Ni wazi sasa uchumi wa nchi unapumulia mashine

jiwe angavu

JF-Expert Member
Aug 28, 2015
19,092
35,900
Madelo Gawiza.

Naomba niende moja kwa moja kwenye mada husika..hali ya uchumi ya nchi yetu iko taabani..hili limejidhihirisha wazi kabisa kupitia hotuba ya leo ya Rais wetu katika uzinduzi wa ulipaji kodi kwa njia ya kielekitroniki.

Ukiisikiliza kwa umakini hotuba ya JPM zile Mbwembwe na maneno makali ya utumbuaji majipu na vitisho..yameshindikana kutumika katika hotuba yake..badala yake kuongea lugha ya upole na usistizaji juu ya ulipaji kodi.

Amezungumza kwa kuyaomba na kuyataka makampuni kulipa kodi..kwa lugha ya upole sana..hii inaonyesha niwazi sasa hakuna namna zaidi ya kuwabembeleza waingie kwenye mfumo wa kielekitroniki ili angalau tupate kodi.

Kuna vishiria vingi vya kueleza hili suala la anguko kiuchumi..hasa pale alipo sisi tiza suala la kutafuta vyanzo vipya ya ukusanyaji kodi..si suala baya ila inafikia hatua rais anaomba tra wabuni hata mbinu ya kutengeneza vitambulisho na kuviuza kwa wamachinga ili iweze kujiongezea mapato.. kwangu mimi hili linaonyesha wazi hali yetu kiuchumi sio shwari kabisa.

Tunakoelekea nadhani si mbali zile kodi za kichwa zitarudi..ili mradi kuirudisha pesa serikalini ili serikali iweze kujiendesha..

Suala pia la kusitisha ajira na kupunguza wa fanya kazi serikalini kwa kisingizio cha kuleta weledi katika utumishi wa umma ni la kisiasa zaidi..ila ukweli ni kwamba serikali imeelemewa kiuchumi.

Ukitizama pia katika bajeti ya mwaka wa fedha unaoisha 2016/2017 bajeti ilishindwa kuvuka hata asilimia 30 kwa baadhi ya wizara..huku wizara zingine zikipata zaidi ya aslimia 150..huu pia ni uendeshwaji mbovu wa serikali kupitia matamko ya JPM bila kuzingatia sera na utawala bora..katika mgawanyo wa bajeti ya serikali.

N.B: naunga mkono juhudi zote za Raisi katika kuleta maendeleo ya taifa hili.. ila naomba azingatie sera,na utawala bora hasa kufuata mwongozo na kanuni za bunge katika utekelezaji wa bajeti..
 
Toka mdogo hii kauli ya "uchumi unapumulia mashine" nimekuwa nikiusikia. Inaonekana hii mashine ni kiboko, maana imeweza kuuweka uchumi hai siku zote hizo.

Lini huo uchumi utaanza kupumua bila mashine? Sijui, aliyetoa mada atujuze.
 
Kila mwaka wanatikisa Utalii, unategemea nini?

VAT mwaka jana in short notice

Concession Mwaka huu again in Short notice

Utalii haukuwi inapotakiwa

Ethiopia, Mauritius ---Tourism income is amazing

Sasa Tanzania ina vivutio exclusive...lakini Zero Bashite planning
 
CCM Wabunge wanaoua utalii kwa kupitisha budget ya Maghembe Kishabiki

kesho utalii utadumaa kabisa....CCM Wataunda tume na kumtumbua Maghembe
 
Usimjaribu mtukufu. Yeye huwa haamriwi wala kuelekezwa cha kufanya. Anajua kila kitu
 
Uchumi unaporomoka kwa kasi sana

Sasa Wanakuwa wabishi kusikiliza maoni ya watu, wanakiburi. Wakati uchumi ukifika chini...Ndio watakumbuka
 
Ndo maana tunasema kikwete ni mtoto wa mjini na huyu mwingine ni wa kuja.....
Aliwezaje kulipa watumishi hewa, kuruhusu safari za nje, mikutano ya hadhara nk na mambo mifukoni mwa watu yalikuwa murua?
HUYU WA KUJA MJINI ANASUMBUA NA KUHARIBU KABISA UCHUMI WA NCHI
 
Hakuna nchi inayobaki salama hata baada ya kui-abuse sekta binafsi!!!

Hata Tanzania ya Baba wa taifa ilikuwa mbaya kwa sababu walii-abuse sekta binafsi!!!
tatizo si UKUSANYAJI MAPATO (Ukusanyaji KODI)

Tatizo ni pale MKUU WA KAYA anapotaka WAPIGA DILI waishi kama MASHETANI....
Tunao umia ni sisi WANANCHI wa kawaida (hohe hahe)
 
Kila mwaka wanatikisa Utalii, unategemea nini?

VAT mwaka jana in short notice

Concession Mwaka huu again in Short notice

Utalii haukuwi inapotakiwa

Ethiopia, Mauritius ---Tourism income is amazing

Sasa Tanzania ina vivutio exclusive...lakini Zero Bashite planning

You talking nonsense. Umeangalia mapato ya utalii ya Ethiopia ukalinganisha na Tanzania? Jengeni utamaduni wa kufanya utafiti kabla ya kurukia mada.
 
tatizo si UKUSANYAJI MAPATO (Ukusanyaji KODI)

Tatizo ni pale MKUU WA KAYA anapotaka WAPIGA DILI waishi kama MASHETANI....
Tunao umia ni sisi WANANCHI wa kawaida (hohe hahe)
Sijazungumzia suala la kodi bali nimezungumzia suala la ku-abuse private sector! Na hapo tukaja kuaminishwa wafanya biashara na matajiri ni wezi na wapiga dili! Hata akina sie ambae mwanzoni kabisa tulianza kulalamika kwamba huko tunakoenda sio kuzuri nasi tukaambiwa tulizoea kuishi kwa madili na lazima tuisome namba!!!
 
Back
Top Bottom