King_Villa
JF-Expert Member
- Feb 6, 2012
- 574
- 378
Nampenda sana mke wangu ila cha ajabu haniamini kabisa mi nampenda. Ninamwambia kila siku vile nampenda hanielewi. Amekuwa akinifuatilia hadi ofisini. Na akifika hataki hata kuongea na secretary. Ni moja kwa moja anakimbilia niliko na kushika simu yangu.
Boss ameshaniambia sio vizuri eneo la kazi kufanya hivyo ila huwa ye haelewi. Nami nilishamwambia hilo hataki kuelewa. Sasa kumfukuza siwezi na kumwacha siwezi ila natafuta njia ya kuweka mambo sawa awe mpole.
Kwani tatizo nini mtu kuwa na mtu wa pembeni alafu akawa hamjali na anakujali wewe tu. Cha msingi wewe ndo mke halali na si mwingine na wewe ndio amekutambulisha hajatambulisha mwingine. Yani tatizo linakuja wapi enyi wanawake mnaokuwa na wivu wa namna hii usio na maana.?
Wanawake badilikeni na muende na wakati kuna mabadiliko mengi yanayowatokea ambayo lazima muelewe kuwa yatamtesa umpendae .
Nyakati za mwanamke anapokuwa mjamzito ni nyakati ngumu sana kwa mwanaume. Kwasababu itamlazimu akae kipindi kirefu bila kufanya tendo pendwa na mke wake (najua mnajua)
Sasa kuna wanaume wanaoweza wengine hatuwezi kiukweli ni swala la kuelewa na wakati mwingine kunishauri nifanye kwa uangalifu magonjwa ni mengi. Sio kuanza kukurupuka kugombana na majirani unaowakuta na mimi, unanifanya naonekana sio mwaminifu kwa mke wangu.
Ni swala la nyakati ulionayo ndio linasababisha yote haya ukisharudi kwenye hali yako ya kawaida maisha yanaendelea kama kawaida na mambo yatakuwa sawa. Inamaana nivumilie muda wote huo asee miezi kama tisa hivi ni mambo ya kizamani kiukweli nimeshindwa.
Unakuta kuna nyakati zinafika unasikia hamu mpaka mwili unatetemeka asee. Tena kama vijana tuliowahi kuoa tunateseka sana katika wakati huu. Aseee mi naomba mke wangu anisamehe na anikubali tu bado upendo uko kwake.
Nawashauri tu wanawake wapendeni waume zenu na mkubaliane na hali halisi wakati mwingine majaribu yanazidi kipimo.
Kwa wanaume nipeni ushauri tu niweze kuwa na mama watoto muda wote asinione namsaliti ajue bado mi ni wake tu na asijali kuhusu mambo mengine.
Boss ameshaniambia sio vizuri eneo la kazi kufanya hivyo ila huwa ye haelewi. Nami nilishamwambia hilo hataki kuelewa. Sasa kumfukuza siwezi na kumwacha siwezi ila natafuta njia ya kuweka mambo sawa awe mpole.
Kwani tatizo nini mtu kuwa na mtu wa pembeni alafu akawa hamjali na anakujali wewe tu. Cha msingi wewe ndo mke halali na si mwingine na wewe ndio amekutambulisha hajatambulisha mwingine. Yani tatizo linakuja wapi enyi wanawake mnaokuwa na wivu wa namna hii usio na maana.?
Wanawake badilikeni na muende na wakati kuna mabadiliko mengi yanayowatokea ambayo lazima muelewe kuwa yatamtesa umpendae .
Nyakati za mwanamke anapokuwa mjamzito ni nyakati ngumu sana kwa mwanaume. Kwasababu itamlazimu akae kipindi kirefu bila kufanya tendo pendwa na mke wake (najua mnajua)
Sasa kuna wanaume wanaoweza wengine hatuwezi kiukweli ni swala la kuelewa na wakati mwingine kunishauri nifanye kwa uangalifu magonjwa ni mengi. Sio kuanza kukurupuka kugombana na majirani unaowakuta na mimi, unanifanya naonekana sio mwaminifu kwa mke wangu.
Ni swala la nyakati ulionayo ndio linasababisha yote haya ukisharudi kwenye hali yako ya kawaida maisha yanaendelea kama kawaida na mambo yatakuwa sawa. Inamaana nivumilie muda wote huo asee miezi kama tisa hivi ni mambo ya kizamani kiukweli nimeshindwa.
Unakuta kuna nyakati zinafika unasikia hamu mpaka mwili unatetemeka asee. Tena kama vijana tuliowahi kuoa tunateseka sana katika wakati huu. Aseee mi naomba mke wangu anisamehe na anikubali tu bado upendo uko kwake.
Nawashauri tu wanawake wapendeni waume zenu na mkubaliane na hali halisi wakati mwingine majaribu yanazidi kipimo.
Kwa wanaume nipeni ushauri tu niweze kuwa na mama watoto muda wote asinione namsaliti ajue bado mi ni wake tu na asijali kuhusu mambo mengine.