Red Giant
JF-Expert Member
- Mar 9, 2012
- 15,658
- 20,887
- Thread starter
- #21
SURA YA 16
KUHUSU WEMA(UTOAJI) NA UKAUZU(UBAHILI)
Nianze kwa kuzungumzia hiyo sifa ya kwanza. Nasema kuwa, ni vizuri kujulikana kwa sifa ya utoaji, lakini utoaji bila kujulikana ni jambo lenye hasara. Japo kutoa ni kitu kizuri na kinachopaswa kufanywa, lakini kama haijulikani kuwa umetoa hautaweza kuepuka kuitwa bahili(kauzu).
Kwa hiyo, ukifanya jambo la utoaji, na ili dunia ikufahamu kwa sifa hiyo, inatakiwa kufanya hivyo kwa kujionyesha. Tofauti na hilo ni kuwa, kiongozi mwenye muelekeo wa utoaji, na ili kudumisha sifa hiyo, atatumia mali zake zote kufanya hivyo. Na atalazimika kuwatwisha watu wake mzigo mkubwa wa kodi, na baadaye atahamia kwenye kutaifisha mali za watu na kutafuta pesa kokote ziliko. Kufanya hivyo kutamfanya achukiwe na wananchi wake, na kwa kuwa amekuwa maskini sababu ya kutoa, wananchi wake watamdharau.
Kwa hiyo, kwa kuwa utoaji wake umewakasirisha wengi kwa kodi, na kuwanufaisha wachache, atajikuta kwenye hali mbaya kuliko alivyokuwa mwanzo. Zaidi ya hilo, atajikuta hatari alizojitahidi kuziepuka zipo mbele yake. Kwa kugundua hili, na baada ya kutafuta alipokosea, mara moja atageuka na kuwa bahili(kauzu).
Hivyo basi, kwa kuwa kiongozi hawezi kufanya wema ili ajulikane kwa sifa hiyo bila kujiletea matatizo, na kama ana busara, hatojali iwapo watu watamwita kauzu(bahili). Mtu wa aina hii, baada ya muda watu wataanza kumuona ni mwema zaidi. Pale ambapo kupitia ubahili wake anakuwa na pesa za kutosha kujilinda dhidi ya adui bila kuwapa mzigo wa kodi wananchi wake. Na zaidi ni kwamba, anafanya wema kwa raia wengi bila kuwaumiza kwa kodi huku akiwa na sifa ya ukauzu(ubahili) kwa wale ambao hawapatii kitu, na hawa ni wachache tu.
Katika nyakati zetu hatujaona viongozi wanaofanya mambo makubwa, isipokuwa wale wanaosifika kwa ukauzu. Wengine wote waliingia matatizoni. Papa Julius II baada ya kujinadi kuwa na sifa ya wema ili kupata upapa, hakufanya jitihada zozote za kuendelea na sifa hiyo alipokuwa vitani dhidi ya mfalme wa Ufaransa. Lakini aliendesha vita zake bila kutoza watu wake kodi yoyote, aligharamia vita kutoka katika akiba yake aliyokuwa ametumia muda mrefu kuitunza.
Kama mfalme wa sasa wa Hispania angekuwa na sifa ya wema, asingeweza kufanya na kufanikiwa katika mambo mengi aliyoyafanya.
Kwa hiyo, kama kiongozi anaweza kuepuka kupora mali za wananchi wake, kutofilisika, ameweza kujilinda na kuepuka kutodharaulika, hatakiwi kujali kupewa sifa ya ukauzu. Hiyo ni moja ya sifa inayomuwezesha kubaki madarakani.
Na mtu akipinga na kusema kuwa wema ulimfanya Kaisari kushika madaraka, na kuwa kuna wengine wengi waliopanda vyeo vikubwa kwa kuwa wema, nitajibu hivi; 'unaweza kuwa tayari ni kiongozi au unataka kuwa kiongozi, kama ni kiongozi, wema utakutia matatizoni, na kama unataka kuwa kiongozi ni muhimu watu wakuone ni mwema. Kaisari alikuwa anataka kuwa mtawala wa Roma, lakini baada ya kupata cheo hicho angeendelea na matendo yake ya wema, na utoaji bila kubana matumizi, himaya ya Roma ingeanguka.'
Mtu akiendelea kubisha kuwa, viongozi wengi waliosifika kuwa ni wema sana waliweza kufanya mambo makubwa kwa kutumia majeshi yao. Nitajibu hivi; kiongozi anaweza kutumia mali yake na ya wananchi wake, au ya watu wengine kabisa. Kama anatumia mali yake au ya wananchi wake, lazima awe makini katika matumizi. Lakini kama mali hizo ni za watu wengine hatakiwi kujibana katika kuzitumia kutenda wema. Sababu kiongozi anayeongoza jeshi lake yeye mwenyewe, na anayelihudumia kwa kupora wengine na michango ya lazima, huku akitumia mali zao apendavyo, hatakiwi kujibana katika kuhudumia jeshi lake.
Vinginevyo wanajeshi wake wataacha kumfuata.
Kitu ambacho si chako, wala si cha wananchi wako, unatakiwa kukigawa bila kujibana, kama tu walivyokuwa Cyrus, Kaisari na Alexander. Kugawa mali ya wengine hakukuharibii sifa bali kunaiimarisha zaidi. Kitu kitakachokuletea matatizo ni kutumia mali yako mwenyewe, na hakuna sifa inayomuangamiza mtu haraka kama ya kuwa mwema(mtoaji); kadri unavyoitenda, ndivyo unavyopoteza uwezo wa kuitenda. Hilo linakufanya uwe fukara na mtu wa kudharaulika, au labda kwa kuepuka ufukara uamue kuwa mporaji(ukichukua mali za raia wako kwa nguvu), jambo litakalokufanya uchukiwe. Utu wema husababisha moja kati ya hayo mambo mawili(kudharauliwa au kuchukiwa) na kiongozi anatakiwa kujilinda sana dhidi ya hizi sifa mbili.
Kinyume chake; ni jambo la busara kuvumilia kuitwa kauzu(bahili). Sifa hiyo huleta aibu lakini haikufanyi uchukiwe. Lakini tamaa ya kusifiwa kuwa ni mwema(mtoaji), hupelekea kuwa mporaji, na hilo husababisha uchukiwe na kudharaulika pia.
KUHUSU WEMA(UTOAJI) NA UKAUZU(UBAHILI)
Nianze kwa kuzungumzia hiyo sifa ya kwanza. Nasema kuwa, ni vizuri kujulikana kwa sifa ya utoaji, lakini utoaji bila kujulikana ni jambo lenye hasara. Japo kutoa ni kitu kizuri na kinachopaswa kufanywa, lakini kama haijulikani kuwa umetoa hautaweza kuepuka kuitwa bahili(kauzu).
Kwa hiyo, ukifanya jambo la utoaji, na ili dunia ikufahamu kwa sifa hiyo, inatakiwa kufanya hivyo kwa kujionyesha. Tofauti na hilo ni kuwa, kiongozi mwenye muelekeo wa utoaji, na ili kudumisha sifa hiyo, atatumia mali zake zote kufanya hivyo. Na atalazimika kuwatwisha watu wake mzigo mkubwa wa kodi, na baadaye atahamia kwenye kutaifisha mali za watu na kutafuta pesa kokote ziliko. Kufanya hivyo kutamfanya achukiwe na wananchi wake, na kwa kuwa amekuwa maskini sababu ya kutoa, wananchi wake watamdharau.
Kwa hiyo, kwa kuwa utoaji wake umewakasirisha wengi kwa kodi, na kuwanufaisha wachache, atajikuta kwenye hali mbaya kuliko alivyokuwa mwanzo. Zaidi ya hilo, atajikuta hatari alizojitahidi kuziepuka zipo mbele yake. Kwa kugundua hili, na baada ya kutafuta alipokosea, mara moja atageuka na kuwa bahili(kauzu).
Hivyo basi, kwa kuwa kiongozi hawezi kufanya wema ili ajulikane kwa sifa hiyo bila kujiletea matatizo, na kama ana busara, hatojali iwapo watu watamwita kauzu(bahili). Mtu wa aina hii, baada ya muda watu wataanza kumuona ni mwema zaidi. Pale ambapo kupitia ubahili wake anakuwa na pesa za kutosha kujilinda dhidi ya adui bila kuwapa mzigo wa kodi wananchi wake. Na zaidi ni kwamba, anafanya wema kwa raia wengi bila kuwaumiza kwa kodi huku akiwa na sifa ya ukauzu(ubahili) kwa wale ambao hawapatii kitu, na hawa ni wachache tu.
Katika nyakati zetu hatujaona viongozi wanaofanya mambo makubwa, isipokuwa wale wanaosifika kwa ukauzu. Wengine wote waliingia matatizoni. Papa Julius II baada ya kujinadi kuwa na sifa ya wema ili kupata upapa, hakufanya jitihada zozote za kuendelea na sifa hiyo alipokuwa vitani dhidi ya mfalme wa Ufaransa. Lakini aliendesha vita zake bila kutoza watu wake kodi yoyote, aligharamia vita kutoka katika akiba yake aliyokuwa ametumia muda mrefu kuitunza.
Kama mfalme wa sasa wa Hispania angekuwa na sifa ya wema, asingeweza kufanya na kufanikiwa katika mambo mengi aliyoyafanya.
Kwa hiyo, kama kiongozi anaweza kuepuka kupora mali za wananchi wake, kutofilisika, ameweza kujilinda na kuepuka kutodharaulika, hatakiwi kujali kupewa sifa ya ukauzu. Hiyo ni moja ya sifa inayomuwezesha kubaki madarakani.
Na mtu akipinga na kusema kuwa wema ulimfanya Kaisari kushika madaraka, na kuwa kuna wengine wengi waliopanda vyeo vikubwa kwa kuwa wema, nitajibu hivi; 'unaweza kuwa tayari ni kiongozi au unataka kuwa kiongozi, kama ni kiongozi, wema utakutia matatizoni, na kama unataka kuwa kiongozi ni muhimu watu wakuone ni mwema. Kaisari alikuwa anataka kuwa mtawala wa Roma, lakini baada ya kupata cheo hicho angeendelea na matendo yake ya wema, na utoaji bila kubana matumizi, himaya ya Roma ingeanguka.'
Mtu akiendelea kubisha kuwa, viongozi wengi waliosifika kuwa ni wema sana waliweza kufanya mambo makubwa kwa kutumia majeshi yao. Nitajibu hivi; kiongozi anaweza kutumia mali yake na ya wananchi wake, au ya watu wengine kabisa. Kama anatumia mali yake au ya wananchi wake, lazima awe makini katika matumizi. Lakini kama mali hizo ni za watu wengine hatakiwi kujibana katika kuzitumia kutenda wema. Sababu kiongozi anayeongoza jeshi lake yeye mwenyewe, na anayelihudumia kwa kupora wengine na michango ya lazima, huku akitumia mali zao apendavyo, hatakiwi kujibana katika kuhudumia jeshi lake.
Vinginevyo wanajeshi wake wataacha kumfuata.
Kitu ambacho si chako, wala si cha wananchi wako, unatakiwa kukigawa bila kujibana, kama tu walivyokuwa Cyrus, Kaisari na Alexander. Kugawa mali ya wengine hakukuharibii sifa bali kunaiimarisha zaidi. Kitu kitakachokuletea matatizo ni kutumia mali yako mwenyewe, na hakuna sifa inayomuangamiza mtu haraka kama ya kuwa mwema(mtoaji); kadri unavyoitenda, ndivyo unavyopoteza uwezo wa kuitenda. Hilo linakufanya uwe fukara na mtu wa kudharaulika, au labda kwa kuepuka ufukara uamue kuwa mporaji(ukichukua mali za raia wako kwa nguvu), jambo litakalokufanya uchukiwe. Utu wema husababisha moja kati ya hayo mambo mawili(kudharauliwa au kuchukiwa) na kiongozi anatakiwa kujilinda sana dhidi ya hizi sifa mbili.
Kinyume chake; ni jambo la busara kuvumilia kuitwa kauzu(bahili). Sifa hiyo huleta aibu lakini haikufanyi uchukiwe. Lakini tamaa ya kusifiwa kuwa ni mwema(mtoaji), hupelekea kuwa mporaji, na hilo husababisha uchukiwe na kudharaulika pia.