meningitis
JF-Expert Member
- Nov 17, 2010
- 8,349
- 4,674
Dr Slaa hakukataa hivi hivi kudahili makapi ya CCM bila mpangilio.
Hii ni kwa sababu Dr Slaa alikuwa na mpango mkakati wa kuunda Chadema yenye nguvu kwa maslahi ya upinzani na watanzania kwa ujumla.
Jambo hili lisingeweza kufanikiwa kwa kutegemea makapi tena yenye sifa chafu kutoka CCM.jambo hili lilihitaji wanachama asili wanaounda chadema kutokea kwenye msingi.
Ilifaa kuwe na utaratibu maalumu zaidi ya biashara za kununuliwa katika kudahili oil chafu na makapi kutoka CCM.
Wengi wa wanachadema mamluki walidhania kuwa Slaa ni mbishi,asiyejua mahesabu au aliyehongwa na CCM.HIVYO maoni ya Slaa juu ya utaratibu wa kuchukua makapi ya CCM yalipuuzwa.
Juma Duni hajji aliondoka Chadema mara baada ya uchaguzi ilihali ushirika wa UKAWA ukisemekana bado upo...sasa kilichomtoa Chadema ni kipi??
Lawrance Masha anaondoka Chadema akitaja hoja za msingi kabisa kwamba yale aliyoyaamini kuwa yanafaa ndani ya Chadema sio ya kweli bali ni ujanja ujanja wa kula ruzuku za serikali na wafadhili tu.
Mwenyekiti Mbowe anatakiwa ajiuzulu kwa kwenda njia ya kushoto kabisa ukilinganisha na matarajio ya Chadema kama chama na matarajio ya wananchi kwa chadema.
Hoja ya kwamba kupigania demokrasia na haki inahitaji uvumilivu haimaanishi lawarance Masha ndio kakosa uvumilivu bali ni Chadema yenyewe iliyokosa pumzi ya kujiamini na kujisimamia bila utegemezi wa makapi ili kufikia tamati.
Chadema ya Mbowe inaamini kutuletea mabadiliko,kupigania haki na demokrasia nchini huku ikitaka kuwatumia wale wale tuliowasema wanakandamiza haki,mafisadi na wabadhirifu...Huu ni ujuha ambao hata mtoto mdogo anaushangaa.
Mwenyekiti Mbowe kubali kuwa umekosea sana kutaka kuipandisha Chadema kwa makapi yaliyotaka kusababisha CCM ife.
Leo hii ninafurahi sana kuona somo la kwanza kutoka kwa Masha linaandikwa na kusomwa...tuendelee kusubiri somo la pili na hatimaye injili takatifu.
Nategemea Kingunge...Sumaye...Makongoro na hatimaye lowassa kurejea CCM na watafanya hivyo hivi karibuni au baadaye katika wakati utakaoumiza sana.
Mwenyekiti Mbowe atupe sababu ya kwa nini wanachadema wanahama na sio kutubabaisha na porojo za watu kuhongwa kama ilivyokuwa kwa madiwani...Masha hajahongwa ameamua kidemokrasia kabisa hata katibu Mashinji amekiri hivyo.
CCM ilipata tiketi ya kutawala milele mwaka 2015 kwa uzembe au makusudi ya Mbowe.
Hii ni kwa sababu Dr Slaa alikuwa na mpango mkakati wa kuunda Chadema yenye nguvu kwa maslahi ya upinzani na watanzania kwa ujumla.
Jambo hili lisingeweza kufanikiwa kwa kutegemea makapi tena yenye sifa chafu kutoka CCM.jambo hili lilihitaji wanachama asili wanaounda chadema kutokea kwenye msingi.
Ilifaa kuwe na utaratibu maalumu zaidi ya biashara za kununuliwa katika kudahili oil chafu na makapi kutoka CCM.
Wengi wa wanachadema mamluki walidhania kuwa Slaa ni mbishi,asiyejua mahesabu au aliyehongwa na CCM.HIVYO maoni ya Slaa juu ya utaratibu wa kuchukua makapi ya CCM yalipuuzwa.
Juma Duni hajji aliondoka Chadema mara baada ya uchaguzi ilihali ushirika wa UKAWA ukisemekana bado upo...sasa kilichomtoa Chadema ni kipi??
Lawrance Masha anaondoka Chadema akitaja hoja za msingi kabisa kwamba yale aliyoyaamini kuwa yanafaa ndani ya Chadema sio ya kweli bali ni ujanja ujanja wa kula ruzuku za serikali na wafadhili tu.
Mwenyekiti Mbowe anatakiwa ajiuzulu kwa kwenda njia ya kushoto kabisa ukilinganisha na matarajio ya Chadema kama chama na matarajio ya wananchi kwa chadema.
Hoja ya kwamba kupigania demokrasia na haki inahitaji uvumilivu haimaanishi lawarance Masha ndio kakosa uvumilivu bali ni Chadema yenyewe iliyokosa pumzi ya kujiamini na kujisimamia bila utegemezi wa makapi ili kufikia tamati.
Chadema ya Mbowe inaamini kutuletea mabadiliko,kupigania haki na demokrasia nchini huku ikitaka kuwatumia wale wale tuliowasema wanakandamiza haki,mafisadi na wabadhirifu...Huu ni ujuha ambao hata mtoto mdogo anaushangaa.
Mwenyekiti Mbowe kubali kuwa umekosea sana kutaka kuipandisha Chadema kwa makapi yaliyotaka kusababisha CCM ife.
Leo hii ninafurahi sana kuona somo la kwanza kutoka kwa Masha linaandikwa na kusomwa...tuendelee kusubiri somo la pili na hatimaye injili takatifu.
Nategemea Kingunge...Sumaye...Makongoro na hatimaye lowassa kurejea CCM na watafanya hivyo hivi karibuni au baadaye katika wakati utakaoumiza sana.
Mwenyekiti Mbowe atupe sababu ya kwa nini wanachadema wanahama na sio kutubabaisha na porojo za watu kuhongwa kama ilivyokuwa kwa madiwani...Masha hajahongwa ameamua kidemokrasia kabisa hata katibu Mashinji amekiri hivyo.
CCM ilipata tiketi ya kutawala milele mwaka 2015 kwa uzembe au makusudi ya Mbowe.