Kuna wimbo fulani kuna sehemu msanii anaimba "mama yake amesema niachane na mwanae na mwanae bado anasoma eeh" sijui ni Q chief yule aliimba au nani.wimbo mwingine kuna sehemu msanii anaimba "nimedharauliwa sana" wimbo huu una mahadhi kama ya ule wimbo wa pico wa kumpenda kikongwe.Na wa mwisho ni ule "acha kupiga mayoe wacha wayaone mwenyewe" nadhani ni wimbo wa zilipendwa
 
Natafuta wimbo mmoja hivi naupenda sana japo sijui ameimba nani...

Jamaa analalamika sana kwamba baba yake anampiga kwa fimbo mbele ya mkewe. Anahuzunika sana kisha anauliza baba kama ulijua mimi ni mdogo sasa kwanini uliniozesha

(anachanganya na lugha fulani ya kikabila nadhani ni kisukuma na hata mahadhi ya wimbo yamekaa kisukuma)
 
Natafuta shairi (nasheed) moja ambayo wanapenda sana kuitumia kwenye audio za wahadhiri wa kiislam

Kabla shekh hajaanza kuzungumza utasikia "...mau ubayyinu 'alaa maainiy wa maa qaala sawfa tajriy 'alayhi thakiil, thakil tujazzidu alaa shughuriy..."

Hiyo kitu kila ninachofanya ili kuipata nimedunda
 
 
Wimbo wa Park Lane, upo katika miondoko ya Funky hivi.

RFA walitumia beat yake kwenye kipindi chao fulani cha asubuhi saa kumi na mbili na nusu hivi.

Mwenye nao tafadhali.
 
mwenye nyimbo hiz jaman kaka yuko town by UVC ,Kanizimia by K basil ,Nataka by Wandago family.nimezitafuta sana mwenye nazo pliiz 👏 natanguliza shukran
 
Wakuu kuna wimbo nautafuta ni aina ya kama bolingo ivi aliyeimba sijamjua ila kuna baadhi ya maneno nayakumbuka katika wimbo huo,

Mpenziii nimekuzoea
Kuwa nawe wakati woote
Mpenziii nmekuzoea
Kuwa nawe wakati wooote

Mawazo mawazo mawazooo
Ukiwa ukiwa ukiwa
Binti nimekuzoea
Kuwa nawe wakati wote.


Kama kuna mtu ameutambua naomba anisaidie jina la mwimbaji au wimbo, kama anao itapendeza zaidi
 
Wakuu kuna wimbo nautafuta ni aina ya kama bolingo ivi aliyeimba sijamjua ila kuna baadhi ya maneno nayakumbuka katika wimbo huo,

Mpenziii nimekuzoea
Kuwa nawe wakati woote
Mpenziii nmekuzoea
Kuwa nawe wakati wooote

Mawazo mawazo mawazooo
Ukiwa ukiwa ukiwa
Binti nimekuzoea
Kuwa nawe wakati wote.


Kama kuna mtu ameutambua naomba anisaidie jina la mwimbaji au wimbo, kama anao itapendeza zaidi
Betty nimekuzoea kuwa nawe wakati wowote mawazo mawazo mawazo, ukiwa ukiwa.....
 
Wakuu kuna wimbo nautafuta ni aina ya kama bolingo ivi aliyeimba sijamjua ila kuna baadhi ya maneno nayakumbuka katika wimbo huo,

Mpenziii nimekuzoea
Kuwa nawe wakati woote
Mpenziii nmekuzoea
Kuwa nawe wakati wooote

Mawazo mawazo mawazooo
Ukiwa ukiwa ukiwa
Binti nimekuzoea
Kuwa nawe wakati wote.


Kama kuna mtu ameutambua naomba anisaidie jina la mwimbaji au wimbo, kama anao itapendeza zaidi
Juma kakele wimbo unaitwa bety
 
Kuna wimbo fulan wa bend hv ya zamani baadhi ya kipande chake kinaimba hv
"...... Kushindwa kutoka ahhh hapa nyumbani.. najuta eh najuta nimekosa najuta eh najuta nisamehe...
Fikiri naomba unisamehe kushindwa kutoka ahhhapa nyumbani......."
Msaada wakuu
 
...akajifungua mtoto wa kike akampa jina lake vumilia...

alipofika darasa la tatu akampa historia ya Maisha na kumsihi asome kwa bidii...

alipofika kidato cha tatu.....

naombeni hii nyimbo jina limenitoka ila baadhi ya mistari ndiyo hiyo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom