NICOL iwezeshwe iagize mafuta ili kuokoa upungufu wa mafuta

Godwine

JF-Expert Member
Jan 15, 2010
1,371
281
kutokana na makampuni ya kuagiza mafuta kusita na kuendelea kutunishiana misuli na serikali , nadhani itakuwa ni busara kwa serikali kuikopesha NICOL shilingi bil 23 ambayo ni sawa na hisa za kampuni hii ndani ya banki ya NMB (6%) , jambo ili litawawezesha wananchi kuingia na kushika biashara ya mafuta na serikali kuwa salama.

kutokana na kampuni hii kuingia kwenye soka la biashara ya mafuta itawezesha kuboresha usalama wa nchi kwani mafuta ni bidhaa muhimu na wageni wameanza kuitumia kama zana za kuiteketeza serikali yetu.

lazima serikali sasa ianze kufikiri mbali na kuanza kuyawezesha makampuni ya kizalendo kushika uchumi wa nchi na kuacha kutegemea wageni kwani kwa hali ya uchumi wa sasa wa dunia , makampuni makubwa yameanza kuziyumbisha na kuzipindua nchi mbali mbali kwa sera za uchumi na udhibiti wa bidhaa na kusababisha mfumuko mkubwa wa bei na kusababisha maandamano ya wananchi na kudondoshwa kwa serikali hizo
 
hivi nicol si ndio wale walishindwa kusimamia miradi waliyoiazisha na kutia hasara mtaji wa wawekezaji wao?nadhani hata kwenye soko la hisa walisimamishwa,kama nimewachanganya na kampuni nyingine natanguliza samahani.
lakini kwa maoni yangu kama hizo bilioni zipo kwanini wasipewe TPDC waagize hayo mafuta kama ilivyowahi kupendekezwa na bunge?
 
nicol wafanye hiyo kazi afu tpdc wafanye nini? na tpdc waliomba kufanya hii,manake wamebakia kusindikiza tu explorers!
 
hivi nicol si ndio wale walishindwa kusimamia miradi waliyoiazisha na kutia hasara mtaji wa wawekezaji wao?nadhani hata kwenye soko la hisa walisimamishwa,kama nimewachanganya na kampuni nyingine natanguliza samahani.
lakini kwa maoni yangu kama hizo bilioni zipo kwanini wasipewe TPDC waagize hayo mafuta kama ilivyowahi kupendekezwa na bunge?

NICOL walishindwa kuwekeza mtaji wao kwenye biashara salama ,lakini ninachopendekeza mimi hakitakuwa na madhara kwa serikali na kwa nicol na wanahisa wake kwani kama serikali wakiipa sh bil 23 na kukalia hisa za nicol ambazo ni asilimia sita 6% HISA za NMB wakishindwa inamaana hisa hizi zitatumika kuziba pengo la fedha za serikali pia fedha hizi ziwe kama stimulas package kwa kampuni hii ili iweze kurudi kwenye nafasi yake ya kawaida
 
nicol wafanye hiyo kazi afu tpdc wafanye nini? na tpdc waliomba kufanya hii,manake wamebakia kusindikiza tu explorers!
wafanye kwa ubia na nicol kwani nicol ni kampuni ya kizalendo ambayo inaweza shirikiana na taasisi ya serikali
 
TPDC should solely monopolize the impotrtation of petrol and its products.
The forgotten Transport Equalization Fund could be revived this way in order to have a pricing mechanism that is uniform all over Tz - siyo hii biashara uria.
 
NICOL walishindwa kuwekeza mtaji wao kwenye biashara salama ,lakini ninachopendekeza mimi hakitakuwa na madhara kwa serikali na kwa nicol na wanahisa wake kwani kama serikali wakiipa sh bil 23 na kukalia hisa za nicol ambazo ni asilimia sita 6% HISA za NMB wakishindwa inamaana hisa hizi zitatumika kuziba pengo la fedha za serikali pia fedha hizi ziwe kama stimulas package kwa kampuni hii ili iweze kurudi kwenye nafasi yake ya kawaida

so waliproove failure na katika miaka yote hiyo wamekaa kimya hawatoi hata tathmini ya biashara afu tuwape tena nyingine, yaani kweli wabongo hatujifunzi, ndio maana mtuhumiwa wa ufisadi ana kesi mahakama kuu lakini bado taasisi nyingine ya serikali (ileile iliyompeleka mahakamani) inampa tenda mtu huyo ya kuagiza matrekta ya kilimo kwanza
 
Duh!
Kweli kuna watu wabishi,Zaidi ya Hizo Hisa za NMB , unaweza ukatuambia mafanikio mengine ya NICOL?
Je ni niniThamani na mwendo wa hisa zao?
 
TPDC should solely monopolize the impotrtation of petrol and its products.
The forgotten Transport Equalization Fund could be revived this way in order to have a pricing mechanism that is uniform all over Tz - siyo hii biashara uria.

ata kama TPDC wakiagiza wao wenyewe tatizo litakuwa kwenye usamabazaji nao utasababisha utofauti wa bei, pia si busara kwa taasisi moja kuleta ukilitimba wa uagizaji na usambazaji bali kama shirika hili kwa kushirikiana na nicol wakijiingiza kwenye uagizaji kutakuwa na mafuta ya ziada na hivyo kutaondoa upungufu ambao ni chanzo cha kupanda kwa bei, pia wote tunajua mashirika ya kiserikali yanavyokuwa kama hakutakuwa na share na private sector , tulikuwa na TIPPER ambayo wajanja wachache wameiua
 
so waliproove failure na katika miaka yote hiyo wamekaa kimya hawatoi hata tathmini ya biashara afu tuwape tena nyingine, yaani kweli wabongo hatujifunzi, ndio maana mtuhumiwa wa ufisadi ana kesi mahakama kuu lakini bado taasisi nyingine ya serikali (ileile iliyompeleka mahakamani) inampa tenda mtu huyo ya kuagiza matrekta ya kilimo kwanza
unajua wakati mwingine matatizo ni yetu sisi watanzania , kwa mfano nadhani wewe ni miongoni mwa wanahisa wa nicol lakini kama utawala wa nicol haufanyi kazi ipasavyo ungeweza kupeleka hoja kwenye mkutano mkuu na kuuondoa utawala uo na wewe kama kijana kuingia kwenye nafasi ya uongozi na kuleta mabadiliko.

nitasikitika sana kusikia wanachama wa nicol wanalia kuhusu uendeshwaji mbaya wa kampuni hii wakati kwa utafiti wangu nimegundua ndani ya nicol kuna takribani wahitimu wa vyuo vikuu 3000 tena wengine kwenye fani za biashara na mainjinia sasa mnangoja nani aje awakuzie kampuni yenu zaidi ya nyinyi kuchukua ngazi na kuonyesha mfano kwa jamii kuwa kama kampuni ikilegalega nini cha kufanya.

kuhusu mtaji nicol ina share 6% ya NMB ambayo ni takribani shs bil 23 , kwanini mnashindwa kuleta mfano mwema kwa kizazi chetu, nadhani kwa mtaji huu mnaweza ata kuanzisha benki na kuajiri watu wengi ndani ya kampuni hii


msitumie muda mwingi kulalamika ni wakati wa vitendo , fanyeni sasa nasi tuige
 
Duh!
Kweli kuna watu wabishi,Zaidi ya Hizo Hisa za NMB , unaweza ukatuambia mafanikio mengine ya NICOL?
Je ni niniThamani na mwendo wa hisa zao?

NMB inathamani ya takribani bil 380 sasa asilimia sita 6% ni kama sh bil 22.8 hii ni takwimu ya mwezi wa pili
 
NICOL kwa sasa ipo kaburini inasubiri kufukiwa tu
Nashangaa saana wakina Idd Simba, Sara Masasi, Mengi, Felix Mosha, Bomani na wale wote waliotushawishi tukanunua hisa, ilikula kwetu

someni hii habari hapa

Two months after being delisted from the Dar es Salaam bourse over financial misconduct, embattled National Investment Company Limited (Nicol) is now asking the High Court to lift an order that froze its bank accounts to save the company from total collapse.

The public company, which faces expulsion from its Raha Tower Building offices over failure to pay $ 42,000 (about Sh63 million) rent, is pleading with the court to quash a decision by the Capital Markets and Securities Authority (CMSA) to block the sale of its shares in the National Microfinance Bank (NMB) for investment.

Its landlord has asked the company to vacate the premises by August 21 if by then the debt is not paid.
The filing of the suit comes five months after CMSA wrote to CRDB, NMB and Exim banks instructing them to block any cash outflows from its accounts to protect the interests of Nicol investors.

Nicol says the freezing of its bank accounts has halted its operations and that it is likely to sink into more trouble if the orders which would enable it to meet its urgent financial obligations are not granted.

The company argues that the attachment of its accounts violated Section 22 of the CMSA Act which stated that such bank accounts may be attached only if they are related to proceeds actually involved in violation of any of the provisions of CMSA Act.

CMSA had, between December 2010 and January this year, carried out investigations into activities by Nicol and uncovered massive irregularities, including failure to maintain proper accounts.

The authority then suspended its board of directors and chairman Felix Mosha and ordered the company to convene an annual general meeting. The company was also scrapped from the Dar es Salaam Stock Exchange (DSE) after it failed to tell its shareholders that a pharmaceutical company in which it has a 51 per cent stake was put into receivership late last year.

Source; Citizen
 
unajua wakati mwingine matatizo ni yetu sisi watanzania , kwa mfano nadhani wewe ni miongoni mwa wanahisa wa nicol lakini kama utawala wa nicol haufanyi kazi ipasavyo ungeweza kupeleka hoja kwenye mkutano mkuu na kuuondoa utawala uo na wewe kama kijana kuingia kwenye nafasi ya uongozi na kuleta mabadiliko.

nitasikitika sana kusikia wanachama wa nicol wanalia kuhusu uendeshwaji mbaya wa kampuni hii wakati kwa utafiti wangu nimegundua ndani ya nicol kuna takribani wahitimu wa vyuo vikuu 3000 tena wengine kwenye fani za biashara na mainjinia sasa mnangoja nani aje awakuzie kampuni yenu zaidi ya nyinyi kuchukua ngazi na kuonyesha mfano kwa jamii kuwa kama kampuni ikilegalega nini cha kufanya.

kuhusu mtaji nicol ina share 6% ya NMB ambayo ni takribani shs bil 23 , kwanini mnashindwa kuleta mfano mwema kwa kizazi chetu, nadhani kwa mtaji huu mnaweza ata kuanzisha benki na kuajiri watu wengi ndani ya kampuni hii


msitumie muda mwingi kulalamika ni wakati wa vitendo , fanyeni sasa nasi tuige
Matatizo makubwa zaidi ya watanzania ni kufikiri wewe utawekeza bila kufanta kazi.
NICOL imekufa hilo kalina ubishi.
Kwa upande mwingine ni wewe GODWINE kuchukua hii kama oppurtunity ya kufanya kile unachoeleza , kuagiza mafuta kama mtu binafsi.
Mbona wengine wanafanya, tena kwa faida kubwa.Hivyo tusitegemee kuendelea kiuchumi kwa kupitia mgongo wa watu wengine bila sisis kufanya kazi.
 
NICOL inakaribia kufa Godwine wazo lako sikubaliani nalo hasa kwakuwa serikali ikiwakopesha NICOL ni kama inachukua pesa na kuzitia into a "sinking fund". Pengine ungelipendekeza shirika jengine au wazalendo wakopeshwe kuanzisha makampuni ya kuagiza mafuta. Tatizo la mafuta nchini linatokana na kukosekana kwa mamlaka ya kulinda watumiaji mafuta na monopolisation ya makampuni ya mafuta kwa kutumia umoja wao wa waagizaji mafuta. Ili kuvunja hii monopolisation lirudishwe shirika la TPDC ambalo litakuwa linaagiza mafuta lenyewe na kusambaza lenyewe kwa wauzaji wanaotaka kuuza mafuta nchini.

Huo umoja una nguvu sasa hivi kwa kuwa hakuna muagizaji mwengine wa mafuta nchini, na wamekuwa wakilobby kuzuia shirika la TPDC lisianzishwa na mradi wa Bulk procurement usianze. Serikali ikiwa na mkono wa uagizaji na usambazi nguvu ya umoja huu itakufa na watabakia wauzaji mafuta nchini. USA ndio wanavyofanya na wameweza kucontrol vizuri bei za mafuta nchini mwao na sie tufanye hivyo ili kuwadhibiti hawa wezi wanaotumia migongo yetu kujipatia supernormal profit kwasababu tu hatujui bei gani wananunua mafuta yao.

Pia ianzishwe mamlaka ya kulinda watumiaji wa huduma mbali mbali (Consumer Protection Bureau) na wapewe meno ya kuwashitaki na kuwadai fidia wale wote wanaolangua bidhaa zao au kutumia udanganyifu kufanya biashara. Consumer Protection Bureau ni kitu nimekuwa nakipigia kelele tangu mwaka juzi kuwa kitatusaidia sisi watumiaji dhidi ya wauzaji wasio na imani na tamaa ya kutajirika haraka. Lazima wauzaji wadhibitiwe ama sivyo matokeo yake ni kama haya sasa. Pia wanaathiri na uchumi wa nchi.
 
TPDC iagize mafuta,bei ikiwa poa zaidi ya wengine,retailers watanunua na kusambaza.....it's all about who sells what at what price.Let the govt compete with private sector.
 
@majoja

kwa upande wangu nimetumia muda wangu mwingi kutenda kuliko kalalamika na nadhani kwa mwenendo wangu si mbaya lakini tambua kuna kitu wanakiita specilization(base on core activities) kwa hiyo kitendo cha kuachana na shughuli unazozifanya na kurukia zingine husababisha usumbufu wa namna fulani.

lakini kwa nicol na wengine ambao hawajachagua cha kufanya nadhani ni miongoni mwa fulsa mzuri kuingia kwenye sector hii, kwani risk yake ni ndogo kulinganisha na biashara zingine.

nitasikitika kama jamii hasa wanachama wa nicol ninawaona wanaendelea kukata tamaa na kupoteza lengo la biashara na kudhani mtaji wao umezama na kuishia kulalamika tu.


hakika taifa ili linaelekea pabaya kama tukiacha biashara ya mafuta mikononi mwa wageni kwani kadri siku zinapoenda ndio kaburi la nchi hii linaendelea kukamilika,

ni wakati wa kila mtanzania na kila kampuni ya kizalendo kuhakikisha ya kuwa biashara ya mafuta inakuwa mikononi taifa na wazalendo la sivyo tungoje, machafuko na mfumuko wa bei wa kutisha
 
habari ya uhakika TPDC wameshaonywa wasiingilie biashara ya mafuta kwani makampuni ya mafuta kwa sasa ni ya waheshimiwa mafisadi!hivyo wao waangalie gesi tuu na utafiti wa mafuta!
 
@majoja

kwa upande wangu nimetumia muda wangu mwingi kutenda kuliko kalalamika na nadhani kwa mwenendo wangu si mbaya lakini tambua kuna kitu wanakiita specilization(base on core activities) kwa hiyo kitendo cha kuachana na shughuli unazozifanya na kurukia zingine husababisha usumbufu wa namna fulani.

lakini kwa nicol na wengine ambao hawajachagua cha kufanya nadhani ni miongoni mwa fulsa mzuri kuingia kwenye sector hii, kwani risk yake ni ndogo kulinganisha na biashara zingine.

nitasikitika kama jamii hasa wanachama wa nicol ninawaona wanaendelea kukata tamaa na kupoteza lengo la biashara na kudhani mtaji wao umezama na kuishia kulalamika tu.


hakika taifa ili linaelekea pabaya kama tukiacha biashara ya mafuta mikononi mwa wageni kwani kadri siku zinapoenda ndio kaburi la nchi hii linaendelea kukamilika,

ni wakati wa kila mtanzania na kila kampuni ya kizalendo kuhakikisha ya kuwa biashara ya mafuta inakuwa mikononi taifa na wazalendo la sivyo tungoje, machafuko na mfumuko wa bei wa kutisha
Why NICOL?
 
Back
Top Bottom