MchunguZI
JF-Expert Member
- Jun 14, 2008
- 4,006
- 2,165
Kwa wakaazi wa Dar munafahamu wazi kwamba kuishi karibu na kambi yoyote ya kijeshi ni balaa! Ukiwaondoa magereza, wengine wote ni tatizo la kudumu. Wanatembea mitaani wakinywa pombe wakisaka akina mama na baadaye ni ugomvi hata wa kutumia siraha bila sababu yoyote. Bahati mbaya sehemu kubwa ya watu hawa ni wanaume.
Ajira ktk majeshi yetu ilikuwa ni kwa sifa za misuri na uwezo wa kukimbia. Baadaye usomi umepewa nafasi lakini nidhamu imebaki Kuwa ni sifa isiyopatikana jeshini.
Matukio ya hivikaribuni kwangu Mimi niliyategemea. Jeshi letu Lina waajiliwa wapuuzi kwa kiwango cha juu sana. Askari wa kuuliza ghasia Mara nyingi wamepambana na raia na bahati mbaya akina mama huoni aibu kutaja matukio Kama haya. Vijana wa vyuo vikuu ni shahidi kwamba Mara zote wanapopambana, matukio ya kudhalilisha akina dada imekuwa ni tabia inayotajwa. Sasa kwa watawala hudhani ni sifa kwa muhalifu kudhalilishwa au vyuo vikuu 'kukomeshwa'. Hii ni aibu!
JWTZ pia ni aibu tu. ktk vita ya Uganda, sehemu kubwa ya wanajeshi waliufanyaje baada ya vita kuliko wakati wa vita. Matukio makubwa yakitokana na tabia ya ngono. Walitumia siraha kulazimisha ngono. Waganda wamekufa kwa kupigwa risasi pia wengine kwa sababu tu ya kugoma kuifanya ngono! Walipowahiwa pia wakauwawa.
Msumbiji yalikuwa hayo hayo! Huko pia uporaji uliwalenga wenye pesa. Tumeshuhudia ma-Benz yakishushwa kwenye ndege za jeshi zinazotoka Msumbiji.
Jeshi lenye ubongo wa aina hii utalitumiaje ktk shughuli za kiraia? Bahati mbaya anayesema anapewa zigo la kuambiwa atowe ushahidi badala ya muhusika kuchunguza undani na Kuwatia nidhamu.
Duniani kote matukio haya hutokea lakini uzuri wahusika huchukuwa hatua na kukomesha upuuzi Kama huo. Imekuwaje kwa TZ hata kuzuiya askari kuwapiga majirani imekuwa ni ndoto? Tena ndani ya Dar!
Je, wahusika huvaa kimya kwa sababu hata wao wamewatumia kutimiza upuuzi wao? Pia inawezekana. Tunajua jinsi siasa inavyotumika vibaya kwa kuvitumia vyombo vya dola. Hata bungeni tunayaona. Mwanasheria mkuu wa Serikali amegeuzwa kuwa Mwanasiasa mkuu wa serikali.
Bila vichwa vipya ktk serikali, hatutapiga hatua yoyote. Kwa ujumla tumeruhusu wapuuzi wengi kujiunga siasa na sasa wanaongoza nchi.
Ajira ktk majeshi yetu ilikuwa ni kwa sifa za misuri na uwezo wa kukimbia. Baadaye usomi umepewa nafasi lakini nidhamu imebaki Kuwa ni sifa isiyopatikana jeshini.
Matukio ya hivikaribuni kwangu Mimi niliyategemea. Jeshi letu Lina waajiliwa wapuuzi kwa kiwango cha juu sana. Askari wa kuuliza ghasia Mara nyingi wamepambana na raia na bahati mbaya akina mama huoni aibu kutaja matukio Kama haya. Vijana wa vyuo vikuu ni shahidi kwamba Mara zote wanapopambana, matukio ya kudhalilisha akina dada imekuwa ni tabia inayotajwa. Sasa kwa watawala hudhani ni sifa kwa muhalifu kudhalilishwa au vyuo vikuu 'kukomeshwa'. Hii ni aibu!
JWTZ pia ni aibu tu. ktk vita ya Uganda, sehemu kubwa ya wanajeshi waliufanyaje baada ya vita kuliko wakati wa vita. Matukio makubwa yakitokana na tabia ya ngono. Walitumia siraha kulazimisha ngono. Waganda wamekufa kwa kupigwa risasi pia wengine kwa sababu tu ya kugoma kuifanya ngono! Walipowahiwa pia wakauwawa.
Msumbiji yalikuwa hayo hayo! Huko pia uporaji uliwalenga wenye pesa. Tumeshuhudia ma-Benz yakishushwa kwenye ndege za jeshi zinazotoka Msumbiji.
Jeshi lenye ubongo wa aina hii utalitumiaje ktk shughuli za kiraia? Bahati mbaya anayesema anapewa zigo la kuambiwa atowe ushahidi badala ya muhusika kuchunguza undani na Kuwatia nidhamu.
Duniani kote matukio haya hutokea lakini uzuri wahusika huchukuwa hatua na kukomesha upuuzi Kama huo. Imekuwaje kwa TZ hata kuzuiya askari kuwapiga majirani imekuwa ni ndoto? Tena ndani ya Dar!
Je, wahusika huvaa kimya kwa sababu hata wao wamewatumia kutimiza upuuzi wao? Pia inawezekana. Tunajua jinsi siasa inavyotumika vibaya kwa kuvitumia vyombo vya dola. Hata bungeni tunayaona. Mwanasheria mkuu wa Serikali amegeuzwa kuwa Mwanasiasa mkuu wa serikali.
Bila vichwa vipya ktk serikali, hatutapiga hatua yoyote. Kwa ujumla tumeruhusu wapuuzi wengi kujiunga siasa na sasa wanaongoza nchi.