Ni Wezi na Hawajasajiliwa, Kwa Nini Wanaendelea Kuchimba na Kuuza Dhahabu?

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,762
71,145
Mwenye uelewa mpana wa maamuzi ya Mkuu na kamati yake atusaidie hapa. Mkuu jana akihitimisha ripoti ya pili ya Makanikia ametuaminisha kuwa ACACIA ni wezi wakubwa, wanafanya biashara kinyume cha sharia kwani hawajasajiliwa hapa nchini na waongo wakubwa.
Lakini kinacho shangaza ni kuwa kilichozuiwa ni kusafirisha mchanga tuu, ila uchimbaji, uchakataji na usafirishaji wa dhahabu uko palepale kwa hawa watu wanaofanya shughuli kinyume cha sharia bila kusajiliwa. Matumaini ya wengi yalikuwa shughuli zao ambazo hazipo kisheria baada ya kugundulika zingesimamishwa ile ile jana, sasa kulikoni?
Sasa hao wakina Chenge na wenzake tutawaita wa nini kuwahoji wakati wezi na wasiopo kisheria bado tupo nao? Mie naona kama drama Fulani hivi na kama kawaida tunalishwa matango pori na malengo ya kiki za kisiasa yametimia na hali kubaki ile ile.
 
Maoni yangu juu ya hawa wezi
WATATULIWE MARINDA HADHARANI KWA SIKU 7 MFULULIZO
Na hiyo kazi apewe bwana Nokia83
[HASHTAG]#HappyAnniversaryToMeInJF[/HASHTAG]
 
Haya Ndio maajabu yanayopatikana Tanzania tu!
Mimi niliposikia acacia hawajasajiliwa pale pale nikajua wataambiwa kuanzia sasa wasimishe uzalishaji! Ila eti waombe samahani
 
Nadhani wameachwa ili washughulikiwe taratibu,walipe walichoiba,wapigwe faini huku ajira ikiendelea na ile hadhi ya kujali na kuthamini wawekezaji iendelee kuwepo! Kwakuwa idara zote za serikali zimeambiwa zilifanyie kazi haraka basi nisahihi ilivyoshauriwa na tume.
Hili jambo ninyeti sana na linafatiliwa na wawekezaji wakubwa duniani kote,haihitajiki kulikurupukia Kama tunavyosema kilasiku rais asikurupuke.
 
Kiki za kisiasa ni mbaya sana..matarumbeta siku nzima halfu ripoti ya uchunguzi ovyo kweli
 
Mtu mmoja aliniambia kwa jinsi nchi nzima inavyo hamasishwa kuangalia TV hiyo ripoti kuwa hakuna kitu zaidi ya Kiki tuu. Na kwa kuona hivyo eti Mwigulu naye anatangaza kuwa amezuia wote walio tajwa kutoka nje ya nchi! Jee anayo mamlaka hayo?
 
Kampuni haijasajiliwa halafu bado inachimba madini.
Teh teh teh
CCM NI KICHWA CHA MWENDAWAZIMU. Waliwezaje kufanya kazi na kulipa kodi wakati hawajasajiliwa?
CCM NI CHAMA CHA MAJAMBAZI
 
Nadhani wameachwa ili washughulikiwe taratibu,walipe walichoiba,wapigwe faini huku ajira ikiendelea na ile hadhi ya kujali na kuthamini wawekezaji iendelee kuwepo! Kwakuwa idara zote za serikali zimeambiwa zilifanyie kazi haraka basi nisahihi ilivyoshauriwa na tume.
Hili jambo ninyeti sana na linafatiliwa na wawekezaji wakubwa duniani kote,haihitajiki kulikurupukia Kama tunavyosema kilasiku rais asikurupuke.
Kumbe unadhani mi nilijua una uhakika.
 
Hata hao wazungu wanatushangaa sana. kwa kifupi hakuna kitu hapa
 
Back
Top Bottom