Ni wakati wa kutoa ultimatum kwa watawala, bila Katiba Mpya ya wananchi hakuna uchaguzi

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,491
40,999
Ifike wakati Watanzania tutoe amri kwa watawala kwamba kama hakuna katiba mpya, hakuna uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2024, wala uchaguzi mkuu mwaka 2025.

Nchi hii ni ya Watanzania. Watanzania ndio wanaotakiwa kuwa na maamuzi ya namna gani wanataka nchi yao ifanye kila kitu.

Katiba hii ambayo Baba wa Taifa alisema inamfanya Rais kuwa dikteta sasa ifike mwisho. Rais anatakiwa kupewa mwongozo tuliokubaliana namna anavyotakiwa kutuongoza, na siyo yeye kutupangia namna anavyotaka kututawala kama ilivyo sasa.

Leo hii kila kitu ni Rais, kama vile nchi ni ya Rais. Kodi ni ya mwananchi, lakini Rais ndiye anakuletea mkurugenzi kuja kusimamia matumizi ya pesa yako. Hata ukiona huyo mkurugenzi anaiba, wewe unayetoa pesa huna uamuzi, mpaka aliyemteua apende, asipopenda, mteule wake anaendelea kutafuta pesa ya wananchi na hamna uwezo wa kumfanya chochote.

Fikiria, mpaka pesa ya wananchi, siku hizi inatajwa kuwa ni pesa ya Rais, eti Rais emetoa bilioni kadhaa kwaajiki ya ujenzi wa kisima, zahanati, shule, n.k.

Hata huko kwenye mataifa yenye katiba nzuri, sheria nzuri na mifumo mizuri ya utawala, siyo kwamba watawala walikuwa malaika, bali pressure ya wananchi iliwalazimisha watawala kukubali matakwa ya wananchi.

Kwa kuwa Serikali inalegalega, na kupiga danadana nyingi kuhusiana na suala la katiba nzuri mpya, katiba ya wananchi, lazima nguvu ya wananchi ishike hatamu, na Serikali ilazimishwe kufuata matakwa ya wananchi.

Na kwenye hili wananchi tushikamane, tuache mambo ya uCHADEMA, uCCM, uCUF, uACT, au tofauti zile nyingine za kijinga eti huyu ni sukuma gang, yule ni msoga gang, nasema huo ni upuuzi, sote tuunganishwe na utaifa wetu.

Leo mmesikia kuwa TANESCO, inayoendeshwa kwa ruzuku ya Serikali ya bara (nishati siyo suala la muungano) imesamehe deni la zaidi ya shilingi bilioni 60 iliyokuwa ikiidai Zanzibar. Hizi ni pesa za wananchi walipa kodi. Msamaha huo umetolewa kwa namna gani? Ni utaratibu upi uliofuatwa? Ni nani aliyetoa uamuzi wa kusamehe hilo deni? Ana mamlaka hayo?

Mambo haya inawezekana yanafanywa ama kwa shinikizo ama kwa kujipendekeza kwa Rais kwa sababu ni mzanzibari. Hatupingi kusamehe deni, tena kwa sehemu mojawapo ya muungano au kutoa msaada inapolazimu, lakini ni utaratibu upi umefuatwa kwa shirika linaloendesha kwa pesa za walipa kodi kuweza kufuta deni? Mbona hatujawahi kusikia kuwa TANESCO imewafutia deni wadaiwa sugu wa huku bara?

Katiba mpya itayaweka haya mambo yote wazi, na kuweka taratibu zilizokubalika na ambazo kila mmoja, na hasa viongozi, watatakiwa kufuata.

Hii ya kila kitu Rais, haikubaliki kabisa kwa namna yoyote ile. Kwenye teuzi, Rais aishie kuwateua mawaziri tu ambao wataidhinishwa na wabunge. Wengine wote waajiriwe au wachaguliwe. Wakivurunda, mamlaka za uajiri ziwafukuze kiurahisi.

Katiba siyo ya akina Lisu na Mbowe, siyo ya Rais wala Mutungi, siyo ya Chongolo, bali ni ya Watanzania wote. Yeyote anayetaka kujimilikisha uandaaji wa katiba ni adui yetu sote. Yeyote anayetaka kutushirikisha sote kwenye kupata katiba tunayoitaka, ni mzalendo wa Taifa letu, ni mtu mwenye upendo kwa Watanzania wa leo na vizazi vijavyo, na huyo ndiye tuandamane naye.

Hatutaki katiba maslahi ya watawala au wanasiasa tu, bali katiba itakayompa mamlaka makubwa mwananchi.
 
Nafikiri rais hana nguvu ya kuamua kuhusu katiba mpya,bali waliomuweka madarakani (kundi la watu wachache wenye ukwasi na sauti),ambao kupitia katiba hii wananufaika sana,hivyo rais huwasikiliza hao jamaa.

Je,hivi vyama maslahi (CCM B),vitagomea uchaguzi?
 
Ni muda wa kuirudisha rasimu ya Jaji Warioba mezani maana ndo imesheeni maoni ya wananchi wa pande zote mbili ili kila mmoja afaidike na keki ya taifa maana taifa let tumekuwa na viongozi wabinafsi ( na hii ni hulka na tabia ya waafrika) ndio maana Kuna wizara imepitisha bajeti ya 47b ili kulipana posho

"Katiba ni mali ya umma anayepinga juhudi ya kupatikana kwa katiba mpya ni adui wa umma"
 
Ifike wakati Watanzania tutoe amri kwa watawala kwamba kama hakuna katiba mpya, hakuna uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2024, wala uchaguzi mkuu mwaka 2025.
Maadam Mama ameamua kutumia njia ya majadiliano, tumpe ushirikiano, tumpe muda na sio amri!
Nchi hii ni ya Watanzania. Watanzania ndio wanaotakiwa kuwa na maamuzi ya namna gani wanataka nchi yao ifanye kila kitu.
Ni kweli, nchi ni mali ya wananchi na ndio wenye katiba iliyompa kiongozi wao mamlaka yote.
Katiba hii ambayo Baba wa Taifa alisema inamfanya Rais kuwa dikteta sasa ifike mwisho.
Kwa vile tayari ipo, ili ifike mwisho ni lazima Watanzania tuitane ndipo tuitamatishe na ndicho anachofanya sasa Rais Samia
Rais anatakiwa kupewa mwongozo tuliokubaliana namna anavyotakiwa kutuongoza, na siyo yeye kutupangia namna anavyotaka kututawala kama ilivyo sasa.
Kiukweli kabisa wengi hawaijui katiba, yote Samia anayoyafanya ni kwa mujibu wa katiba!. Kwa bahati nzuri sana, humu jf, tupo baadhi yetu tunaijua katiba na tukaamua kujitolea kuwafundisha wengine kuhusu katiba, angalia response ya members humu kwenye somo hili Ijue Katiba ya JMT-1: Katiba ni nini, ya nani, ya kazi gani? Msemo "Katiba ndio ila kitu" Una maana gani? Katiba ina umuhimu gani?
Kwa mujibu wa katiba yetu, imempa mamlaka rais wa JMT atafikia maamuzi yeye kama yeye bila kufuata ushauri wa yeyote!.
Leo hii kila kitu ni Rais, kama vile nchi ni ya Rais.
Kwa mujibu wa katiba yetu, rais wa Tanzania ni executive president, hivyo kila kitu ni rais, na watendaji wote wa serikali Wanafanya kila kitu kwa niaba ya rais.
Hata huko kwenye mataifa yenye katiba nzuri, sheria nzuri na mifumo mizuri ya utawala, siyo kwamba watawala walikuwa malaika, bali pressure ya wananchi iliwalazimisha watawala kukubali matakwa ya wananchi.
Naunga mkono hoja.
Kwa kuwa Serikali inalegalega, na kupiga danadana nyingi kuhusiana na suala la katiba nzuri mpya, katiba ya wananchi, lazima nguvu ya wananchi ishike hatamu, na Serikali ilazimishwe kufuata matakwa ya wananchi.
Mbona Mama ameruhusu mchakato uanze!.
Na kwenye hili wananchi tushikamane, tuache mambo ya uCHADEMA, uCCM, uCUF, uACT, au tofauti zile nyingine za kijinga eti huyu ni sukuma gang, yule ni msoga gang, nasema huo ni upuuzi, sote tuunganishwe na utaifa wetu.
Naunga mkono hoja
Leo mmesikia kuwa TANESCO, inayoendeshwa kwa ruzuku ya Serikali ya bara (nishati siyo suala la muungano) imesamehe deni la zaidi ya shilingi bilioni 60 iliyokuwa ikiidai Zanzibar. Hizi ni pesa za wananchi walipa kodi. Msamaha huo umetolewa kwa namna gani? Ni utaratibu upi uliofuatwa? Ni nani aliyetoa uamuzi wa kusamehe hilo deni? Ana mamlaka hayo?
Japo sijaifuatilia hii ila atakuwa ni Mama, she has all the powers vested on her kwa mujibu wa katiba.
Mambo haya inawezekana yanafanywa ama kwa shinikizo ama kwa kujipendekeza kwa Rais kwa sababu ni mzanzibari. Hatupingi kusamehe deni, tena kwa sehemu mojawapo ya muungano au kutoa msaada inapolazimu, lakini ni utaratibu upi umefuatwa kwa shirika linaloendesha kwa pesa za walipa kodi kuweza kufuta deni? Mbona hatujawahi kusikia kuwa TANESCO imewafutia deni wadaiwa sugu wa huku bara?
Hili neno!.
Katiba mpya itayaweka haya mambo yote wazi, na kuweka taratibu zilizokubalika na ambazo kila mmoja, na hasa viongozi, watatakiwa kufuata.
Naunga mkono hoja
Hii ya kila kitu Rais, haikubaliki kabisa kwa namna yoyote ile. Kwenye teuzi, Rais aishie kuwateua mawaziri tu ambao wataidhinishwa na wabunge. Wengine wote waajiriwe au wachaguliwe. Wakivurunda, mamlaka za uajiri ziwafukuze kiurahisi.
Naunga mkono hoja, hata mimi hili niliwahi kushauri humu Should We Demand More Right to Information Kwenye Teuzi za Key Posts? Ziwe Endorsed na Bunge With Security of Tenure? Mawaziri Wasiwe Wabunge?
Katiba siyo ya akina Lisu na Mbowe, siyo ya Rais wala Mutungi, siyo ya Chongolo, bali ni ya Watanzania wote. Yeyote anayetaka kujimilikisha uandaaji wa katiba ni adui yetu sote.
Naunga mkono
Yeyote anayetaka kutushirikisha sote kwenye kupata katiba tunayoitaka, ni mzalendo wa Taifa letu, ni mtu mwenye upendo kwa Watanzania wa leo na vizazi vijavyo, na huyo ndiye tuandamane naye.
Hiki ndicho anachokifanya Mama
Hatutaki katiba maslahi ya watawala au wanasiasa tu, bali katiba itakayompa mamlaka makubwa mwananchi.
Naunga mkono hoja
P
 
Labda wasisitizie na kukazia zaidi.

Binafsi sijawahi kusikia kauli hiyo ya "Bila Katiba Mpya Hakuna Uchaguzi" wakiikana CHADEMA, hata kwenye hayo mazungumzo ya maridhiano.

Kinachotakiwa sasa ni kukumbushia hilo, kwamba hata kama walinyamaza kidogo, sasa ajenda hiyo imerudi juu kabisa zaidi ya ajenda nyingine yoyote.
Na tokea sasa, hiyo ndiyo iwe sala yao katika kila mkutano watakaoufanya nchini kote.

Walitegeshewa kichaka na mama Tozo, kidogo kichaka hicho kilitaka kuwameza.

Na ifahamike wazi hapa, kazi ngumu siyo hiyo ya "Kutangaza, 'ultimatum' kazi muhimu ni kuhakikisha 'ultimatum' hiyo haidharauliwi na kupuuzwa.

Kwa hiyo CHADEMA ni lazima wajipange tokea sasa kuhakikisha kwamba 'ultimatum' hiyo itakapohitaji kutekelezwa, itafanyika kwa ufanisi mkubwa. Hapa ndipo palipo na kazi inayowasubili.
 
Wazee wetu huwa na jicho la ndani la kuona mbali naomba kukuuliza swali mkuu PM je,rais SSH ana nia ya dhati kabisa ya kuipatia Tanzania uKatiba mpya ?
Mkuu Kinkunti El Perdedo , SSH ana nia ya kweli kabisa na ya dhati kutupatia katiba mpya na hili nimelisema sana humu Ikitokea umeshauri mtu avae Hijab nyekundu, huyo mtu akavaa, utajisikiaje? Kwa hili, Big Up Rais Samia na Serikali yako kwa kuwa wasikivu
Na vipi kuhusu Chama chake kina nia pia hiyo hiyo ?
Japo watu humu wanawatania Chadema ni manyumbu!, hakuna manyumbu wakubwa kama CCM, kwasababu manyumbu wa Chadema ni wanachama tuu lakini manyumbu wa CCM ni hadi viongozi!. Rais Samia ndie Mwenyekiti wa CCM, akiishaonyesha nia na kusema, hakuna anayekohoa, japo kuna wahafidhina wa chini kwa chini, hawa wanaendeleza kusafishwa!.

Nimewaita CCM ni manyumbu wakubwa kuliko Chadema, kwasababu, ile 2015 hoja ya katiba mpya ilikuwepo kwenye ilani ya CCM, Mwenyekiti aliposema sio kipaumbele changu!, wote walinyamaza!, nikawauliza Kitendo cha Kukiuka Ilani ya CCM Bila Kikao Chochote, Sio Udikiteta?
P
 
Ni muda wa kuirudisha rasimu ya Jaji Warioba mezani maana ndo imesheeni maoni ya wananchi wa pande zote mbili ili kila mmoja afaidike na keki ya taifa maana taifa let tumekuwa na viongozi wabinafsi ( na hii ni hulka na tabia ya waafrika) ndio maana Kuna wizara imepitisha bajeti ya 47b ili kulipana posho

"Katiba ni mali ya umma anayepinga juhudi ya kupatikana kwa katiba mpya ni adui wa umma"
Point of correction: Kuna Rasimu na Katiba iliyopendekezwa iliyotoka Oktoba, 2014! Usichanganye hapo!

Kwanini tuirudishe uliyoitaja 'Rasimu'? Wakati mazingira ya kisiasa, kiuchumi, kimfumo na hata kijamii yamebadilika? Ningedhani hoja yako ingekua na mashiko kama unge propose mchakato uanze upyaaa!

Unakumbuka makundi ya uwakilishi kwenye Bunge Maalum? Wavuvi, wafugaji nk? 60% ya waliokua wakitajwa kuwa wawakilishi wa makundi hawakua na lolote zaidi ya kupachikwa na vyama fulani fulani!

Ni namna gani mchakato huu hasa kwenye makundi ya uwakilishi utakua wa wazi? Binafsi nawafahamu watu fulani ambao hata kuku hawakua nao ila leo ni watu wazito!

Hebu tushirikiane kwa mijadala kama hii ya kufumbua bongo za Watanzania! Kuna tatizo mahali..unajua ni lipi? FIKRA!
 
Wazee wetu huwa na jicho la ndani la kuona mbali naomba kukuuliza swali mkuu PM je,rais SSH ana nia ya dhati kabisa ya kuipatia Tanzania Katiba mpya ? Na vipi kuhusu Chama chake kina nia pia hiyo hiyo ?
Hivi uliwahi kujiuliza pale Katibu Mkuu wa CCM anapoiagiza serikali itekeleze hili ama lile hua ana muagiza nani? Boss wa anayetoa tamko lake ni nani? Mkuu wa Serikali ni Nani? Na huyo Boss ana tittle kadhaa, kwahiyo 'Boss anajiagiza' sio? Its crazy
 
Katiba hii ambayo Baba wa Taifa alisema inamfanya Rais kuwa dikteta sasa ifike mwisho. Rais anatakiwa kupewa mwongozo tuliokubaliana namna anavyotakiwa kutuongoza, na siyo yeye kutupangia namna anavyotaka kututawala kama ilivyo sasa.
Dah!

Mkuu 'Bams', naona leo umekula pilipili kali!

Hiyo mistari miwili niliyoinyanyua, nisingeweza kupata maneno fasaha kabisa ya kuwasilisha maneno hayo kama ulivyofanya hapa.

Lakini ni budi niseme, hata wakati wa Mwalimu Nyerere ilipokuwa Katiba hii inatumika bila kuhojiwa, si angalau huko kwenye chama chao cha CCM kulikuwa na uvuguvugu kidogo, ambako mambo yaliamuriwa kwenye vikao baada ya mijadala ya kutosha, na watu kutoa dukuduku zao kwenye mambo walivyoyaona.

Leo hii Mwenyekiti wa Chama, ambaye ndiye huyo huyo mkuu wa nchi, ndiye anayemaliza kila jambo bila ya mjadala wowote wala kuhojiwa na yeyote.
Hii inatokana na mtu huyo huyo mmoja ndiye anayempa ulaji mtu aliyeko kwenye chama au serikalini.

Kila mtu analinda maslahi ya tumbo lake kwanza na mwisho.
Rais mwenyewe yupo, hana uchungu wowote na nchi anayoiongoza. Hapo utategemea kitu gani?
 
Kwanini tuirudishe uliyoitaja 'Rasimu'? Wakati mazingira ya kisiasa, kiuchumi, kimfumo na hata kijamii yamebadilika?
Sielewi una maana gani hapa.
Tanzania hii hii imebadilika haraka kiasi hicho katika maswala hayo? Imebadilika kwa vipi, kwa kwenda mbele zaidi, na kuwa mazuri, au imebadilika kwa kurudi nyuma sana kuliko tulipokuwa tumefikia wakati huo?

Wewe ungependa lipi lifanyike (tuanzie wapi) ili Katiba Mpya ipatikane, au ni mmoja wa hao wasioona maana yoyote ya uwepo wa Katiba Mpya?
 
Sielewi una maana gani hapa.
Tanzania hii hii imebadilika haraka kiasi hicho katika maswala hayo? Imebadilika kwa vipi, kwa kwenda mbele zaidi, na kuwa mazuri, au imebadilika kwa kurudi nyuma sana kuliko tulipokuwa tumefikia wakati huo?

Wewe ungependa lipi lifanyike (tuanzie wapi) ili Katiba Mpya ipatikane, au ni mmoja wa hao wasioona maana yoyote ya uwepo wa Katiba Mpya?
Mahitaji yako ya 2012-2014 na leo 2023 ni sawa?? Bajeti uliyokua ukiacha nyumbani wakati huo na mdumuko wa bei wa sasa unahisi kiwango kile kile kitakidhi mahitaji kama yale na zaidi? Utakua na tatizo.

Para yako ya mwisho unataka kuni provoke nile ban tu! Ningekua na hayo unayodhani nisingehoji maswali ambayo kimsingi HUNA MAJIBU!

Majibu yangu ya juu yanajitosheleza! Soma rudia na uelewe
 
Hata huko kwenye mataifa yenye katiba nzuri, sheria nzuri na mifumo mizuri ya utawala, siyo kwamba watawala walikuwa malaika, bali pressure ya wananchi iliwalazimisha watawala kukubali matakwa ya wananchi.
Kasoro Marekani (USA); lakini hata wao, kuna mambo mengi sana waliyolazimishwa na matakwa ya wananchi, na serkali ikatii. Hapa kwetu ni serikali( hapana Rais) ndiyo inayotuamrisha tufanye nini!
 
Mahitaji yako ya 2012-2014 na leo 2023 ni sawa?? Bajeti uliyokua ukiacha nyumbani wakati huo na mdumuko wa bei wa sasa unahisi kiwango kile kile kitakidhi mahitaji kama yale na zaidi? Utakua na tatizo.

Para yako ya mwisho unataka kuni provoke nile ban tu! Ningekua na hayo unayodhani nisingehoji maswali ambayo kimsingi HUNA MAJIBU!

Majibu yangu ya juu yanajitosheleza! Soma rudia na uelewe
Nipe mfano wa bajeti ilivyohusishwa kwenye hayo maswala ya Rasimu yalivyokuwa wakati huo na kuwa tofauti na hali hii ya leo.
Usiifanye shughuli ya kutayarisha katiba iwe ya muda maalum, tena muda mfupi kiasi hicho. Inawezekana ukawa huelewi maana ya katiba ni nini.,
 
Ifike wakati Watanzania tutoe amri kwa watawala kwamba kama hakuna katiba mpya, hakuna uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2024, wala uchaguzi mkuu mwaka 2025.

Nchi hii ni ya Watanzania. Watanzania ndio wanaotakiwa kuwa na maamuzi ya namna gani wanataka nchi yao ifanye kila kitu.

Katiba hii ambayo Baba wa Taifa alisema inamfanya Rais kuwa dikteta sasa ifike mwisho. Rais anatakiwa kupewa mwongozo tuliokubaliana namna anavyotakiwa kutuongoza, na siyo yeye kutupangia namna anavyotaka kututawala kama ilivyo sasa.

Leo hii kila kitu ni Rais, kama vile nchi ni ya Rais. Kodi ni ya mwananchi, lakini Rais ndiye anakuletea mkurugenzi kuja kusimamia matumizi ya pesa yako. Hata ukiona huyo mkurugenzi anaiba, wewe unayetoa pesa huna uamuzi, mpaka aliyemteua apende, asipopenda, mteule wake anaendelea kutafuta pesa ya wananchi na hamna uwezo wa kumfanya chochote.

Fikiria, mpaka pesa ya wananchi, siku hizi inatajwa kuwa ni pesa ya Rais, eti Rais emetoa bilioni kadhaa kwaajiki ya ujenzi wa kisima, zahanati, shule, n.k.

Hata huko kwenye mataifa yenye katiba nzuri, sheria nzuri na mifumo mizuri ya utawala, siyo kwamba watawala walikuwa malaika, bali pressure ya wananchi iliwalazimisha watawala kukubali matakwa ya wananchi.

Kwa kuwa Serikali inalegalega, na kupiga danadana nyingi kuhusiana na suala la katiba nzuri mpya, katiba ya wananchi, lazima nguvu ya wananchi ishike hatamu, na Serikali ilazimishwe kufuata matakwa ya wananchi.

Na kwenye hili wananchi tushikamane, tuache mambo ya uCHADEMA, uCCM, uCUF, uACT, au tofauti zile nyingine za kijinga eti huyu ni sukuma gang, yule ni msoga gang, nasema huo ni upuuzi, sote tuunganishwe na utaifa wetu.

Leo mmesikia kuwa TANESCO, inayoendeshwa kwa ruzuku ya Serikali ya bara (nishati siyo suala la muungano) imesamehe deni la zaidi ya shilingi bilioni 60 iliyokuwa ikiidai Zanzibar. Hizi ni pesa za wananchi walipa kodi. Msamaha huo umetolewa kwa namna gani? Ni utaratibu upi uliofuatwa? Ni nani aliyetoa uamuzi wa kusamehe hilo deni? Ana mamlaka hayo?

Mambo haya inawezekana yanafanywa ama kwa shinikizo ama kwa kujipendekeza kwa Rais kwa sababu ni mzanzibari. Hatupingi kusamehe deni, tena kwa sehemu mojawapo ya muungano au kutoa msaada inapolazimu, lakini ni utaratibu upi umefuatwa kwa shirika linaloendesha kwa pesa za walipa kodi kuweza kufuta deni? Mbona hatujawahi kusikia kuwa TANESCO imewafutia deni wadaiwa sugu wa huku bara?

Katiba mpya itayaweka haya mambo yote wazi, na kuweka taratibu zilizokubalika na ambazo kila mmoja, na hasa viongozi, watatakiwa kufuata.

Hii ya kila kitu Rais, haikubaliki kabisa kwa namna yoyote ile. Kwenye teuzi, Rais aishie kuwateua mawaziri tu ambao wataidhinishwa na wabunge. Wengine wote waajiriwe au wachaguliwe. Wakivurunda, mamlaka za uajiri ziwafukuze kiurahisi.

Katiba siyo ya akina Lisu na Mbowe, siyo ya Rais wala Mutungi, siyo ya Chongolo, bali ni ya Watanzania wote. Yeyote anayetaka kujimilikisha uandaaji wa katiba ni adui yetu sote. Yeyote anayetaka kutushirikisha sote kwenye kupata katiba tunayoitaka, ni mzalendo wa Taifa letu, ni mtu mwenye upendo kwa Watanzania wa leo na vizazi vijavyo, na huyo ndiye tuandamane naye.

Hatutaki katiba maslahi ya watawala au wanasiasa tu, bali katiba itakayompa mamlaka makubwa mwananchi.
Naomba kuuliza ,Katiba Mpya inayozungumziwa ni ya kuwapa Wananchi mamlaka au ya kuwapunguzia ccm mamlaka na kuwapa wezi wengine in the name of Chadema?

Maana nimesikia somewhere kwamba ati Vyama vya siasa ndio vipendekeze Wataalamu wa kuandika Katiba,kuliko kuandika Katiba ya Wanasiasa Bora tubakie hivi hivi.
 
Kwanza tujiulize, hiyo ultimatum itatolewa na wananchi gani? kumbuka wakati uchaguzi mkuu ukikaribia kuna vile vyama rafiki vya CCM vitaungana nao kushiriki uchaguzi, hivi kwa namna fulani vitasababisha kuhalalisha madai kwamba uchaguzi ulikuwa huru na haki kwa hii Katiba mbovu iliyopo.

Sasa unapozungumzia pawepo ultimatum, vyema tujiulize, hii ultimatum itaanzia wapi na kuishia wapi? ni wakina nani watakaokuwa wahusika wake? lakini pia, vipi kwa wale wengine ambao hawatataka kuhusishwa, wasipofanya hivyo wataonekana wabaya kwa lipi, kama wameamua kufanya hivyo kwa hiyari yao?

Utekelezaji wa hii ultimatum kwa mtazamo wangu, naona nao utakuwa mgumu kama ambavyo tunahangaika sasa hivi na hii michakato ya kuipata Katiba Mpya isiyokwisha, wala kujua Katiba Mpya yenyewe itakayopatikana itakuwa ya sampuli gani, naona kila tunapogusa bado safari yetu ni ndefu sana inayoendelea kuwanufaisha CCM.
 
Ifike wakati Watanzania tutoe amri kwa watawala kwamba kama hakuna katiba mpya, hakuna uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2024, wala uchaguzi mkuu mwaka 2025.

Nchi hii ni ya Watanzania. Watanzania ndio wanaotakiwa kuwa na maamuzi ya namna gani wanataka nchi yao ifanye kila kitu.

Katiba hii ambayo Baba wa Taifa alisema inamfanya Rais kuwa dikteta sasa ifike mwisho. Rais anatakiwa kupewa mwongozo tuliokubaliana namna anavyotakiwa kutuongoza, na siyo yeye kutupangia namna anavyotaka kututawala kama ilivyo sasa.

Leo hii kila kitu ni Rais, kama vile nchi ni ya Rais. Kodi ni ya mwananchi, lakini Rais ndiye anakuletea mkurugenzi kuja kusimamia matumizi ya pesa yako. Hata ukiona huyo mkurugenzi anaiba, wewe unayetoa pesa huna uamuzi, mpaka aliyemteua apende, asipopenda, mteule wake anaendelea kutafuta pesa ya wananchi na hamna uwezo wa kumfanya chochote.

Fikiria, mpaka pesa ya wananchi, siku hizi inatajwa kuwa ni pesa ya Rais, eti Rais emetoa bilioni kadhaa kwaajiki ya ujenzi wa kisima, zahanati, shule, n.k.

Hata huko kwenye mataifa yenye katiba nzuri, sheria nzuri na mifumo mizuri ya utawala, siyo kwamba watawala walikuwa malaika, bali pressure ya wananchi iliwalazimisha watawala kukubali matakwa ya wananchi.

Kwa kuwa Serikali inalegalega, na kupiga danadana nyingi kuhusiana na suala la katiba nzuri mpya, katiba ya wananchi, lazima nguvu ya wananchi ishike hatamu, na Serikali ilazimishwe kufuata matakwa ya wananchi.

Na kwenye hili wananchi tushikamane, tuache mambo ya uCHADEMA, uCCM, uCUF, uACT, au tofauti zile nyingine za kijinga eti huyu ni sukuma gang, yule ni msoga gang, nasema huo ni upuuzi, sote tuunganishwe na utaifa wetu.

Leo mmesikia kuwa TANESCO, inayoendeshwa kwa ruzuku ya Serikali ya bara (nishati siyo suala la muungano) imesamehe deni la zaidi ya shilingi bilioni 60 iliyokuwa ikiidai Zanzibar. Hizi ni pesa za wananchi walipa kodi. Msamaha huo umetolewa kwa namna gani? Ni utaratibu upi uliofuatwa? Ni nani aliyetoa uamuzi wa kusamehe hilo deni? Ana mamlaka hayo?

Mambo haya inawezekana yanafanywa ama kwa shinikizo ama kwa kujipendekeza kwa Rais kwa sababu ni mzanzibari. Hatupingi kusamehe deni, tena kwa sehemu mojawapo ya muungano au kutoa msaada inapolazimu, lakini ni utaratibu upi umefuatwa kwa shirika linaloendesha kwa pesa za walipa kodi kuweza kufuta deni? Mbona hatujawahi kusikia kuwa TANESCO imewafutia deni wadaiwa sugu wa huku bara?

Katiba mpya itayaweka haya mambo yote wazi, na kuweka taratibu zilizokubalika na ambazo kila mmoja, na hasa viongozi, watatakiwa kufuata.

Hii ya kila kitu Rais, haikubaliki kabisa kwa namna yoyote ile. Kwenye teuzi, Rais aishie kuwateua mawaziri tu ambao wataidhinishwa na wabunge. Wengine wote waajiriwe au wachaguliwe. Wakivurunda, mamlaka za uajiri ziwafukuze kiurahisi.

Katiba siyo ya akina Lisu na Mbowe, siyo ya Rais wala Mutungi, siyo ya Chongolo, bali ni ya Watanzania wote. Yeyote anayetaka kujimilikisha uandaaji wa katiba ni adui yetu sote. Yeyote anayetaka kutushirikisha sote kwenye kupata katiba tunayoitaka, ni mzalendo wa Taifa letu, ni mtu mwenye upendo kwa Watanzania wa leo na vizazi vijavyo, na huyo ndiye tuandamane naye.

Hatutaki katiba maslahi ya watawala au wanasiasa tu, bali katiba itakayompa mamlaka makubwa mwananchi.
Naunga mkono, hojayako niyakizalendo na umeongea ukweli mtupu na ndio tunacho takiwa kufanya.

Katiba kwa sasa ni muhimu kuliko kitu chochote.
 
Kongole nyingi kwako mkuu, mada yako imejaa madini matupu kutokana na matakwa ya wakati. Nukuu zifuatazo hapo chini zinahitaji maua,

"Katiba siyo ya akina Lisu na Mbowe, siyo ya Rais wala Mutungi, siyo ya Chongolo, bali ni ya Watanzania wote. Yeyote anayetaka kujimilikisha uandaaji wa katiba ni adui yetu sote. Yeyote anayetaka kutushirikisha sote kwenye kupata katiba tunayoitaka, ni mzalendo wa Taifa letu, ni mtu mwenye upendo kwa Watanzania wa leo na vizazi vijavyo, na huyo ndiye tuandamane naye"
Ifike wakati Watanzania tutoe amri kwa watawala kwamba kama hakuna katiba mpya, hakuna uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2024, wala uchaguzi mkuu mwaka 2025.

Nchi hii ni ya Watanzania. Watanzania ndio wanaotakiwa kuwa na maamuzi ya namna gani wanataka nchi yao ifanye kila kitu.

Katiba hii ambayo Baba wa Taifa alisema inamfanya Rais kuwa dikteta sasa ifike mwisho. Rais anatakiwa kupewa mwongozo tuliokubaliana namna anavyotakiwa kutuongoza, na siyo yeye kutupangia namna anavyotaka kututawala kama ilivyo sasa.

Leo hii kila kitu ni Rais, kama vile nchi ni ya Rais. Kodi ni ya mwananchi, lakini Rais ndiye anakuletea mkurugenzi kuja kusimamia matumizi ya pesa yako. Hata ukiona huyo mkurugenzi anaiba, wewe unayetoa pesa huna uamuzi, mpaka aliyemteua apende, asipopenda, mteule wake anaendelea kutafuta pesa ya wananchi na hamna uwezo wa kumfanya chochote.

Fikiria, mpaka pesa ya wananchi, siku hizi inatajwa kuwa ni pesa ya Rais, eti Rais emetoa bilioni kadhaa kwaajiki ya ujenzi wa kisima, zahanati, shule, n.k.

Hata huko kwenye mataifa yenye katiba nzuri, sheria nzuri na mifumo mizuri ya utawala, siyo kwamba watawala walikuwa malaika, bali pressure ya wananchi iliwalazimisha watawala kukubali matakwa ya wananchi.

Kwa kuwa Serikali inalegalega, na kupiga danadana nyingi kuhusiana na suala la katiba nzuri mpya, katiba ya wananchi, lazima nguvu ya wananchi ishike hatamu, na Serikali ilazimishwe kufuata matakwa ya wananchi.

Na kwenye hili wananchi tushikamane, tuache mambo ya uCHADEMA, uCCM, uCUF, uACT, au tofauti zile nyingine za kijinga eti huyu ni sukuma gang, yule ni msoga gang, nasema huo ni upuuzi, sote tuunganishwe na utaifa wetu.

Leo mmesikia kuwa TANESCO, inayoendeshwa kwa ruzuku ya Serikali ya bara (nishati siyo suala la muungano) imesamehe deni la zaidi ya shilingi bilioni 60 iliyokuwa ikiidai Zanzibar. Hizi ni pesa za wananchi walipa kodi. Msamaha huo umetolewa kwa namna gani? Ni utaratibu upi uliofuatwa? Ni nani aliyetoa uamuzi wa kusamehe hilo deni? Ana mamlaka hayo?

Mambo haya inawezekana yanafanywa ama kwa shinikizo ama kwa kujipendekeza kwa Rais kwa sababu ni mzanzibari. Hatupingi kusamehe deni, tena kwa sehemu mojawapo ya muungano au kutoa msaada inapolazimu, lakini ni utaratibu upi umefuatwa kwa shirika linaloendesha kwa pesa za walipa kodi kuweza kufuta deni? Mbona hatujawahi kusikia kuwa TANESCO imewafutia deni wadaiwa sugu wa huku bara?

Katiba mpya itayaweka haya mambo yote wazi, na kuweka taratibu zilizokubalika na ambazo kila mmoja, na hasa viongozi, watatakiwa kufuata.

Hii ya kila kitu Rais, haikubaliki kabisa kwa namna yoyote ile. Kwenye teuzi, Rais aishie kuwateua mawaziri tu ambao wataidhinishwa na wabunge. Wengine wote waajiriwe au wachaguliwe. Wakivurunda, mamlaka za uajiri ziwafukuze kiurahisi.

Katiba siyo ya akina Lisu na Mbowe, siyo ya Rais wala Mutungi, siyo ya Chongolo, bali ni ya Watanzania wote. Yeyote anayetaka kujimilikisha uandaaji wa katiba ni adui yetu sote. Yeyote anayetaka kutushirikisha sote kwenye kupata katiba tunayoitaka, ni mzalendo wa Taifa letu, ni mtu mwenye upendo kwa Watanzania wa leo na vizazi vijavyo, na huyo ndiye tuandamane naye.

Hatutaki katiba maslahi ya watawala au wanasiasa tu, bali katiba itakayompa mamlaka makubwa mwananchi.
"Fikiria, mpaka pesa ya wananchi, siku hizi inatajwa kuwa ni pesa ya Rais, eti Rais emetoa bilioni kadhaa kwaajiki ya ujenzi wa kisima, zahanati, shule, n.k."
 
Back
Top Bottom