Nigeria: Watakaokaidi agizo la Serikali kufungia Twitter kukabiliana na mkono wa sheria

Sam Gidori

Senior Member
Sep 7, 2020
165
414
Mwanasheria Mkuu wa Nigeria, Jenerali Abubakar Malami ameagiza kufunguliwa mashtaka mara moja kwa watu wote watakaokaidi agizo la serikali la kufungia mtandao wa kijamii wa Twitter.

Mapema jana, makampuni ya simu nchini humo yalisema kuwa yametii agizo la serikali la kufungia mtandao huo wa kijamii, ikiwa ni siku mbili tu baada ya mtandao huo kufuta chapisho la Rais Muhammadu Buhari kwa madai ya kuvunja sheria zake na kuifungia akaunti yake kwa muda wa saa 12.

Chama cha Watoa Huduma za Mitandao Waliosajiliwa nchini humo (ALTON) kimesema kuwa wanachama wake wamepokea maelekezo rasmi kutoka serikalini kuwataka kufungia mtandao wa Twitter nchini Nigeria. Mtandao huo unaweza kupatikana kwa watumiaji wanaotumia Virtua Private Network (VPN).

Wizara ya Habari ilitangaza siku ya Ijumaa kuwa serikali imesitisha kwa muda usiojulikana huduma za mtandao wa Twitter kutokana na mtandao huo kujihusisha na shughuli zinazohatarisha uthabiti wa taifa hilo. Taarifa hiyo haijaeleza chapisho la Rais Buhari lililofutwa wala akaunti yake kufungiwa.

Twitter, yenye zaidi ya wateja milioni 40 nchini Nigeria, imejitetea kuwa imechukua hatua hiyo kutokana na chapisho la Buhari kukiuka kanuni zake, na kueleza kuwa hatua ya Nigeria kusitisha huduma zake ni ya kusikitisha. Imeongeza kuwa inachunguza na itatoa maelezo zaidi pale itakapopata taarifa kamili.

Hatua ya Serikali ya Nigeria imekosolewa na watumiaji na wanaharakati wengi, huku baadhi yao wakitishia kuichukulia serikali hatua za kisheria kwa kuzuia Uhuru wa Kutoa Maoni.

Chanzo: Al Jazeera
 
Viongozi wa Afrika wana shida sana yaani... Sasa huyu rais kafungiwa yeye kwa makosa yake mwenyewe ya kiuandishi halafu sasa eti an awaadhibu wanaigeria milioni 40 kwa ujinga wake. Hawa Twitter wana sheria zao, ambazo ziko wazi kabisa, hata Trump mwenyewe walimfungia ndiyo iwe huyo rais wa Naijeria?
 
Viongozi wa Afrika wana shida sana yaani... Sasa huyu rais kafungiwa yeye kwa makosa yake mwenyewe ya kiuandishi halafu sasa eti an awaadhibu wanaigeria milioni 40 kwa ujinga wake. Hawa Twitter wana sheria zao, ambazo ziko wazi kabisa, hata Trump mwenyewe walimfungia ndiyo iwe huyo rais wa Naijeria?
π™ΊπšŠπš–πšŠ πšƒπš πš’πšπšŽπš› πš πšŠπš—πšŠπšœπš‘πšŽπš›πš’πšŠ 𝚣𝚊𝚘 πš‹πšŠπšœπš’ 𝚊𝚝𝚊 π™½πš’πšπšŽπš›πš’πšŠ πš πšŠπš—πšŠπšœπš‘πšŽπš›πš’πšŠ 𝚣𝚊𝚘.!! πš„πš‘πšžπš›πšž 𝚠𝚊 πš”πšžπš“πš’πšŽπš•πšŽπš£πšŠ πš πšŠπš—πšŠπšžπš“πšžπšŠ 𝚠𝚊𝚘 𝚝𝚞 πšƒπš πš’πšπšŽπš› πš’πš•πšŠ πš πšŽπš—πšπš’πš—πšŽ πš‘πšŠπš πšŠπšžπš“πšžπš’? πš πšŠπš™πš’πšπš πšŽ πš‹πšŠπš— 𝚝𝚞 𝚊𝚘 πšπš πš’πšπšŽπš› πšžπš“πš’πš—πšπšŠ πšžπšπš’πšŽ πš‘πšžπš”πš˜.
 
Viongozi wa Afrika wana shida sana yaani... Sasa huyu rais kafungiwa yeye kwa makosa yake mwenyewe ya kiuandishi halafu sasa eti an awaadhibu wanaigeria milioni 40 kwa ujinga wake. Hawa Twitter wana sheria zao, ambazo ziko wazi kabisa, hata Trump mwenyewe walimfungia ndiyo iwe huyo rais wa Naijeria?
 
Viongozi wa Afrika wana shida sana yaani... Sasa huyu rais kafungiwa yeye kwa makosa yake mwenyewe ya kiuandishi halafu sasa eti an awaadhibu wanaigeria milioni 40 kwa ujinga wake. Hawa Twitter wana sheria zao, ambazo ziko wazi kabisa, hata Trump mwenyewe walimfungia ndiyo iwe huyo rais wa Naijeria?
Je wanachofanya twitter kina utofauti gani na alichofanya Buhari? Twitter wamejigeuza majaji wa kuamua nani yupo sahihi na nani sio. Hii hatua ni nzuri ingependeza kama utaifurahia sababu pengine itawakumbusha nini kinaweza kuwapata kwa kuwapangia watu nini cha kusema. Me youtube wamefuta sana comments zangu sasa si udikteta huo
 
π™ΊπšŠπš–πšŠ πšƒπš πš’πšπšŽπš› πš πšŠπš—πšŠπšœπš‘πšŽπš›πš’πšŠ 𝚣𝚊𝚘 πš‹πšŠπšœπš’ 𝚊𝚝𝚊 π™½πš’πšπšŽπš›πš’πšŠ πš πšŠπš—πšŠπšœπš‘πšŽπš›πš’πšŠ 𝚣𝚊𝚘.!! πš„πš‘πšžπš›πšž 𝚠𝚊 πš”πšžπš“πš’πšŽπš•πšŽπš£πšŠ πš πšŠπš—πšŠπšžπš“πšžπšŠ 𝚠𝚊𝚘 𝚝𝚞 πšƒπš πš’πšπšŽπš› πš’πš•πšŠ πš πšŽπš—πšπš’πš—πšŽ πš‘πšŠπš πšŠπšžπš“πšžπš’? πš πšŠπš™πš’πšπš πšŽ πš‹πšŠπš— 𝚝𝚞 𝚊𝚘 πšπš πš’πšπšŽπš› πšžπš“πš’πš—πšπšŠ πšžπšπš’πšŽ πš‘πšžπš”πš˜.
Wewe bila shaka ni mataga. Akili za ccm ni kama hizi hizi za kwako.
 
cace5133a4eefd8e.jpeg
 
Back
Top Bottom