Ni wazi reli za Arusha na Tanga walirekebisha kutumia kodi yetu ili kujifanyia kampeni maana treni hatuzioni na sasa zimekuwa kero za faini za trafiki

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Kuna vitu vinaudhi sana. Serikali ya CCM walifanya mbwembwe nyingi kusema wanafufua huduma ya treni kwenda Arusha na Tanga. Na tukumbuke walitumia fedha yetu ya kodi, sio fedha za CCM.

Sasa ni wazi kwamba yote haya walifanya kwa ajili ya kampeni waliyotaka kufanya ya maendeleo ya vitu, ili kuwashawishi watu wa kanda ya Kaskazini ambako CHADEMA imeotesha sana mizizi. Hivi hizo treni walizosema zinarudi ziko wapi, mbona hatuzioni?

Na sasa hizi reli zimekuwa kero ya faini za trafiki. Askari wa trafiki wanakaa karibu na reli zinapokatisha barabara halafu wanapiga watu faini eti unatakiwa sio tu upunguze kwendo unapovuka reli bali usimame kabisa kwa sekunde kadhaa. Juzi nimegombana na trafiki kwa ajili ya hili nikamuuliza, kwani leo zimepita treni ngapi, au mara ya mwisho treni imepita hapa lini, na ikipita huwa inapita saa ngapi?

NIliona polisi wameweka hata kibanda cha trafiki karibu na hiyo railway crossing, labda wameona faini ni nyingi sana. Serikali ituambie kama kweli walikuwa na lengo la kurudisha huduma za treni au ilikuwa ni mbwembwe tu za kampeni. Na pia tuelezane basi kama fedha iliyotumika kurekebisha hizi reli mnataka irudi kwa njia ya faini za trafiki!

Jamani tumechoka na hizi faini za trafiki za kulazimisha, mnataka tufanye nini?
 
Hizi zilikuwa mbwembwe tu za kampeni, hakuna lolote la maana linaloendelea!

1603193352624.png
 
Kwa anayejua vema msaada mimi inanichanganya lipi ni jina la shirika la reli kati ya haya ninayoona yanatumika mara kwa mara

TRC
RAHCO
TRL
Kwa sasa shirika linaitwa TRC baada ya serikali kulichukua tena. Liliitwa TRL wakati linaendeshwa kwa mkataba na RAHCO, kampuni kutoka India, wakawa wanatupiga sana kwa kushirikiana na maofisa wetu wenyewe. RAHCO walikuwa na management contract, wakiwa na share ya 51%. Mambo ya Mkapa hayo..
 
Mbofu mbofu nyingine

Hawa wanasema treni za Dar - Arusha zipo JUmatatu na Ijumaa. Novmber 9 ni JUmatatu wanasema hakuna treni siku nimechagua. Kama unnaweza ku-book online tafadhali weka icha hapa nione.

Labda uchaguzi ukipota na treni zitarudi zilikotoka

1603228379603.png
 
Kwa sasa shirika linaitwa TRC baada ya serikali kulichukua tena. Liliitwa TRL wakati linaendeshwa kwa mkataba na RAHCO, kampuni kutoka India, wakawa wanatupiga sana kwa kushirikiana na maofisa wetu wenyewe. RAHCO walikuwa na management contract, wakiwa na share ya 51%. Mambo ya Mkapa hayo..

Asante sana Mkuu nimekuelewa vema
 
Kuna vitu vinaudhi sana. Serikali ya CCM walifanya mbwembwe nyingi kusema wanafufua huduma ya treni kwenda Arusha na Tanga. Na tukumbuke walitumia fedha yetu ya kodi, sio fedha za CCM.

Sasa ni wazi kwamba yote haya walifanya kwa ajili ya kampeni waliyotaka kufanya ya maendeleo ya vitu, ili kuwashawishi watu wa kanda ya Kaskazini ambako CHADEMA imeotesha sana mizizi. Hivi hizo treni walizosema zinarudi ziko wapi, mbona hatuzioni?

Na sasa hizi reli zimekuwa kero ya faini za trafiki. Askari wa trafiki wanakaa karibu na reli zinapokatisha barabara halafu wanapiga watu faini eti unatakiwa sio tu upunguze kwendo unapovuka reli bali usimame kabisa kwa sekunde kadhaa. Juzi nimegombana na trafiki kwa ajili ya hili nikamuuliza, kwani leo zimepita treni ngapi, au mara ya mwisho treni imepita hapa lini, na ikipita huwa inapita saa ngapi?

NIliona polisi wameweka hata kibanda cha trafiki karibu na hiyo railway crossing, labda wameona faini ni nyingi sana. Serikali ituambie kama kweli walikuwa na lengo la kurudisha huduma za treni au ilikuwa ni mbwembwe tu za kampeni. Na pia tuelezane basi kama fedha iliyotumika kurekebisha hizi reli mnataka irudi kwa njia ya faini za trafiki!

Jamani tumechoka na hizi faini za trafiki za kulazimisha, mnataka tufanye nini?
Treni hiyo haina biashara,ccm hawajawahi kua na akili
 
Kuna vitu vinaudhi sana. Serikali ya CCM walifanya mbwembwe nyingi kusema wanafufua huduma ya treni kwenda Arusha na Tanga. Na tukumbuke walitumia fedha yetu ya kodi, sio fedha za CCM.

Sasa ni wazi kwamba yote haya walifanya kwa ajili ya kampeni waliyotaka kufanya ya maendeleo ya vitu, ili kuwashawishi watu wa kanda ya Kaskazini ambako CHADEMA imeotesha sana mizizi. Hivi hizo treni walizosema zinarudi ziko wapi, mbona hatuzioni?

Na sasa hizi reli zimekuwa kero ya faini za trafiki. Askari wa trafiki wanakaa karibu na reli zinapokatisha barabara halafu wanapiga watu faini eti unatakiwa sio tu upunguze kwendo unapovuka reli bali usimame kabisa kwa sekunde kadhaa. Juzi nimegombana na trafiki kwa ajili ya hili nikamuuliza, kwani leo zimepita treni ngapi, au mara ya mwisho treni imepita hapa lini, na ikipita huwa inapita saa ngapi?

NIliona polisi wameweka hata kibanda cha trafiki karibu na hiyo railway crossing, labda wameona faini ni nyingi sana. Serikali ituambie kama kweli walikuwa na lengo la kurudisha huduma za treni au ilikuwa ni mbwembwe tu za kampeni. Na pia tuelezane basi kama fedha iliyotumika kurekebisha hizi reli mnataka irudi kwa njia ya faini za trafiki!

Jamani tumechoka na hizi faini za trafiki za kulazimisha, mnataka tufanye nini?
Lazima unamtindio wa ubongo wewe mtoa mada!
 
Lazima unamtindio wa ubongo wewe mtoa mada!
Unajua wanasaikolojia huwa wanasema watu wenye mtindio wa ubongo huwa wa kwanza kudhani wengine ndio wana mtindio wa ubongo?

Ni sawa na mtu kuwa na jicho moja na kudhani wote wenye macho mawili wana tatizo. Ndio wewe.
 
Hakuna la maana kwenye reli bado ni mbovu na hatari kutumia.
Hilo swali nimejiuliza sana. How safe nitakuwa usiku nimelalal kwenye kale chachumba ka first class kama kapo kabla sijasikia tumbwi ndani ya mto Wami daraja limekatika kwa uchakavu?
 
Back
Top Bottom