sheiza
JF-Expert Member
- Sep 29, 2010
- 7,564
- 11,478
Hata kama wachache wataikataa hii ila wengi watakubali kwamba Magufuli alikuwa zawadi maalum kwa taifa la tanzania. Alikuwa ni mtu mnyonge kwa wanyonge na maskini ambao ndio wengi kwenye taifa aliloliongoza lakini alikuwa simba na mkali kwa mabeberu, mafisadi na wabadhirifu wa jasho la wanyonge.
Kutokana na uwezo wake wa akili na hulka ya kufuatilia mambo, Magufuli aliweza kuwajua viongozi na watu wa chama chake ambao angeweza kufanya nao kazi kwa mlengo wake, lakini pia aliwatambua wapinzani ambao aliamini atafanya nao kazi kwa mlengo wake na maslahi ya nchi.
Watu kama kina zitto, kina Lema, kina January, na wengineo hawakuwa na nafasi sana katika utawala wake, mfano upinzani hakuwaelewa hasa nia yao kwa nchi sababu kila walichokipigania miaka ya 2015 kurudi nyuma yeye alijaribu kukifanikisha kwa kiasi kikubwa lakini aliambulia matusi na kejeli kutoka kwa hao.
Siku zote dua ya myonge hukubalika haraka na Mwenyezi Mungu. Maisha yake ya ukaribu na makundi mbalimbali na wenye shida pia na kifo chake kilivyopokelewa ilidhihirisha kuwa Magufuli alikuwa mpango kamili wa Mungu pamoja na madhaifu kama yanavyoitwa na wachache ambapo bila kama hayo yanayoitwa hayo madhaifu angeonekana kiongozi wa hovyo kama wengine walivyoonekana au hata sasa wanavyoonekana.
Watanzania wengi tulidhani mambo yanajiendesha tu pengine kwa neema lakini sasa tumegundua bila mtu mwenye nguvu na maamuzi makali basi nchi hii watakaobaki salama ni wachache ambao ni wala asali na familia zao.
Ni mwaka sasa umepita toka mwendazake aende, alituachia nchi ikiwa salama kwa aliyekuwa tayari kuleta amani, alituachia watendaji makini kwa waliokuwa tayari kwa maslahi ya nchi. Yale yote yamepanguliwa na sasa tunayaona wenyewe.
Waliomsema na kumdhihaki wamepewa nafasi wanapwaya, tena hapo sio nchi ni idara moja tu au sekta moja tu, hao waliochiwa madaraka na kuamua kuweka utaratibu wao nao mambo yamewavurugikia hadi imefikia sasa wanalinganisha tanzania na marekani. Sijui focus yao ni nini? Hao wapinzani waliomdhihaki Magu wanazidi kuadhirika na kuonyesha walivyo waongo, wabinafsi na wanafiki.
Na kila wanapojaribu kumpiga na mawe Magu basi hali yao ya kiuongozi na upinzani kwa ujumla inazidi kuwa mbaya.
Hata sasa nafasi ya upinzani ukiangalia kwa macho ya umakini utaona unavyopoteza kuaminiwa. Mfano kulikuwa na tetesi za uanzishwaji wa chama cha Umoja, mapokeo ya hiki chama yametikisa sana kwenye medias nyingi.
Sasa ukiwa mwelevu utaliona hilo. Tujiulize tuna vyama chungu nzima vya upinzani kama Chauma, ACT, Jahazi Asilia, NRA na vinginevyo, je mbona uanzishwaji wake haukuleta muamko hivi?
Na je watu hawaviamini tena Chadema, ACT na CUF ambavyo viliaminika kama vyama vikuu vya upinzani?
Kuna baadhi ya viongozi wanatakiwa wakasafishe kaburi la Magu, vinginevyo muda utasema.
Kutokana na uwezo wake wa akili na hulka ya kufuatilia mambo, Magufuli aliweza kuwajua viongozi na watu wa chama chake ambao angeweza kufanya nao kazi kwa mlengo wake, lakini pia aliwatambua wapinzani ambao aliamini atafanya nao kazi kwa mlengo wake na maslahi ya nchi.
Watu kama kina zitto, kina Lema, kina January, na wengineo hawakuwa na nafasi sana katika utawala wake, mfano upinzani hakuwaelewa hasa nia yao kwa nchi sababu kila walichokipigania miaka ya 2015 kurudi nyuma yeye alijaribu kukifanikisha kwa kiasi kikubwa lakini aliambulia matusi na kejeli kutoka kwa hao.
Siku zote dua ya myonge hukubalika haraka na Mwenyezi Mungu. Maisha yake ya ukaribu na makundi mbalimbali na wenye shida pia na kifo chake kilivyopokelewa ilidhihirisha kuwa Magufuli alikuwa mpango kamili wa Mungu pamoja na madhaifu kama yanavyoitwa na wachache ambapo bila kama hayo yanayoitwa hayo madhaifu angeonekana kiongozi wa hovyo kama wengine walivyoonekana au hata sasa wanavyoonekana.
Watanzania wengi tulidhani mambo yanajiendesha tu pengine kwa neema lakini sasa tumegundua bila mtu mwenye nguvu na maamuzi makali basi nchi hii watakaobaki salama ni wachache ambao ni wala asali na familia zao.
Ni mwaka sasa umepita toka mwendazake aende, alituachia nchi ikiwa salama kwa aliyekuwa tayari kuleta amani, alituachia watendaji makini kwa waliokuwa tayari kwa maslahi ya nchi. Yale yote yamepanguliwa na sasa tunayaona wenyewe.
Waliomsema na kumdhihaki wamepewa nafasi wanapwaya, tena hapo sio nchi ni idara moja tu au sekta moja tu, hao waliochiwa madaraka na kuamua kuweka utaratibu wao nao mambo yamewavurugikia hadi imefikia sasa wanalinganisha tanzania na marekani. Sijui focus yao ni nini? Hao wapinzani waliomdhihaki Magu wanazidi kuadhirika na kuonyesha walivyo waongo, wabinafsi na wanafiki.
Na kila wanapojaribu kumpiga na mawe Magu basi hali yao ya kiuongozi na upinzani kwa ujumla inazidi kuwa mbaya.
Hata sasa nafasi ya upinzani ukiangalia kwa macho ya umakini utaona unavyopoteza kuaminiwa. Mfano kulikuwa na tetesi za uanzishwaji wa chama cha Umoja, mapokeo ya hiki chama yametikisa sana kwenye medias nyingi.
Sasa ukiwa mwelevu utaliona hilo. Tujiulize tuna vyama chungu nzima vya upinzani kama Chauma, ACT, Jahazi Asilia, NRA na vinginevyo, je mbona uanzishwaji wake haukuleta muamko hivi?
Na je watu hawaviamini tena Chadema, ACT na CUF ambavyo viliaminika kama vyama vikuu vya upinzani?
Kuna baadhi ya viongozi wanatakiwa wakasafishe kaburi la Magu, vinginevyo muda utasema.