Red Giant
JF-Expert Member
- Mar 9, 2012
- 15,658
- 20,883
KIONGOZI (nimeonelea ndiyo iwe title)
Sasa kitabu hiki kinapatikana ndani ya maktaba app (by pictuss). Inapatikana playstore.
Kimeandikwa na: Niccolo Machiaveli, 1513.
Kimetafsiriwa na: Pictuss, 2021.
Email: Pictuspublishers@gmail.com.
©Pictuss2021
Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu yoyote ya tafsiri hii inayoweza kunakiliwa, kutolewa kivuli(photocopy), kuhamishwa, kurekodiwa au kutolewa kwa namna yoyote ile bila ya taarifa ya awali ya kimaandishi kutoka kwa mmiliki.
Kwa mtukufu Lorenzo Di Piero De' Medici
Ni desturi kwa wale wanaotaka kujipendekeza kwa viongozi kumpatia zawadi ya vitu wanavyovithamini sana. Wanaamini kuwa naye atavithamini. Hivyo tumekuwa tukitumia farasi, mavazi ya vita, nguo za dhahabu, vito na zawadi nyingine za gharama zinazostahili kupewa viongozi.
Kwa kufuata desturi hiyo, nimekuja mbele zako kutoa zawadi. Lakini katika mali zangu sijaona kitu cha thamani kama ujuzi wa matendo ya watu hodari. Maarifa niliyoyapata kwa uzoefu wangu juu ya mambo ya sasa, na kwa kusoma historia ya kale. Maarifa ambayo nimeyachunguza na kuyachuja, na kisha kuzalisha kitabu hiki kidogo. Nakutumia kitabu hicho ewe mtukufu, japo naona kazi hii hailingani na utukufu wako. Lakini natarajia rehema zako zitakufanya ukipokee, hasa ukizingatia kuwa nakupatia njia ya kuelewa kwa muda mfupi yale niliyo jifunza kwa muda wa miaka mingi, chini taabu na hatari.
Kazi hii sijaipamba kwa lugha nzuri na madoido mengine kama ilivyo desturi ya waandishi wengi. Ni bora nisijipatie sifa lakini ukweli wa mambo wa suala hili uwe wazi.
Ni sidhani kama nitakuwa najikweza kwa mtu wa chini kama mimi, kuanza kuzungumza habari za namna ya utawala. Sababu ni kuwa; wale wanaochora ramani ya nchi hukaa mabondeni ili kupata ramani ya milima, na hukaa juu milimani ili kupata muonekano mzuri wa mabonde. Kwa namna hiyohiyo, ili mtu awajue watu vizuri, anapaswa kuwa kiongozi, na ili kuwajua viongozi vizuri, anapaswa kuwa mtu wa kawaida.
Hivyo basi, nakuomba ewe mtukufu upokee zawadi hii ndogo ninayoitoa kwa nia njema. Kama ukikisoma kwa bidii utagundua nia yangu ya kutaka ufikie ukuu unaostahili uwezo na fursa ulizonazo. Na iwapo katika kilele cha ukuu wakoutaangalia pande hizi za chini, utaelewa ni jinsi gani, sikustahili lakini nilivumilia ukatili usiokoma wa bahati mbaya.
SURA YA 1
KUHUSU AINA MBALIMBALI YA UTAWALA NA JINSI ZINAVYOSIMAMA
Kuna aina mbili tu ya Serikali ambazo watu wametawaliwa nazo na wanaendelea kutawaliwa. Serikali za kifalme au jamuhuri. Ufalme unaweza kuwa wa kurithi kutokana na uhusiano wa damu na wafalme waliopita au unaweza kuwa ni ufalme mpya kabisa. Ufalme mpya, unaweza kuwa mpya kabisa kama ule wa Milan chini ya Francesco Sforza, au unaweza kuwa ni muendelezo wa mfalme aliyeteka kama ulivyokuwa ufalme wa Napoli chini ya wafalme wa Hispania.
Nchi iliyotekwa inaweza kuwa ilikuwa chini ya mfalme au ilikuwa huru bila mfalme. Anayeteka nchi anaweza fanya hivyo kwa nguvu zake mwenyewe au kwa kutumia nguvu za wengine. Kwa bahati njema au kwa uwezo wake.
SURA YA 2
UFALME WA KURITHI
Sitaongelea kuhusu jamhuri, kwa sababu jambo hilo nimeshaliongelea kwa kirefu sehemu nyingine. Mimi nitaongelea tawala za kifalme tu. Nitaongelea jinsi ya kuongoza tawala za kifalme.
Ufalme unaotokana na kurithi ni rahisi kuongoza kuliko ufalme mpya, kwa sababu wananchi wanakuwa wameizoea familia ya kifalme. Kinachotakiwa ni kiongozi mpya kutokengeuka kutoka katika njia za watangulizi mababu zake.
Kwa hiyo, hata kama kiongozi ana uwezo wa kawaida hatapata taabu kuongoza labda akutane na magumu ambayo ni ngumu kuyashinda. Na hata ikitokea kang'olewa madarakani kwa uasi, ni rahisi kwake kurudi mara tu mambo yanapowaendea vibaya waasi/wahaini hao.
Katika Italia tuna mfano mzuri wa jambo hili kutoka kwa Duke wa Ferrara. Duke huyu asingeweza kuhimili mashambulizi ya wavenice ya mwaka 1484, wala yale ya Papa Julius wa II ya mwaka 1510 Iwapo mamlaka yake isingekuwa imara. Isipokuwa amefanya matendo mabaya kupita kiasi; kiongozi anayetokana na kurithi ana mambo machahe yanayoweza kumfanya kuwa chukizo, na maudhi kwa watu wake. Na zaidi ni kuwa, muendelezo wa utawala wake ambao upo tokea enzi za mababu zake, utafanya watu kutojali sana mabadiliko yoyote yanayoweza kutokea. Na mara zote badiliko moja huzaa nafasi kwaajili ya jingine.
Sasa kitabu hiki kinapatikana ndani ya maktaba app (by pictuss). Inapatikana playstore.
Kimeandikwa na: Niccolo Machiaveli, 1513.
Kimetafsiriwa na: Pictuss, 2021.
Email: Pictuspublishers@gmail.com.
©Pictuss2021
Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu yoyote ya tafsiri hii inayoweza kunakiliwa, kutolewa kivuli(photocopy), kuhamishwa, kurekodiwa au kutolewa kwa namna yoyote ile bila ya taarifa ya awali ya kimaandishi kutoka kwa mmiliki.
Kwa mtukufu Lorenzo Di Piero De' Medici
Ni desturi kwa wale wanaotaka kujipendekeza kwa viongozi kumpatia zawadi ya vitu wanavyovithamini sana. Wanaamini kuwa naye atavithamini. Hivyo tumekuwa tukitumia farasi, mavazi ya vita, nguo za dhahabu, vito na zawadi nyingine za gharama zinazostahili kupewa viongozi.
Kwa kufuata desturi hiyo, nimekuja mbele zako kutoa zawadi. Lakini katika mali zangu sijaona kitu cha thamani kama ujuzi wa matendo ya watu hodari. Maarifa niliyoyapata kwa uzoefu wangu juu ya mambo ya sasa, na kwa kusoma historia ya kale. Maarifa ambayo nimeyachunguza na kuyachuja, na kisha kuzalisha kitabu hiki kidogo. Nakutumia kitabu hicho ewe mtukufu, japo naona kazi hii hailingani na utukufu wako. Lakini natarajia rehema zako zitakufanya ukipokee, hasa ukizingatia kuwa nakupatia njia ya kuelewa kwa muda mfupi yale niliyo jifunza kwa muda wa miaka mingi, chini taabu na hatari.
Kazi hii sijaipamba kwa lugha nzuri na madoido mengine kama ilivyo desturi ya waandishi wengi. Ni bora nisijipatie sifa lakini ukweli wa mambo wa suala hili uwe wazi.
Ni sidhani kama nitakuwa najikweza kwa mtu wa chini kama mimi, kuanza kuzungumza habari za namna ya utawala. Sababu ni kuwa; wale wanaochora ramani ya nchi hukaa mabondeni ili kupata ramani ya milima, na hukaa juu milimani ili kupata muonekano mzuri wa mabonde. Kwa namna hiyohiyo, ili mtu awajue watu vizuri, anapaswa kuwa kiongozi, na ili kuwajua viongozi vizuri, anapaswa kuwa mtu wa kawaida.
Hivyo basi, nakuomba ewe mtukufu upokee zawadi hii ndogo ninayoitoa kwa nia njema. Kama ukikisoma kwa bidii utagundua nia yangu ya kutaka ufikie ukuu unaostahili uwezo na fursa ulizonazo. Na iwapo katika kilele cha ukuu wakoutaangalia pande hizi za chini, utaelewa ni jinsi gani, sikustahili lakini nilivumilia ukatili usiokoma wa bahati mbaya.
SURA YA 1
KUHUSU AINA MBALIMBALI YA UTAWALA NA JINSI ZINAVYOSIMAMA
Kuna aina mbili tu ya Serikali ambazo watu wametawaliwa nazo na wanaendelea kutawaliwa. Serikali za kifalme au jamuhuri. Ufalme unaweza kuwa wa kurithi kutokana na uhusiano wa damu na wafalme waliopita au unaweza kuwa ni ufalme mpya kabisa. Ufalme mpya, unaweza kuwa mpya kabisa kama ule wa Milan chini ya Francesco Sforza, au unaweza kuwa ni muendelezo wa mfalme aliyeteka kama ulivyokuwa ufalme wa Napoli chini ya wafalme wa Hispania.
Nchi iliyotekwa inaweza kuwa ilikuwa chini ya mfalme au ilikuwa huru bila mfalme. Anayeteka nchi anaweza fanya hivyo kwa nguvu zake mwenyewe au kwa kutumia nguvu za wengine. Kwa bahati njema au kwa uwezo wake.
SURA YA 2
UFALME WA KURITHI
Sitaongelea kuhusu jamhuri, kwa sababu jambo hilo nimeshaliongelea kwa kirefu sehemu nyingine. Mimi nitaongelea tawala za kifalme tu. Nitaongelea jinsi ya kuongoza tawala za kifalme.
Ufalme unaotokana na kurithi ni rahisi kuongoza kuliko ufalme mpya, kwa sababu wananchi wanakuwa wameizoea familia ya kifalme. Kinachotakiwa ni kiongozi mpya kutokengeuka kutoka katika njia za watangulizi mababu zake.
Kwa hiyo, hata kama kiongozi ana uwezo wa kawaida hatapata taabu kuongoza labda akutane na magumu ambayo ni ngumu kuyashinda. Na hata ikitokea kang'olewa madarakani kwa uasi, ni rahisi kwake kurudi mara tu mambo yanapowaendea vibaya waasi/wahaini hao.
Katika Italia tuna mfano mzuri wa jambo hili kutoka kwa Duke wa Ferrara. Duke huyu asingeweza kuhimili mashambulizi ya wavenice ya mwaka 1484, wala yale ya Papa Julius wa II ya mwaka 1510 Iwapo mamlaka yake isingekuwa imara. Isipokuwa amefanya matendo mabaya kupita kiasi; kiongozi anayetokana na kurithi ana mambo machahe yanayoweza kumfanya kuwa chukizo, na maudhi kwa watu wake. Na zaidi ni kuwa, muendelezo wa utawala wake ambao upo tokea enzi za mababu zake, utafanya watu kutojali sana mabadiliko yoyote yanayoweza kutokea. Na mara zote badiliko moja huzaa nafasi kwaajili ya jingine.