NIDA kuanzia mwezi huu wataanza kutoza fedha Taasisi zote za Umma na Binafsi ambazo zinatumia taarifa za Mamlaka hiyo kuhudumia Wananchi

Hapa inatakiwa kuwa specific, mnaweza jikuta hamuzitozi taasisi hizo badala yake mkahamisha mzigo kwa wananchi. Hizo taasisi zipewe Utaratibu kuwa wait ndio watatozwa sio wateja wao
 
Hapa inatakiwa kuwa specific, mnaweza jikuta hamuzitozi taasisi hizo badala yake mkahamisha mzigo kwa wananchi. Hizo taasisi zipewe Utaratibu kuwa wait ndio watatozwa sio wateja wao
 
Sisi tunawapa NIDA taarifa zetu bure, alafu wao wanatuuzia taarifa zetu tulizowapa bure ili tupate huduma
 
Kimsingi NIDA wanaleta tamaa ya kuvuna wasipo panda.

Wao kutunza taarifa zetu haifanyi kuwe na sababu ya kuziuza hizo taarifa pale ambapo mimi nakuwa ni sehemu ya unufaikaji.

Hizo taasisi nyingine hazijawa kushindwa kujiendesha kisa wanakosa taarifa za nida.

Suala la nida ni moja ya ajenda za kiusalama kwa nchi yetu ya kuwa na taarifa za raia wake wote ( kwa sasa ni wale above 18yrs)

Hivyo taasisi nyingine kutumia taarifa hizo haipaswi kuwa gharama kwao,kwani ndizo mhusika anaweza kuzitoa mwenyewe ili afanikishe jambo flani.

Mfano naenda kufungua akaunti benki ili kuendeleza mfumo rasmi wa fedha..maana si zuiwi kuweka fedha ndani.
 
Hili wazo umetuwakilisha wengi, nilikuwa nawaza kuandika hoja inayofanana na hii.
Keywords ni KUTOA HUDUMA siyo kila kitu BIASHARA.
Kwani tunalipa kodi kwa kazi gani ikiwa kila huduma ya serikali iwe ya kulipia? Maana mwisho wa siku gharama hizi tutakuja kutozwa wananchi.
Taasisi za umma zimejivika joho la wakusanya mapato badala ya watoa huduma.

Hii siyo sawa hata kidogo hizo gharama zitamshukia mtumiaji wa huduma moja kwa moja badala ya watoa huduma wanaohitaji hizo taarifa za NIDA
 
Nami nitahitaji malipo ili kutoa taarifa zangu NIDA kama taarifa ninazo zitoa zinaweza kugeuzwa Biashara kwa makampuni Basi nami nilipwe pacent ya usumbufu kuwe na Huduma kutoka NIDA itwayo NIDA gawio
 
Kama ni hivyo NIDA pia watulipe kwa "kuuza" taarifa zetu kwa watu wengine? Kwa nini wanataka kufanyia biashara taatifa zetu?

hapana hawauzi ila hii inakurahisishia na kukusaidia usipoteze mda mwingi, mfano ukienda sehem yoyote ambapo wanataka taarifa zako unaweka tu kidole kwenye machine na umemaliza, hii itasaidia mambo mengi sana! other wise kila sehem utaenda itakubidi ujaze form tatizo watu wengi kila kitu wanakipokea kwa upande wa negative badala ya kuangalia faida watakayopata! hivi ndoo vitu vinasave mda na sehem nyingi tu mbna wanaitumia hii huduma ikiwemo usajili wa laini ya simu na sehem zingine nyingi bado ztawekewa hii huduma unalipia 500 tu kwa taarifa: ukielewa kwamba time is money huezi lalamika
 
Yaani kuna mtu hapo NIDA, aliamka asubuhi, akaenda toilet, akakata gogo, akarudi chumbani akapiga mswaki, akaoga, akavaa, akanywa kifungua kinywa, akaingia kwenye gari, akaingia main road, akaanza safari ya kuja mjini, kwenye ofisi za NIDA, kisha anafika ofisini, anaanza kuzungumza mambo kama haya, kweli jamani?!
 
Wapuuzi sana hao NIDA...


Shughuli ya Vitambulisho Imewatoa kamasii..Hovyo Kabisa.


Uwezo Mdogo sana Watendaji Wa NIDA.


Hii Nchi inaudhi sana,Ukianza kufatilia Taasisi zake..
 
MAMLAKA ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), imesema kuwa kuanzia mwezi huu wataanza kutoza fedha taasisi zote za umma na binafsi ambazo zinatumia taarifa za mamlaka hiyo kuhudumia wananchi

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa NIDA, Geofrey Tengeneza wakati akizungumza na The Guardian Digital

“Kuna wadau ambao wanatumia taarifa zetu kutoa huduma kwa wananchi napenda niwajulishe kuwa kuanzia mwezi huu (Julai, 2020) tunaanza kutoza tozo kwa taasisi zote za umma na binafsi ambazo zinatumia taarifa zetu kuhudumia wananchi mbalimbali”amesema Tengeneza na kuongeza kuwa;

“Kwa mfano makampuni ya simu, NSSF, Bima ya Afya, mabenki na wadau wengine mbalimbali ambao hili waweze kutoa huduma kwa wateja wao wanahitaji kupata taarifa kutoka kwetu ni lazima kuzilipia ili kuendelea kutoa huduma hiyo”amesema

Ameongeza kuwa taasisi hizo zinapaswa kuingia mkataba na NIDA ili kuweza kupata huduma hizo vinginevyo taasisi ambazo zitashindwa kutimiza matakwa hayo watasitisha huduma hiyo mara moja

Ameongeza kuwa tayari wametoa notisi kwa kampuni ambazo azijaingia mkataba na NIDA kufanya hivyo mpaka Julai 31, 2020 na kwa ambazo zitashindwa watasitisha huduma.

“Kampuni 17 tayari tumewatumia notisi kuanzia Agosti Mosi kama watakuwa hawajaleta maombi kwetu ili kuwapatia mkataba tutawakatia huduma pia tunaendelea kufanya upembuzi kujua ni makampuni gani wanatumia huduma zetu,”amesema

Amesema kuwa kwa hatua ya awali wanategemea kuingia mkataba na watumia taarifa za NIDA zaidi makampuni na taasisi 86.

Amesema kuwa utaratibu huo ni maelekezo kutoka kwa Serikali yalioelekeza NIDA kuanza kujitegemea kukusanya fedha kutumia utaratibu huo ili kuondokana na utaratibu wa kupata fedha za matumizi kutoka serikalini.

“Mpaka sasa kampuni 65 zimeleta maombi ya kusaini mkataba na pia tumepeleka mikataba kwa kampuni 36 bado hawajarudisha, pia makampuni 18 wamerudisha mikataba na 12 kati yao tayari tushasaini nao mkataba”amesema
Na mwananchi ambaye ndiye chanzo cha taarifa hizo mnamlipaje? Maana bila mimi taarifa zangu hamuwezi kuzipata. Sasa naona mnataka kupiga hela kupitia mgongo wa mwananchi.

Nilisiki sikia kuwa card za nida zinaweza kutunza pesa sijui ukweli wa hili, ila kama ni kweli basi ningependa hizo pesa ziwe zinaingia kwenye accaunt ya mwanainchi.
 
Kwan serikali haiwapi ruzuku ya kuendesha shughuli zao
Final consumer ndio anapata mzigo wote huu
Nadhan kwa kuwa NIDA ni non profit oriented wange tazama swala hili tena
 
Wanaanzisha taasisi kwa sababu ya kusimamia shughuli fulani zoezi likiisha hiyo taasisi inajikuta aina source of income, matokeo yake ili ibaki inabidi waanzishe tozo ambazo zina trickle down mpaka kwa mlaji.
 
NIDA siku sio nyingi litakuwa shirika la umma (SU), naona chanzo cha mapato wameisha pata bado tu sheria kutungwa lipewe mamlaka rasmi
 
Back
Top Bottom