Mimi sihangaiki kuwatenga. Wacha wakae nao, kama unawalisha vizuri kuku hawachelewi kuanza kutaga tena na akishaanza kutaga lazima awaache tu hao wengine. Heri risk ya kuku kukaa na vifaranga akachelewa kurudia round kuliko kuwatenga mapema kabla manyoya hayajaota vizuri.Kubwa la kujifunza ni namna ya kulea vifaranga. Mwezi uliopita nimepoteza takribani vifaranga 35, iliniuma sanaaaa! Mwisho niligundua makosa yangu kwani niliwatenga na mama zao mapema mno wiki 2 hivi nikawaweka kwenye box huku niwawashia chemli.