Melki the Storyteller
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 5,700
- 9,778
Napitia kipindi kizito sana ndugu zanguni. Miaka mitano iliyopita nilikutana na binti ambaye niliingia nae kwenye mahusiano ya kimapenzi. Miezi miwili baadae binti alidai kuwa anahitaji kumbukumbu yangu. Hivyo nimpatie japo ujauzito wangu
Kutokana na hali yangu ya kiuchumi niliyokuwa nayo nilimkatalia, lakini aliendelea kulazimisha kwa ahadi ya eti malezi ya mtoto atashughulika nayo yeye mwenyewe. Basi bhana, akina Awa wana nguvu sana, nikajikuta nauza mechi mara kwa mara
Mwisho wa siku binti akapata kibendi. Ujauzito ulipofikia umri wa miezi minne ndipo kuja kugundua kuwa binti kaolewa, tena ni kwa ndoa halali ya kitanzania. Nilimlahum sana na kumkaripia niwezavyo. Binti akafunguka na kusema kuwa mumewe ana tatizo, hawezi kutungisha ujauzito, ingawa ukweni walidhani kuwa yeye ndiye mwenye matatizo, hivyo akaamua kuja kwangu ili a-test kama kweli yeye ndiye mwenye shida au la!
Alidai hawezi kuachana na mumewe kwa kuwa anampenda, akaongezea kwa kusema kuwa akiwa kwa mumewe anapata mahitaji yote anayoyataka. Tukakubaliana iwe siri. Baada ya kujifungua, akawa ananiletea mwanangu kwa siri kisha anamrejesha kwa baba yake wa mchongo. Baada ya miaka mitatu, tukaamua kupanda mbegu nyingine, binti akajifungua. Kwa sasa ninao wawili kwa huyo mwanamke.
Juzi kati tumetoka kuzozana, huyu mwanamke akanikaripia na kukana kuwa hao watoto hawanihusu na si damu yangu. Kwa sasa wana mpango wa kuhama na kwenda mbali na mimi. Naogopa! Nahisi nitawapoteza wanangu. Kwa sasa huyu shetani keshabadili namba ya simu. Msaada niliobaki nao ni wa kupajua kwake tu.
Nifanye nini kuokoa damu yangu? Au niende mahakamani. Naanza kwa kufuata utaratibu upi?
Msaada
Kutokana na hali yangu ya kiuchumi niliyokuwa nayo nilimkatalia, lakini aliendelea kulazimisha kwa ahadi ya eti malezi ya mtoto atashughulika nayo yeye mwenyewe. Basi bhana, akina Awa wana nguvu sana, nikajikuta nauza mechi mara kwa mara
Mwisho wa siku binti akapata kibendi. Ujauzito ulipofikia umri wa miezi minne ndipo kuja kugundua kuwa binti kaolewa, tena ni kwa ndoa halali ya kitanzania. Nilimlahum sana na kumkaripia niwezavyo. Binti akafunguka na kusema kuwa mumewe ana tatizo, hawezi kutungisha ujauzito, ingawa ukweni walidhani kuwa yeye ndiye mwenye matatizo, hivyo akaamua kuja kwangu ili a-test kama kweli yeye ndiye mwenye shida au la!
Alidai hawezi kuachana na mumewe kwa kuwa anampenda, akaongezea kwa kusema kuwa akiwa kwa mumewe anapata mahitaji yote anayoyataka. Tukakubaliana iwe siri. Baada ya kujifungua, akawa ananiletea mwanangu kwa siri kisha anamrejesha kwa baba yake wa mchongo. Baada ya miaka mitatu, tukaamua kupanda mbegu nyingine, binti akajifungua. Kwa sasa ninao wawili kwa huyo mwanamke.
Juzi kati tumetoka kuzozana, huyu mwanamke akanikaripia na kukana kuwa hao watoto hawanihusu na si damu yangu. Kwa sasa wana mpango wa kuhama na kwenda mbali na mimi. Naogopa! Nahisi nitawapoteza wanangu. Kwa sasa huyu shetani keshabadili namba ya simu. Msaada niliobaki nao ni wa kupajua kwake tu.
Nifanye nini kuokoa damu yangu? Au niende mahakamani. Naanza kwa kufuata utaratibu upi?
Msaada