drphone
JF-Expert Member
- Sep 29, 2009
- 3,542
- 281
wakuu nimepatwa na tatizo nilimpeleka mdogo wangu shule hizi zinazoanziwa na majina ya st.(mtakatifu) mwezi wa pili mwanzoni kabisa kwavile alichelewa wakanishauri nilipe special tuition 100000 kwa miezi sita nikalipa nikawaleza tatizo la mtt kuja huku kutoka mkoani ni hali ya hewa dr akashauri aje dar kwa vile kunajoto, wiki yakwanza mtt akasumbuliwa na kichwa akamwambia matroni nahisi nina malaria matroni akamwambia hapana utakuwa na pumu wakabishana sana matroni akamlazimisha kumpa dawa ya pumu baada ya siku 2 hali ikawa mbaya wakanipigia nikaenda kumchukua mtt akanieleza kichotokea nikampima akawa na malaria alivyomaliza dawa ikamrudisha kuwauliza matroni kwann wamemfanyia mtt hivyo ikawa kosa na bifu na mtt na mm pia, baada ya wiki tena mtt akaanguka baada ya kuishiwa nguvu nikapigiwa nikamfata akanieleza walikuwa awataki kumpa dawa na wamemchukia eti anawachongea ukweli lilinipain nikamweleza mkuu wa shule lakini aikusaidia nilipomrudisha mtt siku hiyo hiyo alichofanya alitoroka na watt wa day akarudi om analia ucku nilipomwoji aliniambia kaka mm sirudi tena ile shule nilipomwoji ndio akanieleza yanoyoendelea pale nikachoka ni mengi sana nilichofanya nikamwambia atulie nikawa nasubiria shule wanitaarifu mtt yuko wapi tangu j3 hadi ijumaa kmya j5 nikapiga cm wakaniambia mtt yupo anaendelea vzuri nikakasirika sana ijumaa ndio nikamtafuta mwenye shule mwenyewe nikamtaarifu ndio akawapigia shule ndio wanastuka mtt hayupo shule nilichofanya niliwaambia nataka ada yangu nimtafutie mtt shule naona wananizingua ktk hilo jamani niwafanyaje?