Ni wapi naweza pata matibabu ya OZONE hapa nchini?

Mpauko

R.I.P
Jan 19, 2019
2,323
3,353
Habari!

Ni wapi naweza kupata tiba kwa njia ya Ozone wakuu?

Ozone ni tiba ambayo Oksijen Inatolewa Kwenye Mtungi Inapita Kwenye Mashine Inachakatwa Kuwa Ozone.

Wakati Huo Damu yako Inatolewa Mkonon Na Kupelekwa Kwe Mashine Ndogo Mpaka Kwe Tube Fulan.

Ile Ozone Inapitishwa Kwenye Mafuta Fulan Inaingia Kwenye Tube Yenye Damu , Damu Inatokea Upande Mwingne Inarudishwa Mwilini.

OZONE inatibu:

-kufubaza wadudu wa HIV na bacteria.

-husaidia wenye kisukari.

-inaondoa seli mbovu na kuunda upya.

-hurekebisha homoni.

Ninahitaji kufahamu ni wapi nitapata tiba hii hapa Tz...
 
Habari!

Ni wapi naweza kupata tiba kwa njia ya Ozone wakuu?

Ozone ni tiba ambayo Oksijen Inatolewa Kwenye Mtungi Inapita Kwenye Mashine Inachakatwa Kuwa Ozone.

Wakati Huo Damu yako Inatolewa Mkonon Na Kupelekwa Kwe Mashine Ndogo Mpaka Kwe Tube Fulan.

Ile Ozone Inapitishwa Kwenye Mafuta Fulan Inaingia Kwenye Tube Yenye Damu , Damu Inatokea Upande Mwingne Inarudishwa Mwilini.

OZONE inatibu:

-kufubaza wadudu wa HIV na bacteria.

-husaidia wenye kisukari.

-inaondoa seli mbovu na kuunda upya.

-hurekebisha homoni.

Ninahitaji kufahamu ni wapi nitapata tiba hii hapa Tz...
JARIBU KUULIZIZ KWENYE HOSPITAL KUBWA KUBWA ZA PRIVATE
 
Ndio maana alikuwa anatafuta hii tiba... Jamani mbona wako watu wenye HIV na wanaishi. Je angekuwa na saratani?

anyway yeye anajua mwenyewe
 
Wana JamiiForums tupo kwaajili ya matani mengi na kebehi za hapa na pale, wachache ndo wanazingatia maumivu ya mtu na kutafuta namna ya kupata suluhisho.

Utakuta mtu Kama Miguu ya kuku anashida kubwa na anaandika kwa hisia Kali lakini watu wapo kwenye matani na kejeli za maneno mabaya na ya mikato, Yani hawajali chochote kile,Tena ukute ndo wanazidi kumtania kwa kumwambie aende kwa mganga wa kienyeji.

Hii si sahihi kabisa tunauana sisi wenyewe Kisha tunakuja kuandika R. I. P ishara ya kuguswa kumbe ni wauaji wakubwa, Jamani tufikie hatua tuthaminiane Kama ni matani Basi yabakie mahala pake na Mambo ya kuzingatia pia tuyape uzito mkubwa.

Huyu Miguu ya kuku alihitaji ushauri na maneno ya faraja Sana na pengine alihitaji kuwekwa sehemu ya jamii ili dhana mbaya imtoke na ajihisi mtu katika watu.

Post zake karibia zote zilikuwa za mashaka mno, alikuwa amekata tamaa na hata alipokuwa anaposti watu hatukuzingatia namna ya kutoa majibu mazuri, Sana Sana majibu yetu yalikuwa ya mkato tu, 'NENDA HOSPITALI ZA BINAFSI HUKO' Sasa haya ndo majibu ambayo yanastahili kutolewa kwa mtu mwenye uhitaji kweli?

Haya majibu na majibu mengine kwakweli hayakuwa ya kuridhisha.

Tupendane, tushauriane tupeane faraja na Kisha tusherekee maisha pamoja.

Apumzike panapostahili Miguu ya kuku.
Amina.

Ahsanteni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inasemekana na file is deceased.
Lakin je,kuna utaratibu gan wa ku confirm kama mtu kasha ndei au lah!!!?
 
Back
Top Bottom