nifanyeje ili aniamini kwa kiwango cha juu?

mutisya mutambu

JF-Expert Member
Nov 21, 2010
208
82
wana jamvi naomba msaada wenu niweze kufanikiwa katika hili linalonisumbua akilini na nadhani wengi pia ni gumu kwao,nifanyeje lipi basi nijenge uaminifu wa hali ya juu sana kwa mpenzi wangu,yani aniamini kama vile ninavyomwamini.kuna siri gani hapa ya namna ya kumfanya mpenzi wako akuamini kwa kiwango cha juu kinachoridhisha.kuna maeneo kadhaa ya muhimu sana
1.kwenye mapato na pesa
2.aamini kwamba mimi ni wake pekee,sina mwingine
waweza ongeza vingine ujuavyo kisha ukatoa ushauri.
 
Usimfiche chochote. Usimkataze kujibu simu zako ua kutumia simu yako. Hata email unaweza kumpa password. Usiwe na urafiki na watu wa jinsia tofauti.

Yaani kwa kifupi, usifanye chochote kitakachomfanya asikuamini na uwe mwaminifu kikwelikweli. Ni hivyo tu.
 
usimfiche chochote. Usimkataze kujibu simu zako ua kutumia simu yako. Hata email unaweza kumpa password. Usiwe na urafiki na watu wa jinsia tofauti.

Yaani kwa kifupi, usifanye chochote kitakachomfanya asikuamini na uwe mwaminifu kikwelikweli. Ni hivyo tu.
usifanye hayo anayokushauei ngabu yaweza kuharibu zaidi iwe muwazi kidooogo!
 
usifanye hayo anayokushauei ngabu yaweza kuharibu zaidi iwe muwazi kidooogo!

Yataharibu tu endapo utakuwa unafanya yale ambayo hutakiwi kufanya. Na kama hufanyi lolote baya basi hutakuwa na sababu ya kumficha mwenza wako chochote.
 
Mi nadhani ni wivu tu wa kimapenzi.
Na mtu akikuonea wivu jua kuwa anakupenda huyo.
 
eeh wewe ni Nyani Ngabu kweli..duh yaani usimfiche chochote kabisa..apokee simu zote hata za kikazi..lol.
Usimfiche chochote. Usimkataze kujibu simu zako ua kutumia simu yako. Hata email unaweza kumpa password. Usiwe na urafiki na watu wa jinsia tofauti.

Yaani kwa kifupi, usifanye chochote kitakachomfanya asikuamini na uwe mwaminifu kikwelikweli. Ni hivyo tu.
 
usisemee mioyo ya watu wengine kuna watu hata uwaonyeshe kila kitu bado mashaka na wewe hayaishi anatumia historia lake kupeleka yaliyopo sasa unaweza ukaweka mpaka screen ukiwa unatembea akuone ukijikwaa tu swali mbona hukupita njia nyingine mpaka umejikwaa live your life utakuwa na furaha na amani siku zote
 
eeh wewe ni Nyani Ngabu kweli..duh yaani usimfiche chochote kabisa..apokee simu zote hata za kikazi..lol.

Kwa nini asipokee? Halafu nyinyi ni kazi gani hizo ambazo mnapigiwa simu kwenye simu ya matumizi binafsi? Kwani huko makazini kwenu hamna simu?

Na sababu hasa ya kumficha hata hicho kidogo ni ipi hasa? Maana uchi wako haumfichi....
 
Nyani Ngabu;Usimfiche chochote. Usimkataze kujibu simu zako ua kutumia simu yako. Hata email unaweza kumpa password. Usiwe na urafiki na watu wa jinsia tofauti.

Yaani kwa kifupi, usifanye chochote kitakachomfanya asikuamini na uwe mwaminifu kikwelikweli. Ni hivyo tu.[/QUOTE]

Na hapa wengi ndo wanaishia kulalama kila siku kwenye ndoa zao. Uaminifu unajengwa na jinsi wanandoa mnavyowasiliana. Kama kila mtu anakuwa na chake ndo hapo mwanzo wa tatizo. Watu wanaishia kusema simu zao ni zakwao haiitaji ku-share au kuangalia simu ya mwenzi wako. Kama mtu ni mkeo/mumeo na Unampenda kwa nini mfichane? Kama mmoja akingundua kuna kitu hukumweleza na ameking'amua ndo hapo trust level inaanza kushuka.

Nimesoma kwenye post moja hapa mwanamama analalama mumewe anafunga kabati lake anashangaa kwa nini? Nikajiuliza mume anakuwa na kabati na ufunguo wake ambao mke hatakiwi kuona kilichomo ndani yake, sasa huyo ni mke unayempenda au ni mke mtu anakuwa anaishi naye tu miaka inaenda?.

Trust ni nzuri sana kwa wanandoa/mahusiano. Na mkiwa na trust miongoni mwenu maisha ni raha sana maana unajifikilia zaidi ya mara tatu Kumtendea kinyume mwenzi wako. Hivyo hata mambo ya kutoka nje yanapungua kwa kiasi kikubwa. Email zangu anasoma maana ana password, Simu yangu ni ya mke wangu na yake ni yangu, Hata kama ni simu ya biashara/kazini imepigwa kuna kosa gani mke wangu kuijibu? Kazi ipi ambayo mke wangu hatakiwi kuijuwa?

Watu wataishia kulalama kila mara kwenye mahusiano kwa sababu ya neno moja tu ''Trust'' ambalo ni muhimili wa Ndoa yenye furaha na Amani.
 
Mimi sielewi ni kwa nini mtu unayemfunulia uchi wako umfiche au umkataze kuangalia baadhi ya vitu. Sioni kabisa mantiki yake!!!
 
ndugu zangu naona tumehama kabisa kutoka kwenye mstari tuliocholewa na sasa tunachora wa kwetu.kikubwa ni kutaka kujua ni namna gani nifanye mpenzi wangu aniamini tena kwa kiasi cha juu,uaminifu wa ukweli na si ule wa kinafiki,wa leo afu kesho haupo.hapa basi ningependa tuzifahamu baadhi ya njia na namna hizo ambazo zaweza saidia kumfanya mtu yoyote akuamini tena sana kwa kiwango cha juu,nasema mtu yoyote si lazima awe mpenzi wako kwani uaminifu ni muhimu kwa kila mtu na si katika mapenzi tu
1.onesha kumuelewa mtu huyo,understand the individual
2.shiriki katika mambo yake hasa yale yaonekanayo kuwa madogomadogo
na si muhimu sana,attending to the little things
3.tunza ahadi,keep commitments
4.itikia matarajio yake aliyonayo kwako,usisubiri akweleze anatarajia
nini,ndipo ufanye,clarifying expectations
5.onesha heshimu,mheshimu kwa hali ya juu,mpe
thamani yake aliyonayo hata zaidi ya
hapo,showing personal intergrity
6.kuomba msamaha pindi unapokosea au unaposhindwa kutimiza
ahadi uliyokuwa umeweka,kwa jambo lolote lile dogo hata kubwa
apologizing sincerely.

nadhani mpaka hapa tupo pamoja,nina hakika asilimia zote uta
kapo tumia na kutimiza njia hizi mambo yatakuwa sadi sana
utayafurahia maisha wewe na mpenzi
wako pamoja na wote wakuzungukao.

 
Uwe mkweli na uwe makini kwa kila unalomwambia, ukiulizwa upo wapi taja exactly sehem uliyopo, sio upo salender unasema palm beach au upo magomeni unasema mwenge labda anakuuliza hivo kwa vile amekuona na yeye yupo maeneo hayo utaposema uwongo basi hapo hautoeleweka ata ukisema ukweli wa jambo lolote
 
i guess u have to strip off every thing......
if that is not good enough then your partner has a problem..
 
wana jamvi naomba msaada wenu niweze kufanikiwa katika hili linalonisumbua akilini na nadhani wengi pia ni gumu kwao,nifanyeje lipi basi nijenge uaminifu wa hali ya juu sana kwa mpenzi wangu,yani aniamini kama vile ninavyomwamini.kuna siri gani hapa ya namna ya kumfanya mpenzi wako akuamini kwa kiwango cha juu kinachoridhisha.kuna maeneo kadhaa ya muhimu sana
1.kwenye mapato na pesa
2.aamini kwamba mimi ni wake pekee,sina mwingine
waweza ongeza vingine ujuavyo kisha ukatoa ushauri.
Usihangaike kutafuta kuaminiwa, bali kuwa mwaminifu......!
 
Nyani Ngabu;Usimfiche chochote. Usimkataze kujibu simu zako ua kutumia simu yako. Hata email unaweza kumpa password. Usiwe na urafiki na watu wa jinsia tofauti.

Yaani kwa kifupi, usifanye chochote kitakachomfanya asikuamini na uwe mwaminifu kikwelikweli. Ni hivyo tu.


Na hapa wengi ndo wanaishia kulalama kila siku kwenye ndoa zao. Uaminifu unajengwa na jinsi wanandoa mnavyowasiliana. Kama kila mtu anakuwa na chake ndo hapo mwanzo wa tatizo. Watu wanaishia kusema simu zao ni zakwao haiitaji ku-share au kuangalia simu ya mwenzi wako. Kama mtu ni mkeo/mumeo na Unampenda kwa nini mfichane? Kama mmoja akingundua kuna kitu hukumweleza na ameking'amua ndo hapo trust level inaanza kushuka.

Nimesoma kwenye post moja hapa mwanamama analalama mumewe anafunga kabati lake anashangaa kwa nini? Nikajiuliza mume anakuwa na kabati na ufunguo wake ambao mke hatakiwi kuona kilichomo ndani yake, sasa huyo ni mke unayempenda au ni mke mtu anakuwa anaishi naye tu miaka inaenda?.

Trust ni nzuri sana kwa wanandoa/mahusiano. Na mkiwa na trust miongoni mwenu maisha ni raha sana maana unajifikilia zaidi ya mara tatu Kumtendea kinyume mwenzi wako. Hivyo hata mambo ya kutoka nje yanapungua kwa kiasi kikubwa. Email zangu anasoma maana ana password, Simu yangu ni ya mke wangu na yake ni yangu, Hata kama ni simu ya biashara/kazini imepigwa kuna kosa gani mke wangu kuijibu? Kazi ipi ambayo mke wangu hatakiwi kuijuwa?

Watu wataishia kulalama kila mara kwenye mahusiano kwa sababu ya neno moja tu ''Trust'' ambalo ni muhimili wa Ndoa yenye furaha na Amani.[/QUOTE]
upo juu vibaya,yani ulosema ni kweli kabisa mtu ana madudu yake anafanya saa ngapi attakuwa huru na vitu vyake lazima afiche fiche tu na ndo yanayoleta ugomvi halafu kitu kingine mkishaaminiana vya kutosha wala hutaona mtu anakufatafata nyuma hata ukimuaga unaenda mahali gani na ukarudi kwa muda gani hawezi kuwa na wasiwasi na ww na hayo ndo mapenzi ya kweli jamani NGO UMESEMA UKWELI MTUPU
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom