nizakale
JF-Expert Member
- Oct 23, 2019
- 4,029
- 2,894
Mhh, inawezekana Simba ndio hawataki uonekane mubashara kwa kuogopa aibu.Mchezo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa kati ya Plateau United dhidi ya Simba ambao utapigwa baadae leo uwanja wa New Jos huko Nigeria, hautaonyeshwa mbashara
Imeelezwa kuwa maafisa wa Plateau United wamegoma mchezo huo kurushwa mbashara licha ya juhudi kufanywa na Ubalozi wa Tanzania nchini Nigeria kuomba Azam TV wapewe haki ya kuonyesha mchezo huo
Balozi wa Tanzania nchini Nigeria Dk Benson Bana amesema Plateau United wamegoma mchezo huo kurushwa mbashara hivyo amewataka Watanzania kuiombea Simba iweze kufanya vizuri kwenye mchezo huo
Uongozi wa klabu ya Simba umethibitisha kuwa mchezo huo hautakuwa mbashara kwenye kituo chochote cha televisheni
"Kwa masikitiko tunawajulisha Wanasimba na Watanzania wote kwamba mchezo wetu wa kesho dhidi ya Plateau United hautaonyeshwa mbashara baada ya wenyeji wetu Plateau kuzuia matangazo ya moja kwa moja ya mchezo huo"
Hakuna chombo chochoto kitakachoonyesha mkuu...