Barubaru
JF-Expert Member
- Apr 6, 2009
- 7,161
- 2,323
Nianze kwenda kwa nani?
- Leo nimepata simu, Huko kwangu ofisini, Zote tena taslimu, Zimefika mikononi,
Na zote hizo muhimu, Nimezisoma yakini,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.
2. Simu ya kwanza yasema, Tia mguu njiani,
Mama yako ana homa, Imemuanza kondeni,
Fanya uje hima hima, Kupona si tumaini
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.
3. Simu ya pili yasema, Hamza njoo Omani,
Mkweo anakoroma, Kakumbwa na datsani,
Ukweli hana uzima, Ajekupa buriani,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.
4. Simu ya tatu yasema, Barubaru harahara,
Mkeo wa huko Doha, leo kaumwa na nyoka,
Waganga wanavyosema, Imebakia dakika,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.
5.Simu ya nne yasema, usidharau kufika,
Mwanao Dar isalaama, Mguu umevunjika,
Homa raha alalama, Jinsi anavyoteseka,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.
6. Simu ya tano yasema, kaka yako ana kesi,
Kaiba mali ya umma, Wamemzoa polisi,
Majibu ya mahakama, Uje ulipe upesi,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.
7Watunzi huo ukweli, msidhani naropoka,
Zimeniruka akili, Nabaki kuweweseka,
Mwanakijiji na Ali, Choveki nipe hakika,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.
Dr Hamza Yousuf Al Naamany (Barubaru)
H/N 2436, Umm hays Block.
Minal fahal Street.
Doha.
Qatar