Nielewesheni hili kuhusu taasisi ya Tanzania Social Saport Foundation

PANAFRICA

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
335
496
Nimeona tangazo la NGO ya Tanzania social support foundation, kuwa wanatoa ufadhili na mikopo kwa wanachuo wa vyuo vya elimu ya juu.Ili maombi yako yaweze kuhalalishwa inabidi muombaji aambatanishe kiasi cha fedha taslim SHS.50000/=.
Je hii NGO wafadhili wao ni kina nani? tovuti yao haionyshi nani ni wafadhili wa NGO hiyo!

Nimejiuliza kuwa NGO hii haiwezi kutumia fursa ya tatizo la ukosefu wa mikopo na kuja na mbinu ya kutoa scholarships za elimu ya juu kwa lengo la kujinufaisha? Fikiria mfano wakiomba wanafunzi 3000 nchi nzima X shs.50,000=150,000,000. Wakiweza kutoa 50,000,000 wakafadhili baadhi tu ya walioomba itahalalisha malengo ya taasisi wakati ikibaki na 100,000,000/=.

Naomba nisieleweke kama nina mtazamo hasi kuhusu malengo ya TSSF, ila ni swali fikirishi ili isije kuwa ni mbinu ya kujipatia kipato kwa kutumia fursa ya mbinyo kwa watanzania wanaohaha hasa kipindi hiki ambapo mikopo ya elimu ya juu imekuwa ni shida. ni mawazo yangu tu jamani silengi kumkwaza yeyote.
 

Attachments

  • tssf_application_form__for__scholarships_and_tuition_waivers_for_2017_-_2018_academic_year.pdf
    281.5 KB · Views: 354
Nimeona tangazo la NGO ya Tanzania social support foundation, kuwa wanatoa ufadhili na mikopo kwa wanachuo wa vyuo vya elimu ya juu.Ili maombi yako yaweze kuhalalishwa inabidi muombaji aambatanishe kiasi cha fedha taslim SHS.50000/=.
Je hii NGO wafadhili wao ni kina nani? tovuti yao haionyshi nani ni wafadhili wa NGO hiyo!

Nimejiuliza kuwa NGO hii haiwezi kutumia fursa ya tatizo la ukosefu wa mikopo na kuja na mbinu ya kutoa scholarships za elimu ya juu kwa lengo la kujinufaisha? Fikiria mfano wakiomba wanafunzi 3000 nchi nzima X shs.50,000=150,000,000. Wakiweza kutoa 50,000,000 wakafadhili baadhi tu ya walioomba itahalalisha malengo ya taasisi wakati ikibaki na 100,000,000/=. Naomba nisieleweke kama nina mtazamo hasi kuhusu malengo ya TSSF, ila ni swali fikirishi ili isije kuwa ni mbinu ya kujipatia kipato kwa kutumia fursa ya mbinyo kwa watanzania wanaohaha hasa kipindi hiki ambapo mikopo ya elimu ya juu imekuwa ni shida. ni mawazo yangu tu jamani silengi kumkwaza yeyote.

Mtoa posti nadhani labda kuna kitu hujakielewa vizuri kwa sababu kichwa cha habari ya posti yako kinasema kwamba "Uelewa kuhusu Taasisi ya Tanzania Social Support Foundation" lakini kwenye maelezo ya hoja yako yanaelezea kwa kujichanganya maana mwanzoni unazungumzia mikopo halafu huku mwishoni unazungumzia scholarship!!! Sasa binafsi sijaelewa unazungumzia nini ila nimehamasika tu kuchangia kwa sababu mimi ni Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (Mbeya University of Science and Technology). Hilo tangazo la TSSF nimeliona kwenye tovuti ya chuo chetu (http://www.mustnet.ac.tz/documents/Scholarships.pdf) na nimefuatilia chuoni nikapewa mrejesho kwamba, chuo kilipokea taarifa kutoka TSSF kuhusiana na hizo scholarship na hiyo TSSF iliwasilisha taarifa zote za huo ufadhili chuoni na chuo kikajiridhisha na kutangaza.

Vilevile mimi nimesoma tangazo lao na sifa za mwombaji, kigezo siyo hiyo elfu hamsini tu pia vipo na vigezo vingine ambavyo vinaelekeana na vile vya bodi ya mikopo. Sasa wewe umeona hicho kimoja tu?? Lakini uliwahi kuona wapi msaada wa bure??? Hata Bodi ya Mikopo napo unalipia sasa sioni tatizo lipo wapi afterall hiyo TSSF siyo ya kwanza kutangaza nafasi za ufadhili wa masomo. Mbona DAAD, Statoil, GGM, Fulbright, Chievening na wao pia hutangaza??
Vilevile ukisoma taarifa ya TSSF kwa vyombo vya habari ambayo ipo kwenye mtandao wao, inaonyesha kuwa anayeifadhili TSSF ni CDF International kutoka Seattle, Washington, Nchini Marekani.

Kama mtu ana wasiwasi wa kutapeliwa au vinginevyo nadhani JF siyo mahali pa kulalamikia ila mtu unachukua hatua kwa kuwasiliana wahusika au kwenda serikalini na kuhoji kama hao wanatambulika kisheria ili kama ni matapeli wachukuliwe hatua! Ila kuleta hoja kama hizi huku ni uchochezi na unaweza kushtakiwa kwa kuharibu jina na hadhi ya taasisi za watu!! Ni mawazo yangu tu lakini! Usinifikirie vibaya kwa sababu siyo kwamba ninawatetea hao TSSF ila tunafikirishana tu kwa upande mwingine maana mjini cha bure salamu!! Vingine vyote gharama na bure ghali!!!
 
Nimeona tangazo la NGO ya Tanzania social support foundation, kuwa wanatoa ufadhili na mikopo kwa wanachuo wa vyuo vya elimu ya juu.Ili maombi yako yaweze kuhalalishwa inabidi muombaji aambatanishe kiasi cha fedha taslim SHS.50000/=.
Je hii NGO wafadhili wao ni kina nani? tovuti yao haionyshi nani ni wafadhili wa NGO hiyo!

Nimejiuliza kuwa NGO hii haiwezi kutumia fursa ya tatizo la ukosefu wa mikopo na kuja na mbinu ya kutoa scholarships za elimu ya juu kwa lengo la kujinufaisha? Fikiria mfano wakiomba wanafunzi 3000 nchi nzima X shs.50,000=150,000,000. Wakiweza kutoa 50,000,000 wakafadhili baadhi tu ya walioomba itahalalisha malengo ya taasisi wakati ikibaki na 100,000,000/=. Naomba nisieleweke kama nina mtazamo hasi kuhusu malengo ya TSSF, ila ni swali fikirishi ili isije kuwa ni mbinu ya kujipatia kipato kwa kutumia fursa ya mbinyo kwa watanzania wanaohaha hasa kipindi hiki ambapo mikopo ya elimu ya juu imekuwa ni shida. ni mawazo yangu tu jamani silengi kumkwaza yeyote.

Fungua hii anwani ujisomee. Huenda ikajibu maswali yako.

http://tssf-org-tz.weebly.com/uploa...vyombo_vya_habari__mfuko_wa_elimu_ya_juu_.pdf
 
Back
Top Bottom