NIDA waagizwa kufanya kazi saa 16 ili kutimiza agizo la Rais Magufuli

mamayoyo1

JF-Expert Member
Jul 25, 2018
1,011
1,019


Katika kwenda sambamba na siku 20 zilizoongezwa na Rais Dkt. John Magufuli wakati akisajili laini yake ya simu kwa alama za vidole Desemba 27,2019 mjini Chato mkoani Geita, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wametakiwa kuongeza idadi ya watumishi katika kituo cha kuchakata taarifa za waombaji nchi nzima kilichopo Kibaha mkoani Pwani ili kuhakikisha kila mwananchi anayekidhi vigezo kupata Kitambulisho cha Taifa ili aweze kusajili laini yake ya simu.

Akizungumza baada ya kutembelea kituo hicho Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dkt. Anold Kihaule kuongeza idadi ya watumishi katika kituo hicho na kuongeza pia masaa ya kufanya kazi kutoka nane mpaka kumi na sita ili kuhakikisha wananchi wanapata namba na vitambulisho baada ya nyongeza ya siku 20 ziliyotolewa na Rais Magufuli.

“Nimetembea katika vituo mbalimbali vya NIDA nchi nzima, changamoto kubwa wanayotoa wananchi ni kwenda kila siku kufuatilia kitambulisho au namba katika kituo husika lakini wamekuwa wakipata majibu kwamba bado kipo kwenye mchakato, wakati mwingine ameomba miaka mitatu iliyopita sasa anapoteza muda na gharama kufuatilia kitambulisho lakini nimetembelea hapa leo nimegundua uchache wa watumishi,mkurugenzi ongeza watumishi hapa..” alisema Masauni

Naomba pia ongeza muda wa kufanya kazi,kutoka masaa nane mpaka kumi na sita, Rais ashasema muda hautaongezwa wa usajili laini za simu, sasa wananchi wanafurika na kupata taabu vituoni huko, sisi ndio wawakilishi wao lazima tuwasemee na mkuu wa nchi ashatoa maelekezo sasa ni utekelezaji tu” aliongeza Masauni

Akizungumza katika ziara hiyo Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dkt. Anold Kihaule alisema watayatekeleza maagizo hayo ya serikali huku akiwaasa wananchi ambao tayari wana namba za utambulisho waende kusajili laini zao ili kwenda sambamba na muda ulioongezwa na Rais Dkt. Magufuli.

“Jumla ya watu milioni 7.6 tayari wana namba za utambulisho nchi nzima na kila siku tunaendelea kutoa namba hizo sehemu mbalimbali nchini na mnaweza kuona kwa Dar es Salaam katika Viwanja vya Mnazi Mmoja tunatoa namba pale na ni zoezi la siku zote za wiki, hatuna sikukuu wala siku za mwisho za wiki” alisema Dkt.Kihaule

Kila mmiliki wa simu ya mkononi anatakiwa kusajili laini yake kwa alama za vidole kwani kutofanya hivyo itamaanisha kutoweza kupiga wala kupokea simu, vile vile muhusika hatoweza kutuma wala kupokea ujumbe mfupi wa maneno.
 
Ajira hizo wazee wa IT
Hawa jamaa ingawa serikali hawatambui wala hamna hata salary scale yao huko ofisi paendwa ila wanae kazi muhimu aiseh
 


Katika kwenda sambamba na siku 20 zilizoongezwa na Rais Dkt. John Magufuli wakati akisajili laini yake ya simu kwa alama za vidole Desemba 27,2019 mjini Chato mkoani Geita, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wametakiwa kuongeza idadi ya watumishi katika kituo cha kuchakata taarifa za waombaji nchi nzima kilichopo Kibaha mkoani Pwani ili kuhakikisha kila mwananchi anayekidhi vigezo kupata Kitambulisho cha Taifa ili aweze kusajili laini yake ya simu.

Akizungumza baada ya kutembelea kituo hicho Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dkt. Anold Kihaule kuongeza idadi ya watumishi katika kituo hicho na kuongeza pia masaa ya kufanya kazi kutoka nane mpaka kumi na sita ili kuhakikisha wananchi wanapata namba na vitambulisho baada ya nyongeza ya siku 20 ziliyotolewa na Rais Magufuli.

“Nimetembea katika vituo mbalimbali vya NIDA nchi nzima, changamoto kubwa wanayotoa wananchi ni kwenda kila siku kufuatilia kitambulisho au namba katika kituo husika lakini wamekuwa wakipata majibu kwamba bado kipo kwenye mchakato, wakati mwingine ameomba miaka mitatu iliyopita sasa anapoteza muda na gharama kufuatilia kitambulisho lakini nimetembelea hapa leo nimegundua uchache wa watumishi,mkurugenzi ongeza watumishi hapa..” alisema Masauni



Akizungumza katika ziara hiyo Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dkt. Anold Kihaule alisema watayatekeleza maagizo hayo ya serikali huku akiwaasa wananchi ambao tayari wana namba za utambulisho waende kusajili laini zao ili kwenda sambamba na muda ulioongezwa na Rais Dkt. Magufuli.

“Jumla ya watu milioni 7.6 tayari wana namba za utambulisho nchi nzima na kila siku tunaendelea kutoa namba hizo sehemu mbalimbali nchini na mnaweza kuona kwa Dar es Salaam katika Viwanja vya Mnazi Mmoja tunatoa namba pale na ni zoezi la siku zote za wiki, hatuna sikukuu wala siku za mwisho za wiki” alisema Dkt.Kihaule

Kila mmiliki wa simu ya mkononi anatakiwa kusajili laini yake kwa alama za vidole kwani kutofanya hivyo itamaanisha kutoweza kupiga wala kupokea simu, vile vile muhusika hatoweza kutuma wala kupokea ujumbe mfupi wa maneno.
Vipi mtu awe kazini masaa 16? Atalala saa ngapi kwa siku? Kwanini asiwaambie wafaye kwa shifts za 8 hrs kila shift? Au hajui sheria za kazi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 


Katika kwenda sambamba na siku 20 zilizoongezwa na Rais Dkt. John Magufuli wakati akisajili laini yake ya simu kwa alama za vidole Desemba 27,2019 mjini Chato mkoani Geita, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wametakiwa kuongeza idadi ya watumishi katika kituo cha kuchakata taarifa za waombaji nchi nzima kilichopo Kibaha mkoani Pwani ili kuhakikisha kila mwananchi anayekidhi vigezo kupata Kitambulisho cha Taifa ili aweze kusajili laini yake ya simu.

Akizungumza baada ya kutembelea kituo hicho Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dkt. Anold Kihaule kuongeza idadi ya watumishi katika kituo hicho na kuongeza pia masaa ya kufanya kazi kutoka nane mpaka kumi na sita ili kuhakikisha wananchi wanapata namba na vitambulisho baada ya nyongeza ya siku 20 ziliyotolewa na Rais Magufuli.

“Nimetembea katika vituo mbalimbali vya NIDA nchi nzima, changamoto kubwa wanayotoa wananchi ni kwenda kila siku kufuatilia kitambulisho au namba katika kituo husika lakini wamekuwa wakipata majibu kwamba bado kipo kwenye mchakato, wakati mwingine ameomba miaka mitatu iliyopita sasa anapoteza muda na gharama kufuatilia kitambulisho lakini nimetembelea hapa leo nimegundua uchache wa watumishi,mkurugenzi ongeza watumishi hapa..” alisema Masauni



Akizungumza katika ziara hiyo Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dkt. Anold Kihaule alisema watayatekeleza maagizo hayo ya serikali huku akiwaasa wananchi ambao tayari wana namba za utambulisho waende kusajili laini zao ili kwenda sambamba na muda ulioongezwa na Rais Dkt. Magufuli.

“Jumla ya watu milioni 7.6 tayari wana namba za utambulisho nchi nzima na kila siku tunaendelea kutoa namba hizo sehemu mbalimbali nchini na mnaweza kuona kwa Dar es Salaam katika Viwanja vya Mnazi Mmoja tunatoa namba pale na ni zoezi la siku zote za wiki, hatuna sikukuu wala siku za mwisho za wiki” alisema Dkt.Kihaule

Kila mmiliki wa simu ya mkononi anatakiwa kusajili laini yake kwa alama za vidole kwani kutofanya hivyo itamaanisha kutoweza kupiga wala kupokea simu, vile vile muhusika hatoweza kutuma wala kupokea ujumbe mfupi wa maneno.
Hata wakifanya 24/365 hakuna jipya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom