Mtaji wa Milioni 5-10 (TZS): Biashara gani unaweza kufanya?

Mbu

JF-Expert Member
Jan 11, 2007
12,753
7,839
Wajameni eeh,

Nimebahatika "kupata" mahala ka mtaji. Ni kiasi cha Shs. milioni kumi tu, (10,000,000/=) za Kitanzania.

Nipeni mapendekezo nizi invest wapi, kivipi na matarajio ya faida (i.e biashara gani inalipa (plus location), kwa muda gani, na SWOT analysis zake).

=======


Mimi ni mfugaji, nitakushauri kufuga ngombe kwa mchakato ufuatao:

Ujenzi wa banda = Ths 500,000/=
Manunuzi ya Ngombe 5 x Tsh 900,000 = Tsh 4,500,000/=
(Ngombe utawanunua wakiwa na mimba ya miezi 6)
Kuwahudumia ng'ombe kwa miezi mitatu kabla ya production = Tsh 1,500,000/=
(inahusisha mshahara kwa wafanyakazi wawil + chakula + madawa)

Jumla = Tsh 6,500,000/=

Baada ya Miezi 3;

UZALISHAJI:

Ngombe hawa watakuwa wakitoa maziwa si pungufu ya lita 5 kwa asubuhi na jioni kwa kila ng'ombe. Hivyo uzalishaji kwa siku utakuwa lita 10 kwa siku kwa ng'ombe.

MAPATO

Lita 10 x Ng'ombe 5 = lita 50 kwa siku x Tsh 1000 (bei ninayouza mimi hapa) = Tsh 50,000 kwa siku
Mapato kwa mwezi = Tsh 50,000 x 30 = 1,500,000/=

Gharama za uendeshaji kwa mwezi = Tsh 600,000/=

Faida = Tsh 900,000/= kwa mwezi

BAADA YA MIAKA 5:

Kumbuka ng'ombe huzaa kila mwaka hivyo basi baada ya miaka mitano utakuwa na ng'ombe wasiopungua 25. Kipato chako kwa mwezi unaweza kufikia si pungufu Tsh 18,000,000 endapo utakuwa na ngombe jike 20 kati ya hao 25.

kama una umri kati ya miaka 25 mpaka 35 nakushauri wekeza ktk misitu ya miti ya mbao(exortic) na nguzo za umeme,biashara ya nguzo za umeme kwa sasa inalipa ile mbaya,investment ktk misitu ya nguzo unafanya bila taabu hata kama uko Ulaya. Only risk takers can do it. Tz ardhi ni cheap sana.

Pili kama ungekuwa Dar ningekwambia jaribu Kitimoto,mzee hii kitu inalipa bila mgogoro,si umesikia tishio la mafua limepungua.Dar kinaliwa ile mbaya.Ng`ombe safi pia. Tatizo la kuku wa kienyeji wafugaji wadogo wadogo wengi mno si rahisi kupredict soko la uhakika.Tatu jaribu kufuga samaki,tilapia au nile perch,wanazaliana kwa kasi na soko lake ni kubwa sana kwa sasa.

Jenga Choo ya kulipia eneo la Kariakoo. Utakuwa na uhakika wa kurejesha gharama zako ndani ya muda mfupi kama ifuatavyo:

Wateja - Akina mama (200 * 100/= * 30days) = 600,000/=
- Akina baba (150 * 100/= * 30days) = 450,000/=
- Watoto/vijana/wanafunzi (200 * 100/= * 30days) = 600,000/=
JUMLA KWA MWEZI 1,650,000/=

Kwa mwaka (19,800,000), kwa miaka kumi (198,800,000/=).

Yaani baada ya miaka kumi utakuwa millionea mkubwa sana, na usisahau kurudi hapa JF na kutushukuru.

NB: Kumbuka, uzuri mmoja kwa biashara hii, haina suala la mvua wala kiangazi. Kila siku biashara inaenda.


Kwa ufupi nimekuwa ktk sector hii ya miti kwa muda mrefu sana. Naomba mchague wenyewe eneo mnalotaka nishushe data kati zifuatazo;

1; Ardhi ya bei poa iko wapi? na taabu za huko
2; mbegu zinapatikana wapi? na namna ya kuotesha?
3; Aina ya mti(mbegu,growth rate,soko,na sehemu ya kupanda ktk Tz)
4; Msimu mzuri na maandalizi yake.
5; overhead cost baada ya kupanda.
6; Field management.

Leo niwape item ya tatu tu,mimi nimeajiriwa,najaribu kutumia muda wa mwajiri kwa uangalifu.
Kuna miti mingi ila kwa sisi mizuri ni hii; mitiki(10, nje),milingoti boriti(8),milingoti nguzo (10), milingoti mbao (15),mikrismas(cyprus mbao) (25),
pines (12),ktk mabano ni miaka toka kupanda mpaka kuvuna. Soko la mitiki liko nje ya nchi,locally hakuna commercial market mpaka Kilombero wakijenga kiwanda mwakani. Mbegu zinapatikana kwa wakala wa serikali Morogoro,Iringa,Arusha,Tanga etc. Mbegu za mitiki ni ngarambe kuotesha, kilo moja ni Tsh 6000/ na ukifuata utaalam unapata miche 1000 hivi,lakini wajanja wanafanya kienyeji na wanapata zaidi au wanatumia suckers fulani hivi. Bei ya mche kwa sasa ni Tsh 500/ ya chini na 2000/ ya juu pale dar.

Pine/cyprus kilo moja ni Tsh 18,500/ na unapata miche 30,000 mpaka 35,000 inatosha eka hamsini ya miti ya mbao. Mlingoti kilo moja ni Tsh 22,500/ na unapata miche 120,000. Unapanda boriti eka 100 na unapanda miti ya mbao eka 200.

Utamu uko ktk boriti. Eka moja ni boriti 1200,bei ya boriti moja kwa leo hii ni Tsh 15,000/shambani.kwa hiyo eka moja iliyogharimu Tsh 70,000/ kununua ardhi mpaka kupanda itakupa 1200 x 15,000/=( ) toa gharama za fire break mara moja kwa mwaka. Hakuna kupalilia wala kumwagilia.

Mitiki peke yake inakubali pwani,mingine yote ni ktk nchi za baridi. Nimetoa kwa ufupi sana, ila tutaendelea kuelezana kidogo kidogo, item nyingine kesho.

Kwa Tanzania Mil. 10 unaweza kupata faida ya mwaka kama ifuatavyo:

1. Ukanunua used Corola na kuifanya taxi. Mradi huu unakuhakikishia a minimum net revenue ya Shs 2.92 mil per year (8000*365).
2. Hisa za TCC: 10mil. * 10% = 1 mil per year + annual appreciatiatin ya ?%
3. Gunia za mahindi June na kuuza December: 10 mil * 50% = 5mil
4. Ziweke deposit bank upate interest: 10 mil * 7% = laki 7
5. Anzisha ka-saccos kasiko rasmi (zikopeshe at interest): 10 mil * 17% = 1.7 mil
6. Nunua shamba, chimba kisima ufanye kilimo cha umwagiliaji: 10 mil * 2mil
7. NAENDELEA KUBUNGABONGO. WILL GET BACK TO YOU SHORTLY

Mradi mwingine mzuri wa bei nafuu ni mradi wa kukamua alizeti. Mwaka jana nilipata bahati ya kutembelea Singida kwa ziara ya kitume. Nikapata muda nikaenda mitaa ya sido. Nilitembelea viwanda vidogo vya kukamulia alizeti. Nikatafiti gharama za mradi wote ule. Kwa mujibu wa Sido,mtambo wenyewe unafikia Tsh 6,000,000/ kwa mwaka jana. Ila mitambo ya mitaani inaweza kuwa chini ya hapo. Gharama za jengo zinategemea sehemu.Ukiweza kufunga kimtambo hicho,mikopo ya upanuzi toka Sido ni mingi bila urasimu.

Wale jamaa wanatengeneza hela sio mchezo. Nimegundua pia kuwa watu wanarudi ktk matumizi ya mafuta ya nafaka sana na ukulima wa alizeti/ufuta unaongezeka sana.

Mr MBU think on this also

Uzuri wa IR ni huu,ardhi ipo,mvua zinanyesha sana,barabara zipo,wahehe wanaogopa kuiba cha mtu,wahehe hawabagui mgeni. Wewe fanya kilichokupeleka kwa utaratibu basi,halafu unaambiwa karibu tena. Wasichotaka, usiwadharau tu basi. Kazi wanafanya kwa kiwango cha kuridhisha ila baadhi ya vijiji tutapeli tumeingia.

Milingoti hasa Saligna na grandis,ina kuwa haraka na ni multipurpose yaani waweza kuuza kama nguzo za umeme,au boriti za kawaida au ukachana mbao.Wewe ukiwa na milioni moja inatosha kununua eka kumi na kupanda miche 6000 ya milingoti/pines ya mbao,kisha unaondoka kurudi zako mjini. Unakwenda huko june kuweka fireline na kurudi tena mjini. Baada ya miaka mitatu unaprun miti yako. Kwa hiyo mwendo ni huo.

Mimi na vijana wenzangu tumeunganisha nguvu na kununua eneo kubwa,tunaotesha wenyewe miche ya pines/mlingoti na kupanda ktk plots zetu. Mwaka huu tumepanda miti laki tatu kwa pamoja tuko sita tu. Ila mpaka sasa vijana waliopanda miti eneo lile tuko 24 hivi. Msimu ujao tutakuwa kama 30 jumla.

Wenzetu walikwama msimu huu kwa sababu mbalimbali. Tuna jirani mmoja kutoka Kenya yeye peke yake amepanda milingoti milioni nne. Yeye ardhi kapewa na serikali yetu tukufu. Usijali ndo hali halisi. Mmalawi mmoja kajimegea eka 1000 na amepanda miti.


Tafuta eneo kama ekari mbili mpaka nne chimba kisima kama ulivyoelekezwa na ikiwezekana tenganisha matumizi ya maji binafsi na maji ya biashara. uza maji kwa ajili ya kutafuta gharama za kuendeleza na kukuza mtaji zaidi, lakini ni vizuri ukafuga kuku wa mayai kama 700 ambao nauhakika hutakosa tray 25 kwa siku kwa muda wa mwaka mmoja na nusu, tumia fuga ngombe wa maziwa wawili tu watunze vizuri wakupatie lita 20-30 kwa siku, hata kama mazima haya lipi unahitaji mbolea kwa ajiri ya mbogamboga na kupata bio gas pamoja na matunda achilia mbali kwa sababu maji unayo unaweza kuwa na bwawa dogo la samaki ukaanza kuvuna kila miezi minne mara baada ya kupanga na haya chini ndio mapato kwa miezi sita kwa kila mwezi.

maziwa1,080,000.00
mbogamboga600,000.00
mayai4,500,000.00
maji450,000.00
samaki500,000.00
passion400,000.00
jumla7,530,000.00

Natengeneza mchanganuo ukikamilika nitwawasilisha kwenu, vinginevyo humu ndani kuna vibiashara na mawazo ya watu wengi nayaheshimu sana na yamenisaidia sana.

Kama muoga unaweza ukanunua ardhi kiasi wakati unajipanga.

Wazo linguine la nyongeza mkuu ni hili, uko nje ulipo, angalia yafuatayo,

1.viwanda vya kutengeneza vyakula vya kuku-kama wanaweza kununua dagaa kutoka Tanzania.
2.Viwanda vyakutengeneza vyakula vya mifugo, na dawa za viatu kama kiw-ulizia kama wanaweza kununua mashudu ya alizeti kutoka tanzania
3. Viwanda vya kutengeneza viatu, mikoba, mikanda n.k- ulizia kama unaweza kuwa uzia ngozi za wanyama kama ngombe.
4. Viwanda vya kutengeneza taa za umeme, balb- ulizia kama wanaweza kununua kwato na pembe za ngombe.

Ukisha pata soko lake la uhakika, rudi jamvini kuomba watu wa kushirikiana nao ili kuongeza mtaji.bidhaa zote nilizo eleza kwa apa Tanzania zinapatikana sana. hivyo ukiomba watu wa kushirikiana nao uenda ukawapata na mimi naweza kuwa mmoja wapo kwa kuongeza zingine 10milion. na hivyo ukapeleka hata kwa kuanzia angalau contena moja.

ndo hayo tu mkuu. ubarikiwe

km sio mzoefu itakukata tu
1om sio pesa
Dodoma pameshakuwa pagumu
kwani biashara ni za Msimu
  • Mazao ni Msimu kuanzia Julai hadi Novemba
  • Kulima nako ni Msimu kuanzia Novemba hadi April
  • Kuuza pembejea unatakiwa uleta majembe na mbegu uuze kuanzia Oktoba hadi Januari na mvua inyeshe!
  • Guest sasa hivi ni kichaa 10m haiwezi nunua pagale ukajenga na kuweka maji umeme na vitanda
  • Biashara ya maji na juice za azam ni kiamgazi km Oktoba hadi januari wakati wa joto kali
Mimi nipo Mjini kati na nina nyumba napangisha kwa ajili ya biashara kodi ni 300,000 hivyo kwa mwaka lazima utangulize 3.6m je shelves na mali zitatoka uweze kunilipa kodi ya 2016 nakushauri tuliza munkari na uanze na mtaji mdogo zaidi kwani wamekuuliza hela yote umeipata wapi ghafla, ni heri uwe na mali ya 10m kuliko cash (km ni kiinua mgongo watu wanamalizahata 70m kwa mwezi)
karibu Dodoma


Mdau rasomaka;

Angalia mazingira unayoish, km inawezekana anzisha biashara ya bodaboda za mkataba (miez 10 baada ya hapo inakuwa ya kwake huyo dereva, matengenezo n jukumu la dereva)

Kwa 10 millions unanunua pkpk 4 (pkpk moja inauzwa around 1.8 mil san lg inapendwa zaid, ingawa zpo nyngne za bei pungufu)

Na kila pkpk kwa siku inaingza sh. elfu 10, baada miez 6 kila pkpk imeshajrudshia hela yake ya manunuz ile miez mi4 ilyobak faida. (Mwisho wa mkataba kila pkpk inazaa nyingine)

Biashara n kupata faida, kutanuka na kuzaa biashara nyingne.

Ukikusanya hela ya pkpk 4 kwa miez 3 (1,200,000×3=3600,000/=) ni hela ambayo unaweza kununua pkpk ya matairi matatu (bajaji) ya mizigo/maji ambayo itakuletea kipande kwa siku sh. elfu 15 ( kwa mwez lak 4 ukiondoa matengenezo)

Au kuamua kununua pkpk nyngne tena na kupanua wigo mkubwa wa bzness ambapo mpk pkpk za kwanza znaisha mkataba wake, ztakuwa zmeshazalisha nyngne nyingi.

Pia kwa hela unayokusanya unaweza kubuni biashara nyngne kutokana na eneo unaloish.

Changamoto:
Kila biashara haikosi changamoto, kwa pkpk changamoto kubwa ni kuibiwa/kutoroka na pkpk.

Mkataba uwe wa maandishi kwa m/kt wa mtaa ikiwezeka hata polisi mnaandkshiana ili kuwe na usalama.

Bodaboda ya mkataba n nzur kwa wote, tajiri na dereva, dereva anafaidika kwa kuwa baada ya kumalza mkataba anaimiliki inakuwa yake hivyo atakuwa makini na ataitunza. Matengenezo n jukumu lake.

Bodaboda za kipande kwa kila siku n majanga sana, dereva akishaona imechoka anaiacha na kutafuta nyingne mpya.

Ni hayo mawazo yangu nawasilisha.
 
Je, unataka investment ya muda mfupi au mrefu, specify,pili biashara hiyo utasimamia mwenyewe au unataka uweke mtu wa kuisimamia? Je, unataka biashara hiyo ndo uitegemee kwa maisha ya kila siku? Uko tayari kwenda kinyume cha imani yako(kama una imani/dini)?
 
Kanunue hisa za crdb ambazo zinauzwa at shs 150 per share. 10 m itakupatia shares 66,666. Hii maana yake nini. Kama ungepeleka DECI labda ungevuna 20m baada ya miezi 4? Sijui formula yao.

Lakini ukinunua shares hizi crdb zikipelekwa kwenye soko la hisa unaweza ukaziuza zote halafu ukavuna zaidi ya asimia 100. Na hii ni baada sana sana ya miezi miwili.

Kwa hiyo ukipata 20m zako iko mbaya gani/ U can decide kuziweka kwenye Fixed deposit ya hao crdb halafu ukaitumia hiyo kuombea mkopo. But this depends very much if u have a steady monthly income.

Huo ni ushauri wangu wa bure
 
Mkuu Mbu,

Njia nyingine pia ya kuharakisha mjadala ingekuwa kutuambia product idea zako halafu ukapata maoni kuhusu soko likoje kwa kila product idea.

Otherwise kama alivyosema WoS what's your core strength? Maana sio siri biashara ni zaidi ya mke, ni zaidi ya familia. You'll find yourself spending more time on your business especially in the beginning kuliko muda utakaokuwa unaspend na mamaa/papaa na watoto.

Off head kuna hii kitu ya online dating. You can throw a twist on the game by requiring your members to test for HIV, and charge men for ladies contacts.

Kuna wagoni wengi tu mfano maofisini ambao ni madomo zege lakini kila mwezi wanapenda kubadili mboga. Hao watakuwa wateja wako wakuu.

Plus internet population ya Tz ita-explode by Aug. this year, so you can start building now.
 
Last edited by a moderator:
Simoni

Kwa matangazo zaidi inabidi upate ruksa ya wenye jamvi akina Invisible..lol

Nways, haya mambo ya stock market wadau wanasema sometimes huwa yanakuwa pata potea. Kwa jinsi ulivyoweka maelezo yako, it is like unauhakika kuwa bei za hisa zitapanda huko mbeleni which is a fallacy.

Stock market are stochastic in nature na kuna factor nyingi mno zinzaochangia bei kushuka au kupanda. Some of the factors are internal and can be internally controlled, some are external and never be controlled.

Ni vyema mhusika asichukulia maneno yako in totality.
 
Last edited by a moderator:
Kanunue hisa za crdb ambazo zinauzwa at shs 150 per share. 10 m itakupatia shares 66,666.

Be careful on this maana its not automatic -kununua shares na kuziuza kwenye secondary market upate pesa ya chap chap siyo rahisi sana kama ilivyokuwa kwenye IPO.

Mbu angeongea au kutafuta ushauri kutoka kwa wataalam..kama uko dar mwone kwa mfano George Fumbuka wa Core Securities akushauri on this... au mtu mwingine gwiji kwenye eneo hili.
 
je unataka investment ya muda mfupi au mrefu, specify,pili biashara hiyo utasimamia mwenyewe au unataka uweke mtu wa kuisimamia? Je unataka biashara hiyo ndo uitegemee kwa maisha ya kila siku? Uko tayari kwenda kinyume cha imani yako(kama una imani/dini) ?

Nafikiri Malila ameuliza maswali muhimu sana.

Kwa kuongezea tu, je unataka kuinvest kwenye biashara utayojihusisha moja kwa moja? Au ungependa kuinvest kwenye biashara ya mtu mwingine na wewe ukaplay kama investor na kusubiri returns?

Jinsi shamra shamra za ujasiliamali zinavyoendelea sasa bongo, kuna watu kibao wanambinu za kibiashara lakini hawana mtaji. Kwa hiyo, watu aina hii unaweza kuwatafuta na kuwaruhusu wa-pitch ideas zao kwako ili utathmini kama zinafaa kutumbukiza mtaji wako.

Au kama ungependelea kuanzisha biashara yako mwenyewe, then ingekuwa vizuri ukae kitako na kupitia kwa uangalifu aina ya biashara zote ambazo zinaweza kuendesheka bongo. Tatizo la hili ni kuwa Tshs. 10m sidhani kama inatosha kuanzisha biashara yoyote bongo ambayo revenue yake inaweza kukamatika ( as in you can feel it).

All in all, kama unaishi nje ya nchi, then cha kwanza kabisa utahitaji kufunga safari na kwenda bongo. Ukiwa nyumbani, tumia muda wako mwingi kukutana na watu mbalimbali. Hii itakupa nafasi ya kudadisi mbinu nyingi za kibiashara zinazoendelea nchini, pamoja na ku-networking.

Goodluck bro.
 
Mbu,

Mbu! naomba uwatake radhi wanaJF wote waliokwisha kukushauri namna ya kuwekeza pesa ulizosema umekwapua sehemu. Kukwapua ni ufisadi tunaoupigia kelele hapa JF mpaka tunakosa muda wa kulala vizuri. Mi nitakushauri ukikanusha kuwa hujakwapua na iwe kweli hujakwapua mahala.

cheers
 
Mie naona Mbu uwekeze kwenye mfumo wa maji safi kule bongo, nenda sehemu ambazo hawana maji ya bomba na ukachimbe visima vya kutumia mota ya umeme ili wapate maji safi badala ya kuchota maji kwenye madimbwi.

Hiyo pesa unaweza kuchimba visima 5, hapo utasaidia wananchi wenzako. Unaweza kurudisha pesa yako, iwapo utafanya kila ndoo ya maji ni shs 100.
 
je unataka investment ya muda mfupi au mrefu, specify,pili biashara hiyo utasimamia mwenyewe au unataka uweke mtu wa kuisimamia? Je unataka biashara hiyo ndo uitegemee kwa maisha ya kila siku? Uko tayari kwenda kinyume cha imani yako(kama una imani/dini) ?

Malila, nikikurudishia hili swali, Investment ipi ina faida zaidi, ya muda mfupi au muda mrefu? Halafu ukisema Investment ya muda mfupi/mrefu una maanisha nini?

Kwa mfano; Biashara ya mama Ntilie, chapati na maandazo maofisini unaziweka kwenye kundi la short/long term investment? Kuhusu usimamizi na utegemezi inategemeana na ushauri nasaha toka kwenu wajasiriamali wazoefu.

What are you good at maana siyo kila mtu ni mjasiriamali au mfanya biashara.
Ushauri mzuri utategemea hilo swali vinginevyo unaweza kupoteza pesa zako.

...Good Question WoS, pamoja na swali lako zuri la nyongeza, naomba nikujibu kwamba nataka kutoka nje ya field yangu. Au kwakuwa nimetumia nusu ya umri wangu wa utu uzima kwenye fani fulani (isiyohusiana kabisa na biashara) haiwezekani kutupa karata kwenye biashara?

Bandugu,

You will fail 100% kama utatumia approach ya kusikia kwa watu ndio utekeleze.

The best project must come from you and not from other people. Sisi wengine ni kukupatia minofu michache lakini you must have the skeleton.

Ndio hayo tu.

WAZEE WA KUCHOMA NDIZI

...Nimekupata mzee wa kuchoma Ndizi, ndio maana nikatumbukiza swali langu hapa kupata mchango wa mawazo yenu. Labda nikuulize, hizo ndizi mnazochoma wateja wenu ni kina nani(bila kutaja majina), wakati gani, na kwanini ukadhani katika biashara zote, kuchoma ndizi ndio biashara inayokufaa?

Mbu! naomba uwatake radhi wanaJF wote waliokwisha kukushauri namna ya kuwekeza pesa ulizosema umekwapua sehemu. Kukwapua ni ufisadi tunaoupigia kelele hapa JF mpaka tunakosa muda wa kulala vizuri. Mi nitakushauri ukikanusha kuwa hujakwapua na iwe kweli hujakwapua mahala.

cheers

...Oh, cheers bm1. Nawataka radhi wana JF wote mliokwazika na neno hilo "kukwapua", maana sahihi ninayomaanisha ni; NIMEPATA/NIMEOKOTEZA/NIMEIBUA/NIMEZINYAKA. (dah, kiswahili kigumu!)
 
DECI
Panda sasa baada ya miezi minne tuu unavuna

...Okay, naona wewe una maanisha biashara yenye malengo ya muda mfupi! Mimi nataka niwekeze kwa maana iwe ni biashara ya mzunguko, inajizalisha, ikijiendeleza na kukua. Au ndio kusema hiyo DECI kila miezi minne faida inarudi na kujiongeza? nikiweka 10m/= nitafaidika kwa % ngapi, na risks ni zipi ukitilia maanani Global financial downturn?

Kanunue hisa za crdb ambazo zinauzwa at shs 150 per share. 10 m itakupatia shares 66,666. Hii maana yake nini. Kama ungepeleka DECI labda ungevuna 20m baada ya miezi 4? Sijui formula yao. Lakini ukinunua shares hizi crdb zikipelekwa kwenye soko la hisa unaweza ukaziuza zote halafu ukavuna zaidi ya asimia 100. Na hii ni baada sana sana ya miezi miwili. Kwa hiyo ukipata 20m zako iko mbaya gani/ U can decide kuziweka kwenye Fixed deposit ya hao crdb halafu ukaitumia hiyo kuombea mkopo. But this depends very much if u have a steady monthly income. Huo ni ushauri wangu wa bure

...Mawazo mazuri sana. Nautafakari kwanza ingawa kiroho kinanidunda hizo shares zinavyopanda na kushuka kila kukicha. Vipi security ya pesa zangu kwenye hayo mambo ya hisa versus Global financial downturn? How greater are the risks?

Mkuu Mosquito,

Njia nyingine pia ya kuharakisha mjadala ingekuwa kutuambia product idea zako halafu ukapata maoni kuhusu soko likoje kwa kila product idea.

Otherwise kama alivyosema WoS what's your core strength? Maana sio siri biashara ni zaidi ya mke, ni zaidi ya familia. You'll find yourself spending more time on your business especially in the beginning kuliko muda utakaokuwa unaspend na mamaa/papaa na watoto.

Off head kuna hii kitu ya online dating. You can throw a twist on the game by requiring your members to test for HIV, and charge men for ladies contacts.

Kuna wagoni wengi tu mfano maofisini ambao ni madomo zege lakini kila mwezi wanapenda kubadili mboga. Hao watakuwa wateja wako wakuu.

Plus internet population ya Tz itaexplode by Aug. this year .. so you can start building now.

...Product idea inatokana na market reseach kwanza au sio? Sijaifanyia hiyo kazi, ndio maana nimetumbukiza karata yangu hapa nijue ndugu zanguni ni biashara gani Tanzania kwa kamtaji ka 10m/= inaweza kulipa.

Kuhusu Online dating, na hiyo 'niche market' ya wanaume wenye midomo zege, ni idea nzuri lakini kwa mtaji wa 10m/= tu bro? halafu soko lenyewe ndio hilo 'maalumu', itawezekana kweli?

Kwa matatngazo zaidi inabidi upate ruksa ya wenye jamvi akina Invisible..lol

Nways, haya mambo ya stock market wadau wanasema sometimes huwa yanakuwa pata potea. Kwa jinsi ulivyoweka maelezo yako, it is like unauhakika kuwa bei za hisa zitapanda huko mbeleni which is a fallacy.

Stock market are stochastic in nature na kuna factor nyingi mno zinzaochangia bei kushuka au kupanda. Some of the factors are internal and can be internally controlled, some are external and never be controlled.

Ni vyema mhusika asichukulia maneno yako in totality.

...nakweli mazee, uki imagine mtu kama Adolf Merckle
amejiua sababu ya hizo stockmarket shares, itakuwa mimi Mbu na hii 'jackpot bingo' yangu!

Nafikiri Malila ameuliza maswali muhimu sana.

Kwa kuongezea tu, je unataka kuinvest kwenye biashara utayojihusisha moja kwa moja? Au ungependa kuinvest kwenye biashara ya mtu mwingine na wewe ukaplay kama investor na kusubiri returns?

Jinsi shamra shamra za ujasiliamali zinavyoendelea sasa bongo, kuna watu kibao wanambinu za kibiashara lakini hawana mtaji. Kwa hiyo, watu aina hii unaweza kuwatafuta na kuwaruhusu wa-pitch ideas zao kwako ili utathmini kama zinafaa kutumbukiza mtaji wako.

Au kama ungependelea kuanzisha biashara yako mwenyewe, then ingekuwa vizuri ukae kitako na kupitia kwa uangalifu aina ya biashara zote ambazo zinaweza kuendesheka bongo. Tatizo la hili ni kuwa Tshs. 10m sidhani kama inatosha kuanzisha biashara yoyote bongo ambayo revenue yake inaweza kukamatika ( as in you can feel it).

...naaam, naam ...ndio maana nikaja hapa kutumbukiza swali langu kama naweza zi 'pitch' hizo ideas zenu.

All in all, kama unaishi nje ya nchi, then cha kwanza kabisa utahitaji kufunga safari na kwenda bongo. Ukiwa nyumbani, tumia muda wako mwingi kukutana na watu mbalimbali. Hii itakupa nafasi ya kudadisi mbinu nyingi za kibiashara zinazoendelea nchini, pamoja na ku-networking.

Goodluck bro.

...Thanks, sijawahi kufanya biashara Tanzania. Sina uzoefu wa biashara yeyote! Naogopea hizo zunguka zunguka mitaani nitakumbana na wajanja halafu nije kula haka kamtaji! ndio maana naanza na mawazo yenu nyie watanzania wenzangu wa kwenye mtandao,...

...hivi Quemu ndio wewe QM aka QuickMover? kama ni wewe, vipi ile biashara ya Billboards uliyokuwa ukiifikiria mwaka juzi kuianzisha Tanzania? Ulifanikiwa?

Oa kama bado hujaoa na kama umeshaoa-ongeza wa pili au nyumba ndogo, life is too short, unaweza ukafa next month ukawaachia ugomvi ndugu zako kwa hizo hela!

...kaka, ndio kusema 10m/= ni invest kwenye ndoa kwa faida gani mkuu? au wakishazaliwa watoto waje wanifae uzeeni?

Mie naona Mbu uwekeze kwenye mfumo wa maji safi kule bongo, nenda sehemu ambazo hawana maji ya bomba na ukachimbe visima vya kutumia mota ya umeme ili wapate maji safi badala ya kuchota maji kwenye madimbwi. Hiyo pesa unaweza kuchimba visima 5, hapo utasaidia wananchi wenzako. Unaweza kurudisha pesa yako, iwapo utafanya kila ndoo ya maji ni shs 100.

Pretty, mawazo yako mazuri hayo ya kuuza maji, sema sasa...hizo sehemu unazosema hazina maji.. ambako naweza chimbisha visima... unahabari gharama ya kuchimbisha kisima kimoja sio chini ya 3.5m/= (shillingi za kitanzania)

Baada ya hapo nini uhakika wa umeme, pampu na ikiwezekana mlinzi au msimamizi wa kisima hicho kimoja. Gharama za uchimbaji na uendeshaji zitamaliza mtaji wote kwa kisima kimoja tu, halafu return yake itachukua miaka mingapi mamaa?

Biashara ya maji naiweka kapuni, labda kama kutoa sadaka tu kwa wananchi aka wapiga kura!
 
...Okay, naona wewe una maanisha biashara yenye malengo ya muda mfupi! Mimi nataka niwekeze kwa maana iwe ni biashara ya mzunguko, inajizalisha, ikijiendeleza na kukua. Au ndio kusema hiyo DECI kila miezi minne faida inarudi na kujiongeza? nikiweka 10m/= nitafaidika kwa % ngapi, na risks ni zipi ukitilia maanani Global financial downturn?
Unaweza kutoa sadaka kwa wapiga kura sio mbaya. hahahahahaha
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Kwa kuwa uko ya nchi,usimamizi kwa biashara nyingi hapa Bongo kwa sasa ni tatizo.Utakosana na jamaa zako bure,vijana wachache sana wanaweza kusimamia kwa uaminifu. Je wewe ni wa umri upi? Biashara za muda mrefu ni zile ambazo mavuno yake si ya leo. Hizo za maandazi na chapati ni za leo leo.

Biashara zenye high risk ndizo zenye high return na ambazo wabongo wengi wanazikimbia mzee. Karibu tuendelee kupeana ushauri.
 
wajameni eeh, nimebahatika "kupata" mahala ka-Mtaji. Ni kiasi cha shs. milioni kumi tu, (10,000,000/=) za Kitanzania.

Nipeni mapendekezo nizi invest wapi, kivipi na matarajio ya faida.
(i.e biashara gani inalipa (plus location), kwa muda gani, na SWOT analysis zake)

Yaani unataka info zote hizi free of charge? Kwa maoni yangu, hili lingekuwa zoezi la kwanza kabla ya hata kuchukua mtaji huo. Kama hujui la kufanya, urudishe tu ndugu yangu kama umekopa ili angalau kupunguza riba.
 
Mimi ni mfugaji, nitakushauri kufuga ngombe kwa mchakato ufuatao:

Ujenzi wa banda = Ths 500,000/=
Manunuzi ya Ngombe 5 x Tsh 900,000 = Tsh 4,500,000/=
(Ngombe utawanunua wakiwa na mimba ya miezi 6)
Kuwahudumia ng'ombe kwa miezi mitatu kabla ya production = Tsh 1,500,000/=
(inahusisha mshahara kwa wafanyakazi wawil + chakula + madawa)

Jumla = Tsh 6,500,000/=

Baada ya Miezi 3;

UZALISHAJI:

Ngombe hawa watakuwa wakitoa maziwa si pungufu ya lita 5 kwa asubuhi na jioni kwa kila ng'ombe. Hivyo uzalishaji kwa siku utakuwa lita 10 kwa siku kwa ng'ombe.

MAPATO

Lita 10 x Ng'ombe 5 = lita 50 kwa siku x Tsh 1000 (bei ninayouza mimi hapa) = Tsh 50,000 kwa siku
Mapato kwa mwezi = Tsh 50,000 x 30 = 1,500,000/=

Gharama za uendeshaji kwa mwezi = Tsh 600,000/=

Faida = Tsh 900,000/= kwa mwezi

BAADA YA MIAKA 5:

Kumbuka ng'ombe huzaa kila mwaka hivyo basi baada ya miaka mitano utakuwa na ng'ombe wasiopungua 25. Kipato chako kwa mwezi unaweza kufikia si pungufu Tsh 18,000,000 endapo utakuwa na ngombe jike 20 kati ya hao 25.
 
...Nimekupata mzee wa kuchoma Ndizi, ndio maana nikatumbukiza swali langu hapa kupata mchango wa mawazo yenu. Labda nikuulize, hizo ndizi mnazochoma wateja wenu ni kina nani(bila kutaja majina), wakati gani, na kwanini ukadhani katika biashara zote, kuchoma ndizi ndio biashara inayokufaa?
Mkuu Mbu,

Sisi hatuchomi ndizi kwa biashara ya kumsubiri mteja tusiemfahamu, hatuhitaji matangazo wala utambulisho. Sisi ni wateja na wao pia ni wateja, hivyo kwa pamoja tunachoma ndizi.
 
36 Reactions
Reply
Back
Top Bottom