Nia si kuelezea bajeti ila kumkabili Dr.Slaa na Zitto: Maben

Kimbembe

Senior Member
May 14, 2006
122
15
Jana katika pita pita yangu nimejikuta nikiwa Mbagala. Kuangalia pembeni nikamuona Mabene Mbunge wa Geita -CCM. Nikatambulishwa na kumsalimu kwa jina Buzwagi . Akacheka akasema kijana haya ni mambo makubwa. Nikamuuliza kuna nini Buzwagi akasema ni shwari kabisa .Nikamkazia macho na maswali lukuki ndipo akasema , wao kama wabunge wanafungwa na Katiba ya CCM na Lowasa ndiyo maana wanashindwa kusimamia maslahi ya Taifa. Akasema ukienda kinyume Lowasa anakumaliza na akasema Mawaziri hawaelezei bajeti ila ndiyo wametumwa na JK kufukia mashimo. Akasema kama ni Bajeti sisi ndiyo wa kuiongelea. Nilimpiga maswali hadi akasema CCM kuna uongo wa hali ya juu na akasema hata ukiwa safi ukiingia CCM lazima ujifunze kusema uongo. Anakiri kwamba Wapinzani wanawapeleka puta ila anasema hawatakaa wakakubaliana na wapinzani hata kama jambo ni la ukweli maana haya si matakwa ya Lowasa na JK .

Ameshangaa Mawaziri kupita mikoani kwa jina la kuelezea bajeti lakini akasema najua Serikali imeshikwa pazito.Hapa ni kujibu tuhuma za Zitto na yeye akasema nimwache achape karata zake anangoja kula then wakati wa Bunge.

Nikamuuliza mbona hakupiga kelele juu ya Buzwagi akasema ni ngoma nzito wao wanaitwa na kuambiwa pitisheni. Hatupendi kijana lakini tunapewa amri . Ni bora kuna na kitu mbadala badala ya kugombea kwenye Chama .Ila wapinzani hatuwezi kukubaliana nao hata wakiwa sahihi .

Nikamwacha aendelee na karata zake .
 
Kimbembe,
Majibu ya huyu mbunge wetu Mabene Mbunge wa Geita -CCM, yanasikitisha sana lakini ndio Ukweli.. kama nilivyowahi kusema ktk siasa hakuna kitu RIGHT ama WRONG ila ni politically correct or incorrect!..
Kwa hiyo wao kutokubali ukweli pamoja na kwamba wanafahamu kuwa Upinzani wapo right wanaufanya kuwa mchezo wa kisiasa.
Tatizo moja tu hawa jamaa zetu wanayaona haya upande wa Upinzani kama ni siasa kati ya vyama hali swala la mikataba ya madini (Buswagi) na kadhalika ni maslahi ya taifa zima yaani ni sawa na kuchezea ama kukiuka katiba ya Taifa!
Hapa ndipo wanapozidi kuharibu sifa za chama na wao wenyewe kwani wameshindwa kutenganisha siasa na maslahi ya Taifa hili chini ya Katiba ya nchi yetu na sio katiba ya chama CCM.
 
Mkandara mawazo ya Mabene hayana tofauti na ya JK na watu wake maana yeye alishindwa kutamka neno juu ya tuhuma za ufisadi lakini alivyo kuwadi kaenda kusema US.Kwa mtizamo huu na kasi ya Mawaziri kuwa mikoani na Membe kusema na mabolizi I have feeling kwamba mchezo umeisha hakuna kuwajibika maana wao sasa wanalia na lile la BOT la Buzwagi no one mentioning it .Hapa dawa ni Dlaa kwenda Mahakamani kufungua kesi ama CCM waanze kuadabishwa kuanzia uchaguzi wa Serikali za mitaa na Madiwani ambao Serikali na Tume wana ulazimisha .
 
Kimbembe,
Majibu ya huyu mbunge wetu Mabene Mbunge wa Geita -CCM, yanasikitisha sana lakini ndio Ukweli.. kama nilivyowahi kusema ktk siasa hakuna kitu RIGHT ama WRONG ila ni politically correct or incorrect!..
Kwa hiyo wao kutokubali ukweli pamoja na kwamba wanafahamu kuwa Upinzani wapo right wanaufanya kuwa mchezo wa kisiasa.
Tatizo moja tu hawa jamaa zetu wanayaona haya upande wa Upinzani kama ni siasa kati ya vyama hali swala la mikataba ya madini (Buswagi) na kadhalika ni maslahi ya taifa zima yaani ni sawa na kuchezea ama kukiuka katiba ya Taifa!
Hapa ndipo wanapozidi kuharibu sifa za chama na wao wenyewe kwani wameshindwa kutenganisha siasa na maslahi ya Taifa hili chini ya Katiba ya nchi yetu na sio katiba ya chama CCM.

Mkuu mbona wabunge kibao walishatofautiana na serikali kwenye manufaa ya taifa na bado wanapeta? mmoja wao ni Mzindakaya ambaye miaka na miaka alikuwa anawaumbua bungeni mpaka hapa juzi na yeye alipogundua pesa tamu akamegewa na BOT na kakaa kimya.

Huyo mheshimiwa kachaguliwa na wananchi na inatakiwa atetee maslahi ya wananchi na wala sio CCM au JK peke yao. Akishindwa kufanya hivyo wananchi tutamkaba yeye.
 
Hii ni kauli ya Juma Ngasongwa kwa wananchi

``Bush asingetoa dola hizo kama mambo ya Buzwagi yangegubikwa na rushwa..., Buzwagi ni bomba kweli kweli waacheni wapinzani na propaganda zao za kutamani Ikulu,`` alisema.

Dk. Ngasongwa alilazimika kutoa kauli hiyo baada ya wananchi wa mjini Katesh kutaka kujua kauli ya serikali dhidi ya madai ya wapinzani yakiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Karatu, Dk. Wilbroad Slaa kuhusu ukiukwaji wa taratibu katika kusaini mkataba wa mgodi wa Buzwagi unaodaiwa kusainiwa nje ya nchi na Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Nazir Karamagi mwanzoni mwa mwaka huu.

``Mnaambiwa serikali ilisaini haraka ikasahau maslahi ya nchi, hili nalikanusha mbele yenu sio kweli, hawa watu walijuaje jambo hilo wakati hawakuwa London.

Wale ni wakazi wa Canada, kusainiwa London ilikuwa rahisi sababu waziri na Rais walikuwa London``alifafanua.

``Ilikuwa rahisi kusaini katika ubalozi wetu pale London. pale ni kwetu hakuna tofauti na hapa nchini na sio hotelini kama wanavyopakaza,`` asisitiza.

Hata hivyo, Dk. Ngasongwa alisistiza kuwa katika utiaji wa saini wa mkataba huo hakukuwa na ufisadi wowote uliofanyika kutokana na kauli hizo zimesababisha kuchangia kuboreka kwa mradi huu kuliko yoyote ya madini iliyowahi kusainiwa.

source: Nipashe

nilikuwa nimekasirika imebidi nicheke, kweli viongozi wetu ni wasanii kweli kweli, naona wanaanza kumzidi hata ELI.
tutafika tu pole pole ndio mwendo.
 
Kimbembe,
Alichosema Mabene, ndicho kimekuwa kikifanyika miaka nenda miaka rudi. wale wanaoonekana kwenda kinyume, cha moto wanakiona hasa wakati wa uteuzi kugombea ubunge.
Nina wasiwasi kwamba kauli aliyoitoa kwako pia inaweza kumletea matatizo. muhimu hapa katusaidia kujua kwamba serikali inaendeshwa na Lowassa na JK ni boya tu pale ikulu. Ziara za mawaziri zimetokana na shinikizo la Lowassa.

Inawezekana Lowassa anayo ajenda ya siri kama ilivyokuwa kwa Kagame na Bizimungu huko Rwanda. kwa maana nyingine Lowassa ni mtu hatari sana kuliko JK. Mabadiliko yoyote ya serikali tuyategemee kutokana na utashi wa Lowassa na si JK. hata kama JK angeumizwa kiasi gani na hali inavyoendelea, Kama EL hataridhia hakutakuwa na mabadiliko yoyote. hizi ndizo athari za utegemezi.
 
Mtanzania,
Huyo Mzindakaya alianza kupeta lini?..Usije sahau kwamba kuna malengo ya maslahi binafsi na maslahi ya Taifa. Ukiona watu kama mzindakaya walifanya hayo ili wapate kuitingisha CCM ili wakatiwe chao mapema.
Kwa hiyo Upinzani ndani ya chama CCM ama chochote kile hutokana na mtu kutokuwa ktk mduara wa sinia la Pilau la mauridi kwa hiyo mtu hupiga makelelee wee hadi asikiwe na kuvutwa janvini, baada ya hapo hutamsikia tena.
sasa kwa mara ya kwanza wamekutana na sauti nje ya chama chao na kama walivyozoea chama kushika hatamu wameyafanya maswala ya Kitaifa kuwa maswala ya chama against outsiders..Raia wote tunaitwa Outsiders, wenye wivu nakadhalika. Hapa mjomba watajikaanga kwa mafuta yao wenyewe kwani Population nzima ya WaTanzania sio wana CCM..Watu wameanza kuelewa tofauti ya uanachama na Uraia!
 
Mtanzania,
Huyo Mzindakaya alianza kupeta lini?..Usije sahau kwamba kuna malengo ya maslahi binafsi na maslahi ya Taifa. Ukiona watu kama mzindakaya walifanya hayo ili wapate kuitingisha CCM ili wakatiwe chao mapema.
Kwa hiyo Upinzani ndani ya chama CCM ama chochote kile hutokana na mtu kutokuwa ktk mduara wa sinia la Pilau la mauridi kwa hiyo mtu hupiga makelelee wee hadi asikiwe na kuvutwa janvini, baada ya hapo hutamsikia tena.
sasa kwa mara ya kwanza wamekutana na sauti nje ya chama chao na kama walivyozoea chama kushika hatamu wameyafanya maswala ya Kitaifa kuwa maswala ya chama against outsiders..Raia wote tunaitwa Outsiders, wenye wivu nakadhalika. Hapa mjomba watajikaanga kwa mafuta yao wenyewe kwani Population nzima ya WaTanzania sio wana CCM..Watu wameanza kuelewa tofauti ya uanachama na Uraia!

Mkandara,

Mzindakaya tokea miaka ya chama kimoja mpaka wakati wa vyama vingi alikuwa na uwezo wa kuikosoa serikali na kulipua mabomu.

Walimpa vyeo bado alikuwa anasema kweli.

Mkapa ndiye alifanikiwa kumnunua kwa kumkatia mabilioni ya BOT wakati jamaa hata hajui biashara ni nini. Matokeo yake hizo pesa za walipa kodi zimepotea na sasa Mzindakaya hawezi kusema neno zaidi ya kutetea mafisadi.

Siasa ni mchezo mchafu sana na njia pekee ya kubaki msema kweli ni wewe mwenyewe kuwa msafi, huku wangesema to be whitter than white. Kwenye chama chochote cha siasa huwezi kujifanya mkweli huku una matatizo yako mengi ambayo unategemea hao unaowaumbua ndio wakusaidie.

Tamaa ndio inawafanya wana siasa wawe malaya. Wabunge hawajachaguliwa na JK wala Lowassa, wamechaguliwa na wananchi, sasa kama wana akili kwa nini wawaache watu waliowachagua?

Wanataka vyeo zaidi na maslahi zaidi na ndio maana wanawasahau wananchi waliowapeleka bungeni.
 
hawa watu wapumbavu kweli yaani anakili anafumbishwa mdomo na EL? kwana huyo ndiye aliyemchagua? akifanya mambo sawa hata akienda chama cha wapinzani siwatamchagua tu? mbona na hawa wabunge wa ccm wanakuwa mbumbumbu? kweli itakuwa kazi kuleta mabadiliko TZ kama kila mtu anangalia maslahi yake mwenyewe.
 
Mtanzania,
Mzindakaya tokea miaka ya chama kimoja mpaka wakati wa vyama vingi alikuwa na uwezo wa kuikosoa serikali na kulipua mabomu
Una maana wakati wa Nyerere huyu jamaa aliweza kuikosoa serikali, mbona sikumbuki?.walioikosoa CCM chini ya chama kimoja tunajua kabisa wako nje ya chama na hawatapewa nafasi kamwe..kina Mtei...
Mjomba kusema kweli ndani ya chama CCM ni usanii mtupu na wao wenyewe wanasema hakuna maslahi nje ya CCM. Kama angekuwa mnoko hivyo asingeweza kudumu CCM hii inafahamika tazama akina Mrema, Seif Sharif, Salim na Malecela ni miongozi mwa viongozi wachache waliokuwa wakisimama kutetea kile wanachoamini wao hata kama kilikuwa ni polically incorrect.. NOT any more mjomba sio ktk dunia hii ya Utandawazi na soko huria maanake hata siasa ya Bongo imekuwa biashara ya Utandawazi na soko huria!..mwenye mtaji hakosi kununua nafasi yake..... Lol!
 
ss jamani kweli tutapata viongozi wazuri au kila mmoja yuo kwa ajili ya kulitetea tumbo lake
 
naona mafisadi wapo wengi kumbe sio wale jk 11 tu peke yao....maana mtu uchaguliwe na wananchi umuogope mkuu wako wa kazi haya mwaka 2010 na amwambie huyo lowasa basi ampatie ubunge
 
Wabunge wengi wa CCM huwekwa kwa nguvu za wizi wa kura . Kwa mfano Mabina mwenyewe juzi kazomewa mbele ya rais na akakataliwa kusimama kuhutubia na hakuweza kusema lolote , leo akitetea maslahi ya Lowasa namwelewa maana anajua atakuwa kama alivyo shinda Mudhihiri hakutakiwa lakini alishinda
 
Back
Top Bottom