Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Nilisikiliza hotuba ya Kikwete jana katika TV katika utaratibu wake wa kuhutubia wananchi kila mwisho wa mwezi. Kwa maoni yangu kwa muda wote wa hotuba yangu sikuona jambo jipya alilozungumza na kuonyesha yeye kaka mkuu wa nchi ana muelekeo wa kuchukua hatua na hasa kwa mambo yanaoonekana wazi kuwachosha watanzania. Suala la mgao wa umeme, Dowans, mfumuko wa bei, kupanda kwa gharama za maisha anazumgumzia katika mtazamo wa kuwaonea huruma wananchi wake badaa ya kuonesha nini atafanya yeye kama raisi.
Lakini kubwa zaidi alilonishangaza ni juu ya lawama zake kwa CHADEMA. Kuwa chama hiki kinamuelekeo wa kuleta chuki, vurugu na kutaka kuitoa serikali iliyoko madarakani kwa nguvu. Nadhani Kikwete anakimbia kivuli chake mwenyewe. Kinachofanywa na CHADEMA kwa mtazamo wangu ni kuwaamsha watanzania juu ya utendaji mbovu wa serikali ya CCM na pia kuiamsha serikali hiyo kuwa mnakolipeleka taifa sio.
Mambo mengi yaliyokuwa yakitokea ndani ya serikali ya CCM wanatanzania wasingeyajua kama si wabunge na viongozi wa CHADEMA kuyaweka hadharani.Na mengi ya mambo hayo ni yale yaliyopeleka kuingiza nchi katika wakati mgumu kabisa.
Sasa kiongozi wa nchi anapotoa hotuba ya kuonyesha masikitiko kwa wananchi wake badala ya kutoa njia za kutatua matatizo yanayojitokeza napata mashaka na uwezo wa kiutendaji wa huyu bwana.
Nadhani umefika muda sasa watanzania wote bila kujali itikadi zetu za vyama, dini, kabila kufanya maombi kama sio matambiko ili kumuomba mungu amsaidie huyu bwana kuliongoza taifa letu katika njia iliyo sahihi kwani kwa sasa gari limepoteza mwelekeo kabisa.
Lakini kubwa zaidi alilonishangaza ni juu ya lawama zake kwa CHADEMA. Kuwa chama hiki kinamuelekeo wa kuleta chuki, vurugu na kutaka kuitoa serikali iliyoko madarakani kwa nguvu. Nadhani Kikwete anakimbia kivuli chake mwenyewe. Kinachofanywa na CHADEMA kwa mtazamo wangu ni kuwaamsha watanzania juu ya utendaji mbovu wa serikali ya CCM na pia kuiamsha serikali hiyo kuwa mnakolipeleka taifa sio.
Mambo mengi yaliyokuwa yakitokea ndani ya serikali ya CCM wanatanzania wasingeyajua kama si wabunge na viongozi wa CHADEMA kuyaweka hadharani.Na mengi ya mambo hayo ni yale yaliyopeleka kuingiza nchi katika wakati mgumu kabisa.
Sasa kiongozi wa nchi anapotoa hotuba ya kuonyesha masikitiko kwa wananchi wake badala ya kutoa njia za kutatua matatizo yanayojitokeza napata mashaka na uwezo wa kiutendaji wa huyu bwana.
Nadhani umefika muda sasa watanzania wote bila kujali itikadi zetu za vyama, dini, kabila kufanya maombi kama sio matambiko ili kumuomba mungu amsaidie huyu bwana kuliongoza taifa letu katika njia iliyo sahihi kwani kwa sasa gari limepoteza mwelekeo kabisa.