Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Takriban watu saba wameuawa katika vita ambavyo vilizuka baada ya msichana wa dini ya Kikristo kubadili dini na kuwa Muislamu Kaskazini magharibi mwa Nigeria.
Vita hivyo vilivyozuka katika jimbo la Kaduma viliwaacha watu 15 wakiwa na majeraha baada ya nyumba kuchomwa moto.
Shahidi mmoja aliiambia BBC kwamba tatizo lilianza baada ya msichana huyo wa Kikristo kutoka Gwari kubadili dini na kuwa Muislamu kutokana na ushawishi wa mpenzi wake.
Shahidi anasema kuwa tatizo hilo liliwachochea vijana wa Kikristo.
Ripoti nyingine zinasema kuwa wasiwasi kati ya wafuasi wa dini hizo mbili ulikiwa tangu awali.
Hata hivyo Kamanda wa Polisi wa Kaduma Muktar Aliyu aliiambia BBC kwamba huku wakifanikiwa kuwakamata watu 10 wanaohusiana na kisa hicho, maafisa bado wanachunguza sababu ya vita hivyo.
"Hatuwezi kuthibitisha kwamba vita vilizuka kwa sababu kuna mtu alibadilisha dini na kuwa Muislamu ama dini nyingine yoyote ile", alisema.
Watu wana haki ya kubadili dini na kuingia dini nyingine yoyote ile, hatua hiyo haifai kuchochea vita".
Chanzo: BBC
Vita hivyo vilivyozuka katika jimbo la Kaduma viliwaacha watu 15 wakiwa na majeraha baada ya nyumba kuchomwa moto.
Shahidi mmoja aliiambia BBC kwamba tatizo lilianza baada ya msichana huyo wa Kikristo kutoka Gwari kubadili dini na kuwa Muislamu kutokana na ushawishi wa mpenzi wake.
Shahidi anasema kuwa tatizo hilo liliwachochea vijana wa Kikristo.
Ripoti nyingine zinasema kuwa wasiwasi kati ya wafuasi wa dini hizo mbili ulikiwa tangu awali.
Hata hivyo Kamanda wa Polisi wa Kaduma Muktar Aliyu aliiambia BBC kwamba huku wakifanikiwa kuwakamata watu 10 wanaohusiana na kisa hicho, maafisa bado wanachunguza sababu ya vita hivyo.
"Hatuwezi kuthibitisha kwamba vita vilizuka kwa sababu kuna mtu alibadilisha dini na kuwa Muislamu ama dini nyingine yoyote ile", alisema.
Watu wana haki ya kubadili dini na kuingia dini nyingine yoyote ile, hatua hiyo haifai kuchochea vita".
Chanzo: BBC