NIDA na Serikali kwa ujumla, mmeshindwa kwa zaidi ya miaka mitatu, mtaweza ndani ya siku 20? Usajili kwa alama za vidole unabagua wananchi wa vijijini

Yacoubu

Member
Nov 23, 2019
29
123
Mmeanza zamani sana kuandikisha vitambulisho vya Taifa. Hali ilipamba moto mwaka 2017 pale watumishi wa umma walipolazimika kujiandikisha kwa lazima.

Tuliwaona jinsi vituo vyao vya kazi vilivyokuwa vinafungwa ili waende kuhakikiwa. Hongera zao, hakuna mtumishi wa umma asiye na kitambulisho cha NIDA.

Shida inakuja kwetu wa kijijini. Walileta fomu tukajaza (fomu zenyewe zilikuwa zinauzwa). Fomu zilikusanywa ila hawajawahi kuja kutupiga picha.

Kwahiyo namba za NIDA hatuna. Achilia mbali vitambulisho.

Hata mkifanya kazi masaa 24, bado raia wa kijijini hamuwezi kuwafikia. Tuseme hivi, usajili wa laini ni kwa watumishi wa umma na wananchi wa mjini.

Mnaenda kuvunja mahusiano ya watu ambayo yalitegemea mawasiliano ya simu. Pia mnarudi pale pale mtu mmoja kusajili laini zaidi ya kumi.

Kwa mfano, hapa kijijini kuna mwalimu kutokea mkoa mwingine kaoa kwenye familia moja. Kwakuwa hawana namba za simu amelazimika kusajili laini zake tatu, laini mbili kwa mke wake, na zingine kwa baba mkwe, mama mkwe na mashemeji wawili.

Hata ukisajili mtandao mmoja laini zaidi ya moja, HAIKATAI, INAKUBALI.

Naona bado kuna tatizo
 
Kijji chetu waalimu tu ndio wamesajili laini.
Na kwa vile wanaenda wilayani.

Ila wengine wote hawana namba za Nida na kwenda wilayani ni umbali.

Viongozi wanadhani Tanzania ni Chato na dsm na dodoma. Kuna vijiji huko waulizeni Haloteli wanajua vijijini kupoje.
Labda tutahamia safaricom
 
Kijji chetu waalimu tu ndio wamesajili laini.
Na kwa vile wanaenda wilayani.

Ila wengine wote hawana namba za Nida na kwenda wilayani ni umbali.

Viongozi wanadhani Tanzania ni Chato na dsm na dodoma. Kuna vijiji huko waulizeni Haloteli wanajua vijijini kupoje.
Labda tutahamia safaricom
Kiukweli, serikali iliangalie hili. Haina maana kuwafungia laini ilihali wao hawana makosa ya kutopata namba za nida. NIDA ni tatizo.

Ndiyo maana nikasema simu sasahivi watatumia wstumishi wa umma na baadhi ya wananchi tu hasa wa mjini
 
Kuandikisha watu wakuwapigia "kula" wanawafikia,lakini hizi habar za ID watumie gharama ili waweza kupata.

Nchi ni yetu sote hata hao walio vijijini.

Nashangaa kampuni sa simu zimekuwa kimya tu...upande wa comply wanashindwa ku complain.

Itawagharimu hadi mapato kwao hata kama walishatupiga vya kutosha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mmeanza zamani sana kuandikisha vitambulisho vya Taifa. Hali ilipamba moto mwaka 2017 pale watumishi wa umma walipolazimika kujiandikisha kwa lazima.

Tuliwaona jinsi vituo vyao vya kazi vilivyokuwa vinafungwa ili waende kuhakikiwa. Hongera zao, hakuna mtumishi wa umma asiye na kitambulisho cha NIDA.

Shida inakuja kwetu wa kijijini. Walileta fomu tukajaza (fomu zenyewe zilikuwa zinauzwa). Fomu zilikusanywa ila hawajawahi kuja kutupiga picha.

Kwahiyo namba za NIDA hatuna. Achilia mbali vitambulisho.

Hata mkifanya kazi masaa 24, bado raia wa kijijini hamuwezi kuwafikia. Tuseme hivi, usajili wa laini ni kwa watumishi wa umma na wananchi wa mjini.

Mnaenda kuvunja mahusiano ya watu ambayo yalitegemea mawasiliano ya simu. Pia mnarudi pale pale mtu mmoja kusajili laini zaidi ya kumi.

Kwa mfano, hapa kijijini kuna mwalimu kutokea mkoa mwingine kaoa kwenye familia moja. Kwakuwa hawana namba za simu amelazimika kusajili laini zake tatu, laini mbili kwa mke wake, na zingine kwa baba mkwe, mama mkwe na mashemeji wawili.

Hata ukisajili mtandao mmoja laini zaidi ya moja, HAIKATAI, INAKUBALI.

Naona bado kuna tatizo
NIDA haikuzingatia “activity calendar” ya kilimo kwa watu wengi wa vijijini. Mvua za vuli huwa Oktoba hadi Desemba na masika ni Machi hadi Juni. Kwa maeneo ya kusini mvua huanza Novemba hadi Machi. Vipindi hivi ni muhimu kwa uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara. Zoezi la NIDA lingefanikiwa kama usajili ungefungwa Juni 2020. Pia huduma zipatikane ngazi ya kijiji sio kata au wilaya. Kipindi hiki usafiri vijijini ni wa shida kwa sababu ya mvua. Pia uchumi vijijini umeshuka kwa wananchi kuwekeza kwenye kilimo na baadhi ya wakulima wa pamba na korosho bado hawajslipwa mazao yao baada kuuza kupitia AMCOS. Mkulima atasita kupoteza siku 2 au zaidi kufuatilia usajili huku anahitajika kupanda au kupalilia mazao yake.
 
Mmeanza zamani sana kuandikisha vitambulisho vya Taifa. Hali ilipamba moto mwaka 2017 pale watumishi wa umma walipolazimika kujiandikisha kwa lazima.

Tuliwaona jinsi vituo vyao vya kazi vilivyokuwa vinafungwa ili waende kuhakikiwa. Hongera zao, hakuna mtumishi wa umma asiye na kitambulisho cha NIDA.

Shida inakuja kwetu wa kijijini. Walileta fomu tukajaza (fomu zenyewe zilikuwa zinauzwa). Fomu zilikusanywa ila hawajawahi kuja kutupiga picha.

Kwahiyo namba za NIDA hatuna. Achilia mbali vitambulisho.

Hata mkifanya kazi masaa 24, bado raia wa kijijini hamuwezi kuwafikia. Tuseme hivi, usajili wa laini ni kwa watumishi wa umma na wananchi wa mjini.

Mnaenda kuvunja mahusiano ya watu ambayo yalitegemea mawasiliano ya simu. Pia mnarudi pale pale mtu mmoja kusajili laini zaidi ya kumi.

Kwa mfano, hapa kijijini kuna mwalimu kutokea mkoa mwingine kaoa kwenye familia moja. Kwakuwa hawana namba za simu amelazimika kusajili laini zake tatu, laini mbili kwa mke wake, na zingine kwa baba mkwe, mama mkwe na mashemeji wawili.

Hata ukisajili mtandao mmoja laini zaidi ya moja, HAIKATAI, INAKUBALI.

Naona bado kuna tatizo
Tusubirie tamko baada ya siku 20 kuisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nasubiri 20/01/2020 laini zangu zifungiwe, nami nifungie simu kabatini.
 
Msiogope hakuna line inayofungiwa hizo ni mbwembwe tu maana sirikali yetu huwa ina viongozi wasiojielewa ndio maana huwa wanakuja na policies zisizotekelezeka.
 
Mmeanza zamani sana kuandikisha vitambulisho vya Taifa. Hali ilipamba moto mwaka 2017 pale watumishi wa umma walipolazimika kujiandikisha kwa lazima.

Tuliwaona jinsi vituo vyao vya kazi vilivyokuwa vinafungwa ili waende kuhakikiwa. Hongera zao, hakuna mtumishi wa umma asiye na kitambulisho cha NIDA.

Shida inakuja kwetu wa kijijini. Walileta fomu tukajaza (fomu zenyewe zilikuwa zinauzwa). Fomu zilikusanywa ila hawajawahi kuja kutupiga picha.

Kwahiyo namba za NIDA hatuna. Achilia mbali vitambulisho.

Hata mkifanya kazi masaa 24, bado raia wa kijijini hamuwezi kuwafikia. Tuseme hivi, usajili wa laini ni kwa watumishi wa umma na wananchi wa mjini.

Mnaenda kuvunja mahusiano ya watu ambayo yalitegemea mawasiliano ya simu. Pia mnarudi pale pale mtu mmoja kusajili laini zaidi ya kumi.

Kwa mfano, hapa kijijini kuna mwalimu kutokea mkoa mwingine kaoa kwenye familia moja. Kwakuwa hawana namba za simu amelazimika kusajili laini zake tatu, laini mbili kwa mke wake, na zingine kwa baba mkwe, mama mkwe na mashemeji wawili.

Hata ukisajili mtandao mmoja laini zaidi ya moja, HAIKATAI, INAKUBALI.

Naona bado kuna tatizo
Kwa nionavyo mimi... Mkurugenzi wa NIDA lazima ni mtu wa karibu sana na Mh. Rais maana sijawahi kuona akiwa na uvumilivu kwa watu wazembe kama huyu mkurugenzi wa NIDA. Yaani mtu miaka mitatu mtu huna hata namba?? /na ukiwa na namba basi details zimekosewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom