Nianze kwenda kwa nani? (Shairi)

Barubaru

JF-Expert Member
Apr 6, 2009
7,161
2,322
Nianze kwenda kwa nani?
  1. Leo nimepata simu, Huko kwangu ofisini, Zote tena taslimu, Zimefika mikononi,
    Na zote hizo muhimu, Nimezisoma yakini,
    Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.

2. Simu ya kwanza yasema, Tia mguu njiani,
Mama yako ana homa, Imemuanza kondeni,
Fanya uje hima hima, Kupona si tumaini
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.


3. Simu ya pili yasema, Hamza njoo Omani,
Mkweo anakoroma, Kakumbwa na datsani,
Ukweli hana uzima, Ajekupa buriani,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.

4. Simu ya tatu yasema, Barubaru harahara,
Mkeo wa huko Doha, leo kaumwa na nyoka,
Waganga wanavyosema, Imebakia dakika,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.

5.Simu ya nne yasema, usidharau kufika,
Mwanao Dar isalaama, Mguu umevunjika,
Homa raha alalama, Jinsi anavyoteseka,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.

6. Simu ya tano yasema, kaka yako ana kesi,
Kaiba mali ya umma, Wamemzoa polisi,
Majibu ya mahakama, Uje ulipe upesi,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.

7Watunzi huo ukweli, msidhani naropoka,
Zimeniruka akili, Nabaki kuweweseka,
Mwanakijiji na Ali, Choveki nipe hakika,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.



Dr Hamza Yousuf Al Naamany (Barubaru)
H/N 2436, Umm hays Block.
Minal fahal Street.
Doha.
Qatar
 
2. Simu ya kwanza yasema, Tia mguu njiani,
Mama yako ana homa, Imemuanza kondeni,
Fanya uje hima hima, Kupona si tumaini
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.
Huyu kwako ni makini, wengine watajifia,
Hima hospitalini, waganga kumtibia,

Utakwepa kisirani, laana kujipatia,
Muwahishe mama yako, wengine hao maiti!
 
Pokea pole wakwetu, kwa mama huko anzia,
Tena sisubiri mtu, kwa mama watimkia
Si namba mbili wala tatu, ya kwanza ashikilia
Hakuna sawa na mama, sikia baba sikia

Wala sisubiri simu, nyengine ije ingia
Umeshapata salamu, mama wasikilizia
Wajibu kwako muhuimu, safari ukianzia
Hakuna sawa na mama, sikia kaka sikia

Wengine watasubiri, kichwani hilo julia
Tulia uwe mahiri, ni mama wakimbilia
Kwa mama kweli nakiri, ni nani akaribia?
Hakuna sawa na mama, sikia ndugu sikia

Na tena una bahati, mamako anapumua
Chomoka kama baruti, usije kuja jutia
Kwa wako wote wa dhati, ni mama anaanzia
Hakuna sawa na mama, sikia shekhe sikia

Tano nasema kikomo, ni miye nakomelea
Nimeshakupa kisomo, kwa mama kuashiria
Natena hana kipimo, muhimu hiyo kujua
Hakuna sawa na mama, we Barubaru sikia!
 
Nianze kwenda kwa nani?
  1. Leo nimepata simu, Huko kwangu ofisini, Zote tena taslimu, Zimefika mikononi,
    Na zote hizo muhimu, Nimezisoma yakini,
    Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.

2. Simu ya kwanza yasema, Tia mguu njiani,
Mama yako ana homa, Imemuanza kondeni,
Fanya uje hima hima, Kupona si tumaini
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.


3. Simu ya pili yasema, Hamza njoo Omani,
Mkweo anakoroma, Kakumbwa na datsani,
Ukweli hana uzima, Ajekupa buriani,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.

4. Simu ya tatu yasema, Barubaru harahara,
Mkeo wa huko Doha, leo kaumwa na nyoka,
Waganga wanavyosema, Imebakia dakika,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.

5.Simu ya nne yasema, usidharau kufika,
Mwanao Dar isalaama, Mguu umevunjika,
Homa raha alalama, Jinsi anavyoteseka,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.

6. Simu ya tano yasema, kaka yako ana kesi,
Kaiba mali ya umma, Wamemzoa polisi,
Majibu ya mahakama, Uje ulipe upesi,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.

7Watunzi huo ukweli, msidhani naropoka,
Zimeniruka akili, Nabaki kuweweseka,
Mwanakijiji na Ali, Choveki nipe hakika,
Nianze kwenda kwa nani, washairi nambieni.



Dr Hamza Yousuf Al Naamany (Barubaru)
H/N 2436, Umm hays Block.
Minal fahal Street.
Doha.
Qatar


Panapo tumika shoka,usije leta jambia,
Sifananishe na soka,na maisha ya dunia,
Mama yako shamchoka,hivi ndo watuambia?
Wakuanzia ni mama,wengine wafuatia

Tena fanya hima,usije ukajutia,
Hakuwekewa kwa bima,maisha yatalipia,
Ufanya kwake khidima,mola tampa afua,
Wakuanzia ni mama,wengine wafuatia

Kakiyo ana dhahama,kwakweli kajitakia,
Hicho kwake ni kiama,apate pa kujutia,
Umwache akale sima,kamwe sije kimbilia,
Wakuanzia ni mama,wengine wafuatia

Mkweo toka omani,mola pekee ajua,
Omba dua kwa imani,apate japo afua
Mke ombea jirani,wapate kumwangalia,
Wakuanzia ni mama,wengine wafuatia

Mtoto yupo salama,hofu ndio yasumbua,
Nenda mwangalie mama,yeye wakupigania,
Kamwe acha kulalama,nakupa japo usia,
Wakuanzia ni mama,wengine wafuatia
 
Pokea pole wakwetu, kwa mama huko anzia,
Tena sisubiri mtu, kwa mama watimkia
Si namba mbili wala tatu, ya kwanza ashikilia
Hakuna sawa na mama, sikia baba sikia

Wala sisubiri simu, nyengine ije ingia
Umeshapata salamu, mama wasikilizia
Wajibu kwako muhuimu, safari ukianzia
Hakuna sawa na mama, sikia kaka sikia

Wengine watasubiri, kichwani hilo julia
Tulia uwe mahiri, ni mama wakimbilia
Kwa mama kweli nakiri, ni nani akaribia?
Hakuna sawa na mama, sikia ndugu sikia

Na tena una bahati, mamako anapumua
Chomoka kama baruti, usije kuja jutia
Kwa wako wote wa dhati, ni mama anaanzia
Hakuna sawa na mama, sikia shekhe sikia

Tano nasema kikomo, ni miye nakomelea
Nimeshakupa kisomo, kwa mama kuashiria
Natena hana kipimo, muhimu hiyo kujua
Hakuna sawa na mama, we Barubaru sikia!

Nashukuru sana kwa ushauri wako.
Nimelipenda sana shairi lako.
 
Panapo tumika shoka,usije leta jambia,
Sifananishe na soka,na maisha ya dunia,
Mama yako shamchoka,hivi ndo watuambia?
Wakuanzia ni mama,wengine wafuatia

Tena fanya hima,usije ukajutia,
Hakuwekewa kwa bima,maisha yatalipia,
Ufanya kwake khidima,mola tampa afua,
Wakuanzia ni mama,wengine wafuatia

Kakiyo ana dhahama,kwakweli kajitakia,
Hicho kwake ni kiama,apate pa kujutia,
Umwache akale sima,kamwe sije kimbilia,
Wakuanzia ni mama,wengine wafuatia

Mkweo toka omani,mola pekee ajua,
Omba dua kwa imani,apate japo afua
Mke ombea jirani,wapate kumwangalia,
Wakuanzia ni mama,wengine wafuatia

Mtoto yupo salama,hofu ndio yasumbua,
Nenda mwangalie mama,yeye wakupigania,
Kamwe acha kulalama,nakupa japo usia,
Wakuanzia ni mama,wengine wafuatia

Hakika upo juu, Nimekukubali.

Ahsante kwa ushauri.
 
Malala miko tumesikia,nashangaa unachelewa.
Majibu umeshapewa,mama ndio wakuanzia.
Mataizo utapata,mama radhi akikuachia.
Wima fanya haraka.dunia iisijekuelemea.

Waomani anamata,mkwe mpehishima pia.
Wapigie ndugu,wamaskati kukusaidia.
wampeleke mkwe,hospitali asijejifia.
Wima fanya haraka,maisha kuyaokoa.

Doha usidharau,mke atajapotea.
Dada atajachukia,pilau hutapikiwa.
Doctari agizia,nyumbani kusaidia.
Wima fanya haraka,sumu yawezauwa.

Angalia Dar,kunawatu wawajua.
Albimany nikonawe,nitakusaidia
Angalu Muhimbili,mtoto kukufikishia,
Wima kwamama,huyu Moi watampasua.

Hamza,sikia.nduguyo kajitakia
Hahitaji kusaidiwa,kuiba nivibaya.
Huyo hakulelewa,dunia kaivamia.
Wima kimbia,matatizo yakujitakia.

Majibu umepewa,mama wakuanzia.
Mkwe akifuatia,baada ya mama nakwambia.
Mke si wakudharauliwa,hachelewi kukukimbia.
Mtoto akiumia,muhimu kutibiwa.
Mwisho kakaako,hujuma katifanyia hapaswi kusaidiwa.

BY
Albimany.
 
Nimefanya hima miye, nije na nikuambie
Barubaru usikiye, haraka ukafanyie
Shauri nikupatie, nawe ulizingatie,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia

Kwanza nakusalimia, na pole nakupatia
Yote yalokufikia, mazito nakubalia
Masahibu ya dunia, bila hodi yatujia
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia.

Swali ulilouliza, moyoni limeniumiza,
Na tena likaniliza, huzuni likinijaza,
Nikakaa nikawaza, sasa jibu nakujuza,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia.

Mama kashikwa na homa, mauti ayatazama,
Hofu yake kama mama, wanae wako wazima?
Mmoja jela katama, habari mbaya kwa mama
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia!

Ukishamtoa kaka, kwa mama fanya haraka,
Wa kaka mkono shika, mwende mpate baraka,
Kwa mama mkishafika, uzima hautatoka,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia

Kisha umtume kaka, awahi kwenda Tandika,
Kwa mwana wako hakika, mguu alovunjika,
Huko akishakufika, hali itatulizika,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia!

Nawe ufanye haraka, kwenda Doha kwa hakika,
Mauti yasije fika, habiba akakutoka,
Msiba ukakufika, wa nyonda akiondoka,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia!

Na piga simu Omani, kwa wakwe walo tabuni,
Binti yao taabani, mautiuti kitandani,
Utachelewa njiani, wauguliwa mtani,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia.

Uwaambia Omani, dua zapaa mbinguni,
Kwa Subhana Maanani, mwingi wa rehemani,
Wawatakia imani, ukiomba ahueni,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia.

Mke akinusurika, Barubaru kwa hakika,
Nenda Omani haraka, uende bila kuchoka,
Mkweo asije toka, bila ya wewe kufika,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia.

Kama wote watatoka, ukenda kumtoa kaka,
Msiba utawafika, pamoja mtawazika,
Mke wewe utazika, mama kaka atazika,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia.

M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
 

Nimefanya hima miye, nije na nikuambie
Barubaru usikiye, haraka ukafanyie
Shauri nikupatie, nawe ulizingatie,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia

Ukishamtoa kaka, kwa mama fanya haraka,
Wa kaka mkono shika, mwende mpate baraka,
Kwa mama mkishafika, uzima hautatoka,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia
....................

Kama wote watatoka, ukenda kumtoa kaka,
Msiba utawafika, pamoja mtawazika,
Mke wewe utazika, mama kaka atazika,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia
.
.....................
M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)


Nahisi huyo ni gamba, kwa nini akimbiliwe?
Ni gwanda kama si gamba, walio wengi viwewe

Mwache apate kingwamba, atupwe selo alewe!

Awe gamba au gwanda, najuwa wote viwewe!


Kakako si kimbilio, hata aliwe na mwewe

Hata atoe kilio, kelele navyo viwewe

Asisubiri ujio, ajue yupo mwenyewe

Awe gamba au gwanda, nahisi wote viwewe!


Asake wapambe wake, aende hata msewe

Kama
kaoa na mke, asake hata mkwewe
Walipokula vya kwake, malipo sasa wajuwe

Awe gamba au gwanda, najuwa wote viwewe!


Wote hao lao moja, wanagawana wenyewe

Gwanda na gamba wamoja, nishaelewa mweyewe

Watuonesha viroja, Dodoma ndiko kwenyewe!

Awe gamba au gwanda, najuwa wote viwewe!


Zangu hizi ndiyo mwisho, naomba unielewe

Nasema yeye wamwisho, foleni aielewe

Avilapo bila jasho, ajuwe vina mwishowe!

Awe gamba au gwanda, najuwa wote viwewe!
 
Nahisi huyo ni gamba, kwa nini akimbiliwe?
Ni gwanda kama si gamba, walio wengi viwewe

Mwache apate kingwamba, atupwe selo alewe!

Awe gamba au gwanda, najuwa wote viwewe!


Kakako si kimbilio, hata aliwe na mwewe

Hata atoe kilio, kelele navyo viwewe

Asisubiri ujio, ajue yupo mwenyewe

Awe gamba au gwanda, nahisi wote viwewe!


Asake wapambe wake, aende hata msewe

Kama
kaoa na mke, asake hata mkwewe
Walipokula vya kwake, malipo sasa wajuwe

Awe gamba au gwanda, najuwa wote viwewe!


Wote hao lao moja, wanagawana wenyewe

Gwanda na gamba wamoja, nishaelewa mweyewe

Watuonesha viroja, Dodoma ndiko kwenyewe!

Awe gamba au gwanda, najuwa wote viwewe!


Zangu hizi ndiyo mwisho, naomba unielewe

Nasema yeye wamwisho, foleni aielewe

Avilapo bila jasho, ajuwe vina mwishowe!

Awe gamba au gwanda, najuwa wote viwewe!

hahaha choveki hakika umenena!
 
Nimefanya hima miye, nije na nikuambie
Barubaru usikiye, haraka ukafanyie
Shauri nikupatie, nawe ulizingatie,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia

Kwanza nakusalimia, na pole nakupatia
Yote yalokufikia, mazito nakubalia
Masahibu ya dunia, bila hodi yatujia
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia.

Swali ulilouliza, moyoni limeniumiza,
Na tena likaniliza, huzuni likinijaza,
Nikakaa nikawaza, sasa jibu nakujuza,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia.

Mama kashikwa na homa, mauti ayatazama,
Hofu yake kama mama, wanae wako wazima?
Mmoja jela katama, habari mbaya kwa mama
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia!

Ukishamtoa kaka, kwa mama fanya haraka,
Wa kaka mkono shika, mwende mpate baraka,
Kwa mama mkishafika, uzima hautatoka,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia

Kisha umtume kaka, awahi kwenda Tandika,
Kwa mwana wako hakika, mguu alovunjika,
Huko akishakufika, hali itatulizika,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia!

Nawe ufanye haraka, kwenda Doha kwa hakika,
Mauti yasije fika, habiba akakutoka,
Msiba ukakufika, wa nyonda akiondoka,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia!

Na piga simu Omani, kwa wakwe walo tabuni,
Binti yao taabani, mautiuti kitandani,
Utachelewa njiani, wauguliwa mtani,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia.

Uwaambia Omani, dua zapaa mbinguni,
Kwa Subhana Maanani, mwingi wa rehemani,
Wawatakia imani, ukiomba ahueni,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia.

Mke akinusurika, Barubaru kwa hakika,
Nenda Omani haraka, uende bila kuchoka,
Mkweo asije toka, bila ya wewe kufika,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia.

Kama wote watatoka, ukenda kumtoa kaka,
Msiba utawafika, pamoja mtawazika,
Mke wewe utazika, mama kaka atazika,
Kamtoe kwanza kaka, ya Mungu yatafuatia.

M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Barubaru we sikiya,wenzangu lotangulia.
Mwakijiji kapoteya,Segerea kapitia.
Kwa mamako harakiya,na gari kumchukua.
Mama wa kwanza sikia.Nduguyo mi nakwambiya
.

Kwenu Manundu wajuwa,tibaye pata poteya
Mama wa maji kutiwa, mwiliwe umenyongeya
Akifa mama ukiwa, habari kikufikiya
Mama wa kwanza sikia.Nduguyo mi nakwambiya
 
Kama hayo yatokea, Hapa kwetu duniani,
Mara moja kwa sawia, Mbona hicho kisirani?
Haraka bila kawia, Tazama juu mbinguni,
Kwa kwanza kukimbilia, Kwa Mungu kuwaombea.

Wanaosema kwa mama, wajuaje utafika?
Waweza katwa mtama, Ukashindwa na kufika,
Mungu muweza daima, Ombi lako likifika,
Kwa kwanza kukimbilia, Kwa Mungu kuwaombea.

Watu wako taabani, Wewe utafanya nini?
Yamefikia pomoni, We una jeuri gani?
Ukawatoe wodini, weshakuwa mautini?
Kwa kwanza kukimbilia, Kwa Mungu kuwaombea.

Pole ninakupatia, kwa yote yalokupata,
Imani kishikilia, Afueni watapata,
Mungu kimtegemea, Yote hayo yatapita
Kwa kwanza kukimbilia, Kwa Mola kuwaombea.

Na Big Braza Asprin -ODM
Kaunta ya Juu.
MMU.
 
1.Yakhilahi ya wadudi, Nizishusha kwa karima,
Nizidishie imani, pamoja na usalama,
Asprini karudi, Dua zote nishasoma.
Nawashukuru kwa dhati,Mola atawajalia.

2 .Hakika nimeshukuru, Mawazo kunipatia,
Nimeridhia hakika, Majibu kunirushia,
Wengi wamenihakika, Mama kumkimbilia,
Nawashukuru kwa dhati,Mola atawajalia

3 .Mwanakijiji hakika, Kweli nimekusikia,
Damu nzito ya kaka,Jela kaikaribia,
Nimemtuma haraka,Ndugu deni kulipia.
Nawashukuru kwa dhati,Mola atawajalia.

4. Ammi nimekuridhia, Choveki nimesikia,
Pakajimi katulia, Jidu amesha kimbia,
Abimani kaishia, majibu kunipatia,
Nawashukuru kwa dhati,Mola atawajalia.



Barubaru
 
TITI LA MAMA


Titi la mama litamu,hata likiwa la mbwa,
Kiswahili naazimu,sifayo iliyofumbwa,
Kwa wasiokufahamu,niimbe ilivyo kubwa,
Toka kama mlizamu, funika palipozibwa,
Titile mama litamu ,Jingine halishi hamu.

Lugha yangu ya utoto,hata sasa nimekua,
Tangu ulimi mzito,sasa kusema najua,
Ni sawa na manukato,moyoni mwangu na pua,
Pori bahari na mto,napita nikitumia,
Titile mama litamu,jingine halishi hamu.


By Shaban Rorbert
from Jahadhmi's anthology of Swahili poetry
 

Similar Discussions

7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom