Nia ya kuanzisha Tawi la CHADEMA

amba.nkya

JF-Expert Member
Jan 7, 2010
446
131
Nina nia ya dhati kabisa ya kuanzisha Tawi la chama cha CHADEMA ili kuimarisha chama from Grassroot level. Nimesukumwa kufanya hivyo kutokana na ukweli kuwa ninaishi eneo ambalo lina matawi mengi ya CCM lakini sijaona ofisi ya Tawi hata moja la CHADEMA. Nimejaribu kufanya utafiti kama wazo la kuanzisha tawi litakubalika nimebaini kuwa kuna wakazi waliotayari kuanzisha Tawi la CHADEMA kwenye eneo hilo na kujiunga na Chama hiki. Nimejaribu pia kutafuta ofisi ya muda nashukuru imepatikana sehemu nzuri karibu na barabara ambapo inatakiwa kulipia pango kwa mwaka.

WanaJF wenye nia njema na nchi hii naomba msaada wa mambo yafuatayo:

  1. Namna ya kumpata Mbunge wetu John Mnyika maana Tawi hili litakuwa kwenye jimbo lake la Ubungo ili niweze kumuona na kuzungumza naye kuhusu nia ya kuanzisha Tawi na aweze kuja kuonana na wakazi wake ambao wana hamu ya kumuona Mbunge wao. Nimejaribu kumpigia Mh Mnyika kwenye simu yake ya kiganjani iliyoko kwenye mtandao wa CHADEMA huwa haipatikani.
  2. Utaratibu wa kupata fedha za kulipia pango la ofisi ya Tawi.
Nawasilisha:israel:.
 
Mh. Amba,
Ubungo ni kubwa sana, kuwa specific unataka kufungua tawi wapi? Au unataka mchango tuuuuuuuuu!!!!!! watu hawadanganyiki mkuu.
 
Nadhani hayo matawi yanahitajika kufahamika katika kila mkoa, kuna watu wengi ambao wana nia ya kujiunga na kukisupport chama na hawajui pa kwenda. Hao CCM tunajua wana ofisi za wilaya na hata mkoa, hii imewasaidia kuwa na wanachama wengi maana taarifa zinapatikana kiurahisi. Tafadhali sana viongozi mliopo mfanyie hili kazi. Ni muhimu sana kwa mustakabadhi wa CHADEMA yetu na watanzania.
NB. Madiwani mliochaguliwa, eneo la kata ni dogo na tunaamini mnaweza kupita kuwasalimia wanachi waliowaweka madarakani, katika hatua hizi za mwanzo ingekuwa vyema sana kama mtatumia fursa hii kupita kwenye kaya (You may target 10 households/week) mkatambua wale ambao wanasupport chama na hawana kadi za uanachama ili muwape, ikiwa ni pamoja na maelekezo muhimu kuhusu uanachama.
 
Hili bonge la wazo mzee, hata mimi natafuta uwezekano wa kufungua tawi huku niliko ila natafuta mawasiliano na makao makuu ya CHADEMA ili kukieneza chama hadi ngai ya kaya.
 
Mh. Amba,
Ubungo ni kubwa sana, kuwa specific unataka kufungua tawi wapi? Au unataka mchango tuuuuuuuuu!!!!!! watu hawadanganyiki mkuu.

Poti, NB (Gwakukaja), eneo lipo kata ya Kimara, taarifa kamili zitatolewa baada ya kuonana na Mbunge wetu. Hivyo, tupo pamoja ondoa hofu hapo kwenye RED, nina nia njema na ni muadilifu pia, ndio maana namhitaji Mh Mbunge nionane naye, pia akutane na wanachama watarajiwa. Naomba nieleweke hivyo.
 
Wazo ni zuri. Ila nina wasiwasi na 'utaratibu wa kupata fedha za kulipia pango'. Ni vyema tunaofikiria kuanzisha matawi ya CHADEMA tukafikiria pia dhana ya kujitolea na kujitegemea ili tutofautiane na Chaka Chua Matokeo (CCM). Tukitaka wote kuanzisha matawi lakini tukahitaji msaada wa fedha za pango toka makao makuu tutaanza kugombea ruzuku sasa hivi.
 
Hilo bonge la wazo mkuu nakuunga mkono maana hata CCM ina wenyewe sasa Chadema wenyewe ndo sisi. Ila tuwe na msimamo maana mimi nilikuwepo kwenye kuanzisha kambi fulani lakini siku za uchaguzi zikikaribia watu wetu walikuwa wanarubuniwa kwa hela.

Big up mwana mabadiliko
 
download katiba ya chadema kutoka website yao then fuata maelekezo utaweza kufungua tawi baada ya kupata idadi ya wananchama wanaotakiwa, halafu tafuta uongozi wa ulio jirani yako ili utambue uongozi wa kata hapoa kwenu then mtapata mawasiliano ya kufika jimboni hadi kwa mnyika. Hivi sasa ccm wengi wanakandia kuwa hatuna hata ofisi wakati wanashindwa kujua na kukubali kuwa viongozi na wanachama wao wngi walimpigia mnyika kura huku wakiuja hatuana ofisi.

Kufungua matawi na ofisi ni jambo la haraka hivi sasa ili mnyika atakapo tembelea eno lenu kwanza anaanzia ofisi ya chadema kusaini kitabu. Msisahau kutambua kero za wananchi eneo ulipo na kutafuta possible solution kwa ajili ya lkumfikishia mbunge
.
 
nina nia ya dhati kabisa ya kuanzisha tawi la chama cha chadema ili kuimarisha chama from grassroot level. Nimesukumwa kufanya hivyo kutokana na ukweli kuwa ninaishi eneo ambalo lina matawi mengi ya ccm lakini sijaona ofisi ya tawi hata moja la chadema. Nimejaribu kufanya utafiti kama wazo la kuanzisha tawi litakubalika nimebaini kuwa kuna wakazi waliotayari kuanzisha tawi la chadema kwenye eneo hilo na kujiunga na chama hiki. Nimejaribu pia kutafuta ofisi ya muda nashukuru imepatikana sehemu nzuri karibu na barabara ambapo inatakiwa kulipia pango kwa mwaka.

wanajf wenye nia njema na nchi hii naomba msaada wa mambo yafuatayo:


  1. namna ya kumpata mbunge wetu john mnyika maana tawi hili litakuwa kwenye jimbo lake la ubungo ili niweze kumuona na kuzungumza naye kuhusu nia ya kuanzisha tawi na aweze kuja kuonana na wakazi wake ambao wana hamu ya kumuona mbunge wao. Nimejaribu kumpigia mh mnyika kwenye simu yake ya kiganjani iliyoko kwenye mtandao wa chadema huwa haipatikani.
  2. utaratibu wa kupata fedha za kulipia pango la ofisi ya tawi.
nawasilisha:israel:.

kuhusu suala la kupata fedha za pango. Tawi hilo ni lenu au ka mnyika? jana sisi wenzenu tumefungua ofisi ya kata na tuko mbioni kufungua ofisi 5 za mitaa na kama 10 za mashina ndnai ya mwezi huu wa novemba. Hakuna kumsubiri mnyika anzeni wenyewe yey atakuja kuongezea nguvu zenu zilpoishia. Wasilaina na msaidi zzi wa mnyika akupatie namba ya diwani wa chadema kama ailishinda eneo lenu ili mshirikiane kufungua mashina, matawi na ofisi za kata 0713 636676. Lakini nguvu yenu wenyewe ndio muhimu zaidi.
 
Nashukuru kwa michango yenu nitaifanyia kazi pamoja na wadau wenzangu wa CHADEMA
 
huku mbezi mshikamano wananchi wa huku wanataka kununua kiwanja 15mx15m kujenga ofisi ya kudumu ya chadema, nimesikia jana, mnyika anzeni kazi
 
Back
Top Bottom