johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,845
- 141,767
RC Makonda ametembelea kituo cha daladala Makumbusho na kuzungumza na wadau wa kituo hicho wakiwemo madereva, makondakta, wafanyabiashara na abiria wanaosubiri kusafiri.
Makonda ameahidi zoezi la kupuliza dawa mitaani litakuwa endelevu na kuwataka wananchi wawe na nidhamu kwenye swala zima la usafi.
Wakati huo huo, Paul Makonda leo April 1, 2020 ameruhusu Bajaji na Bodaboda zote kuingia katikati ya Jiji hilo ili kukabiliana na Adha ya Usafiri wanayokabiliwa wananchi katika kipindi hiki cha kupambana na Ugonjwa wa #Corona.
Makonda ameruhusu bodaboda na bajaji kuingia katikati ya Jiji
Makonda amewataka wenye nyumba za kupanga kupunguza kodi kwa 50%
Makonda amesema yeye hana mamlaka ya kuwaamuru Mwendo kasi hilo ni jukumu la waziri Jaffo
Wasiokuwa na shughuli za maana basi wabaki majumbani wasizurure hovyo.
Kama huna safari ya lazima kwenda mkoani basi usisafiri na kama uko mkoani usije Dar kama huna sababu za msingi.
Amesema Ndege moja ya Ethiopia inaingia kwa ajili ya Watanzania ambao wanahitaji kurudi nyumbani, sasa wakishaingia watafikia karantini kwa ajili ya uangalizi kwa hiyo mtu yeyote asiende Uwanja wa Ndege watapokelewa na ofisi ya Mkoa na kupelekwa Karantini kwa siku 14.
“Mungu akipenda tutakuwa na helkopta zitapita kumwaga dawa za kuua wadudu na gari pia zitapita kila sehemu nitatumia mamlaka yangu kufanya kazi". Amesema RC Makomda
Makonda ameahidi zoezi la kupuliza dawa mitaani litakuwa endelevu na kuwataka wananchi wawe na nidhamu kwenye swala zima la usafi.
Wakati huo huo, Paul Makonda leo April 1, 2020 ameruhusu Bajaji na Bodaboda zote kuingia katikati ya Jiji hilo ili kukabiliana na Adha ya Usafiri wanayokabiliwa wananchi katika kipindi hiki cha kupambana na Ugonjwa wa #Corona.
Makonda ameruhusu bodaboda na bajaji kuingia katikati ya Jiji
Makonda amewataka wenye nyumba za kupanga kupunguza kodi kwa 50%
Makonda amesema yeye hana mamlaka ya kuwaamuru Mwendo kasi hilo ni jukumu la waziri Jaffo
Wasiokuwa na shughuli za maana basi wabaki majumbani wasizurure hovyo.
Kama huna safari ya lazima kwenda mkoani basi usisafiri na kama uko mkoani usije Dar kama huna sababu za msingi.
“Mungu akipenda tutakuwa na helkopta zitapita kumwaga dawa za kuua wadudu na gari pia zitapita kila sehemu nitatumia mamlaka yangu kufanya kazi". Amesema RC Makomda