lako itabidi ukabadili ikiwa ni pamoja na number plate kuweka nyeupe.

3. Kama utaendesha gari wewe mwenyewe inabidi uwe na driving licence with class A B C1 C2 C3 D na E pamoja na hati ya kipolisi ya tabia njema,"police clearance certificate" inayotolewa makao makuu ya polisi.

4. Uwe na smartphone.

5. Uwe ni mkazi wa jiji la dar.

6. Ukishakuwa na vigezo vyote hivyo karibu sana ofisini Viva tower kila siku za wiki Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 9 alasiri
 
1.Gari lako liwe limetengenezwa kiwandani kuanzia mwaka 2001,aidha iwe sedan au hatchback itapendeza zaidi,na liwe na uwezo wa kubeba abiria wanne.
2. Utahitajika kubadilisha usajili wa gari lako kutoka kuwa private car hadi commercial car hivyo kadi ya gari lako itabidi ukabadili ikiwa ni pamoja na number plate kuweka nyeupe.
3. Kama utaendesha gari wewe mwenyewe inabidi uwe na driving licence with class A B C1 C2 C3 D na E pamoja na hati ya kipolisi ya tabia njema,"police clearance certificate" inayotolewa makao makuu ya polisi.
4. Uwe na smartphone.
5. Uwe ni mkazi wa jiji la dar.
6. Ukishakuwa na vigezo vyote hivyo karibu sana ofisini Viva tower kila siku za wiki jumatatu hadi ijumaa kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 9 alasiri
Gari chini ya mwaka 2001,haikubaliwi kwa nini?Na naweza kupatiwa dereva?Wa kuendesha gari,niliyo nayo?
 
Gari chini ya mwaka 2001,haikubaliwi kwa nini?Na naweza kupatiwa dereva?Wa kuendesha gari,niliyo nayo?
Njoo pm nikupe dereva aliekuwa registered,ikumbukwe pia si kila dereva anaweza kuendesha uber maana ni mpaka awe amepatiwa trainings wanazotoa wao uber wenyewe na kisha ndio awe registered.
 
Gari chini ya mwaka 2001,haikubaliwi kwa nini?Na naweza kupatiwa dereva?Wa kuendesha gari,niliyo nayo?
Gari chini ya 2001 haikubaliwi kwa sababu linakuwa ni too old,hivyo linaweza kuwa na uchakavu fulani ambapo halitakidhi kubeba abiria,
#by the way wewe una gari gani?
 
1.Gari lako liwe limetengenezwa kiwandani kuanzia mwaka 2001,aidha iwe sedan au hatchback itapendeza zaidi,na liwe na uwezo wa kubeba abiria wanne.
2. Utahitajika kubadilisha usajili wa gari lako kutoka kuwa private car hadi commercial car hivyo kadi ya gari lako itabidi ukabadili ikiwa ni pamoja na number plate kuweka nyeupe.
3. Kama utaendesha gari wewe mwenyewe inabidi uwe na driving licence with class A B C1 C2 C3 D na E pamoja na hati ya kipolisi ya tabia njema,"police clearance certificate" inayotolewa makao makuu ya polisi.
4. Uwe na smartphone.
5. Uwe ni mkazi wa jiji la dar.
6. Ukishakuwa na vigezo vyote hivyo karibu sana ofisini Viva tower kila siku za wiki jumatatu hadi ijumaa kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 9 alasiri
Aisee mambo magumu sana,kwaiyo sitaruhusiwa kuendesha UBER mpaka nichange from private to commercial,alafu kuhusu leseni mimi ya kwangu haina daraja C hizo,kwa hiyo sitaruhusiwa kuendesha?
 
Aisee mambo magumu sana,kwaiyo sitaruhusiwa kuendesha UBER mpaka nichange from private to commercial,alafu kuhusu leseni mimi ya kwangu haina daraja C hizo,kwa hiyo sitaruhusiwa kuendesha?

Sio kuruhusiwa kuendesha tu bali hautosajiliwa maana yake app yako ya uber driver haitokuwa activated ili uweze kuingia barabarani,na pia hautoweza kupewa trainings maana sio unakurupuka tu unaingia barabarani kubeba abiria inatakiwa upitie mafunzo ya kubeba abiria.

C1. Hii unaendesha costa zote
C2. Hii unaendesha daladala hiace zote
C3. Hii unaendesha tax zote

Sasa hizi C hupewi moja zinatoka kwa series zote tatu hivo ukitoka chuoni na cheti chako ndipo unaenda tra kuomba kuongeza madaraja na ambatanisha na leseni yako ya daraja D.

Na pia ikumbukwe huwezi kupewa hizo C mpaka uwe na class E hivyo automatically mpaka unapata hiyo C 3 utakuwa na class A B C1 C2 C3 D Na E.

Hivyo kwa urahisi ni wewe kupatiwa dereva aliekuwa registered tayari umpe gari awe anakuletea hesabu yako, simple like that!
 
Sio kuruhusiwa kuendesha tu bali hautosajiliwa maana yake app yako ya uber driver haitokuwa activated ili uweze kuingia barabarani,na pia hautoweza kupewa trainings maana sio unakurupuka tu unaingia barabarani kubeba abiria inatakiwa upitie mafunzo ya kubeba abiria.
C1. Hii unaendesha costa zote
C2. Hii unaendesha daladala hiace zote
C3. Hii unaendesha tax zote
Sasa hizi C hupewi moja zinatoka kwa series zote tatu hivo ukitoka chuoni na cheti chako ndipo unaenda tra kuomba kuongeza madaraja na ambatanisha na leseni yako ya daraja D.
Na pia ikumbukwe huwezi kupewa hizo C mpaka uwe na class E hivyo automatically mpaka unapata hiyo C 3 utakuwa na class A B C1 C2 C3 D Na E.
Hivyo kwa urahisi ni wewe kupatiwa dereva aliekuwa registered tayari umpe gari awe anakuletea hesabu yako,simple like that!
Taenda nikajiridhishe haya unayoniambia mkuu,lakini mimi kumpa dereva wa Dar es salaam haitakaa itokee,kwanza naamini lazima biashara iyo ile kwangu na kagari kangu kapya katachakaa,bora niendelee kupiga nalo picha,lakini hawa madereva wahuni wa Dar watanipa stress za bure!
 
Taenda nikajiridhishe haya unayoniambia mkuu,lakini mimi kumpa dereva wa Dar es salaam haitakaa itokee,kwanza naamini lazima biashara iyo ile kwangu na kagari kangu kapya katachakaa,bora niendelee kupiga nalo picha,lakini hawa madereva wahuni wa Dar watanipa stress za bure!
Haya mkuu ila simply uber ni tax na leseni ya kuendesha tax ni C3 sasa huwezi tu kuwa na C3 lazma tu utakuwa na yote hayo na pia trafiki akiona namba nyeupe tu gari ndogo lazma anajua ni uber hvyo atakupiga mkono sasa akukute una D huo moto atakaokuwakia!!
Nb;madereva wa uber sio kama wa daladala,ila sawa nenda ofisini procedures ndio kama hizo nilizokupa japo ni ndefu ila kama una nia naamini utapita zote
 
Taenda nikajiridhishe haya unayoniambia mkuu,lakini mimi kumpa dereva wa Dar es salaam haitakaa itokee,kwanza naamini lazima biashara iyo ile kwangu na kagari kangu kapya katachakaa,bora niendelee kupiga nalo picha,lakini hawa madereva wahuni wa Dar watanipa stress za bure!
Kwa kukusaidia tu ingia playstore au appstore kisha download App ya Uber driver kisha install then signup kwa kuanza kujaza taarifa zako muhimu ku'upload documents muhimu kama vile driving licence yako,hati ya tabia njema kisha mdogo mdogo jongea ofisini mkuu,kila la heri.
 
1.Gari lako liwe limetengenezwa kiwandani kuanzia mwaka 2001,aidha iwe sedan au hatchback itapendeza zaidi,na liwe na uwezo wa kubeba abiria wanne.
2. Utahitajika kubadilisha usajili wa gari lako kutoka kuwa private car hadi commercial car hivyo kadi ya gari lako itabidi ukabadili ikiwa ni pamoja na number plate kuweka nyeupe.
3. Kama utaendesha gari wewe mwenyewe inabidi uwe na driving licence with class A B C1 C2 C3 D na E pamoja na hati ya kipolisi ya tabia njema,"police clearance certificate" inayotolewa makao makuu ya polisi.
4. Uwe na smartphone.
5. Uwe ni mkazi wa jiji la dar.
6. Ukishakuwa na vigezo vyote hivyo karibu sana ofisini Viva tower kila siku za wiki jumatatu hadi ijumaa kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 9 alasiri
Kwa class D inafaa mkuu?
Mambo yakienda kombo niingie huku
 
Serikali ya Tanzania wanakawaida ya kuweka mambo yawe magumu kwa raia kwa kuweka marundo kama sio msururu wa mahatua yasiyo na mantiki yoyote.....

UBER kwenye mataifa yaliyoendelea ni very simple na haina complications......maana wanajua kuwa uber imekuja kuwa universal driving business na anyone mwenye gari yake ambayo ipo vema na ina hali nzuri na dereva mwenye busara zake anaweza kuifanya bila kuhangaika na hayo madaraja ya leseni.

Ila kama ilivyo kawaida ya serikali na watendaji wake wasio na huruma na watoto wa wenzao, kutwa kucha ni kubuni njia mpya za kubana ili wale wasionacho wazidi kupunyuka.....

Wataka nambia kuwa swala la plate number ulaya lipo, swala la haya madaraja ya leseni mengi kama madumu ya maji uswazi ulaya yatakuwapo?!

Ni hapa tu bongo tunakuwa na taratibu zisizo za lazima katika bishara na ndio maana mambo hayaendi......full vikwazo na kupiga piga fine za kijinga jinga na kutoa wananchi pesa isivyolazima....


Serikali ina mambo ya ajabu sana sometimes..... Aaaaaaaagh
 
Serikali ya Tanzania wanakawaida ya kuweka mambo yawe magumu kwa raia kwa kuweka marundo kama sio msururu wa mahatua yasiyo na mantiki yoyote.....

UBER kwenye mataifa yaliyoendelea ni very simple na haina complications......maana wanajua kuwa uber imekuja kuwa universal driving business na anyone mwenye gari yake ambayo ipo vema na ina hali nzuri na dereva mwenye busara zake anaweza kuifanya bila kuhangaika na hayo madaraja ya leseni.

Ila kama ilivyo kawaida ya serikali na watendaji wake wasio na huruma na watoto wa wenzao, kutwa kucha ni kubuni njia mpya za kubana ili wale wasionacho wazidi kupunyuka.....

Wataka nambia kuwa swala la plate number ulaya lipo, swala la haya madaraja ya leseni mengi kama madumu ya maji uswazi ulaya yatakuwapo?!

Ni hapa tu bongo tunakuwa na taratibu zisizo za lazima katika bishara na ndio maana mambo hayaendi......full vikwazo na kupiga piga fine za kijinga jinga na kutoa wananchi pesa isivyolazima....


Serikali ina mambo ya ajabu sana sometimes..... Aaaaaaaagh
Hii serikali nami naishangaa sana. Leo eti ukipita ile njia ya hongera bar kuja kutokea sayansi; ukifika pale sayansi junction hutakiwi kula kulia. Trafki anaacha kuongoza magari anakuvaa! unapigwa cheti. Thanks kwa wasamalia wakanitonya mapema ila nimeshuhudia jamaa anasimamishwa kama jambazi!!
 
1.Gari lako liwe limetengenezwa kiwandani kuanzia mwaka 2001,aidha iwe sedan au hatchback itapendeza zaidi,na liwe na uwezo wa kubeba abiria wanne.
2. Utahitajika kubadilisha usajili wa gari lako kutoka kuwa private car hadi commercial car hivyo kadi ya gari lako itabidi ukabadili ikiwa ni pamoja na number plate kuweka nyeupe.
3. Kama utaendesha gari wewe mwenyewe inabidi uwe na driving licence with class A B C1 C2 C3 D na E pamoja na hati ya kipolisi ya tabia njema,"police clearance certificate" inayotolewa makao makuu ya polisi.
4. Uwe na smartphone.
5. Uwe ni mkazi wa jiji la dar.
6. Ukishakuwa na vigezo vyote hivyo karibu sana ofisini Viva tower kila siku za wiki jumatatu hadi ijumaa kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 9 alasiri
Na tunaohitaji usafiri huo utaratibu wa kujiunga ukoje ?
 
Kwa class D inafaa mkuu?
Mambo yakienda kombo niingie huku
Class D haifai mkuu maana bado ni ndogo sana,jitahidi ukasome HGV upate class E then ukasome PSV pale NIT then ukaongeze C1 C2 na C3 ndio utaruhusiwa kuendesha uber ukishakidhi vigezo.
Nb;vigezo na masharti kuzingatiwa.
 
Na tunaohitaji usafiri huo utaratibu wa kujiunga ukoje ?
Chukua simu yako ingia playstore kwa androia au appstore kwa iphone then download uber app,kisha jisajili then washa location,furahia popote uendapo kwa gharama nafuu kabisa wakati wote.
 
Hivyo kwa urahisi ni wewe kupatiwa dereva aliekuwa registered tayari umpe gari awe anakuletea hesabu yako,simple like that!
Je waweza kutupatia dokezo kuhusu kiasi ambacho kwa wamiliki walio wengi huitaji kuletewa kwa siku? Ni kati ya TZS ngapi hadi ngapi kwa siku?
 
Chukua simu yako ingia playstore kwa androia au appstore kwa iphone then download uber app,kisha jisajili then washa location,furahia popote uendapo kwa gharama nafuu kabisa wakati wote.
Asante sana Mkuu. Gharama za texi zimenitesa sana hapo Dar.
 
Back
Top Bottom