mama D
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 19,760
- 35,205
Mimi ni kijana mwenzio. Nimeoa ila kwa sasa ndoa yangu aipo tena, yaani sipo tena na mke wangu.
Sasa tatizo lilikuja vipi
Mimi nili safiri kwenda zangu USA ndugu zangu wali nifanyia visit invitation nikamuacha mke wangu Dar es Salaam.
Sasa nilivyokuwa kule nikawa naongea naye kama kawaida tu Ila kulifikia kipindi akawa ananijibu mambo ya ovyo ovyo. Nikitaka kumfokea mara ananiambia amenichoka sujui nini.
Kiburi kilipanda mtoto wa kike akafikia hatua ya kuniambia nimekukataa ili nikuonyeshe kama Marekani sio kitu mbele yangu. Yaani maneno ya kujiamini sana.
Mpaka akafikia hatua ya kuniacha ila mke wangu bado nampenda saana. Ninajaribu kumwambia nini tatizo ananiambia hataki tu na siku hizi, she doesn’t call me tena mume wangu ni Jina langu tu.
Sasa jamani nisaidieni nifanye nini ili mke wangu arudi maana nimejaribu kula wanawake wengine lakini naona mmmm ni bure kweli yaani ameniganda kweli kweli.
Safari uliipanga na kukubaliana na mkeo au ulikubaliana na ndugu zako na ikatosha?